Thursday, October 25, 2007

Yanga hoi kwa Simba

Kikosi cha Dar es Salaam Young Africans Sports Club (Yanga)
Matokea mechi Simba v/s Yanga kuanzia 1965-2007, hizo zikiwa ni mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara na Muungano tuNA MWANDISHI MAALUM.

DONDOO MUHIMU:

Zimekutana mara 80 Yanga imeshinda mara 29 Simba mara 26 Sare mara 25 Mabao yaliyotinga wavuni 170 Yanga imefunga 91 Simba imefunga 79

JUNI 7, 1965 Yanga v/s Sunderland (Simba), 1-0MFUNGAJI: Mawazo Shomvi dk 15

.....(Soma zaidi)


Kikosi cha Simba Sports Club ya Dar es Salaam.


Mshambuliaji mwiba wa Simba Ulimboka Mwakingwe akikata mbuga kwenda kuwaumiza Yanga baada ya kumtoka mlinzi wa Jangwani leo uwanja wa Jamhuri Morogoro ambako Msimbazi wameibuka kidedea kwa mara ingine kwa ushindi wa goli 1-0.

Na Dastun Shekidele, Morogoro

Simba ya jijini Dar es Salaam, jana, ikiwa pungufu na wachezaji 10 uwanjani, iliibuka ‘baabkubwa’ mbele ya watani wao wa jadi, Yanga Afrika, katika mchezo wenye upinzani mkali, uliofanyika kwenye Dimba la Jamhuri, Morogoro.Kiungo mwenye kasi, Ulimboka Mwakingwe ndiye aliyechoma msumari mchungu Jangwani, pale alipofunga goli la pekee kunako dakika ya 32 ya mchezo, akiunganisha krosi ya Nurdin Bakar.Katika pambano hilo, Simba ndiyo walianza mchezo vizuri, huku wachezaji wake wakionana vema, tofauti na Yanga ambao walikuwa wakijigonga kila mara walipopata mpira.Kufuatia hali hiyo, Simba walikuwa wakilishambulia lango la Yanga kama nyuki, huku wakiwafunika wapinzani wao kila idara......Soma zaidi...

No comments: