Sunday, May 18, 2008

CUF, CCM, WASUSIANA

MAZISHI, HARUSI


Na Mwandishi Wetu


ATHARI za kuparaganyika kwa mwafaka kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama Cha Wananchi (CUF) uliolenga kumaliza mpasuko wa kisiasa kisiwani Zanzibar zimeanza kujitokeza kwa kasi katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Shirikika la Utangazaji la Uingereza (BBC) leo asubuhi limeripoti habari za wakazi wa visiwa hivyo kuanza kubaguana katika shughuli za kijamii ikiwemo, misiba, harusi, kuuza na kununua bidhaa madukani pamoja na kwenye vyombo vya usafiri.

Pia limeripoti kuwepo kwa vitisho katika visiwa vya Unguja ambapo baadhi ya wakazi wenye asili ya Pemba wamedai kuwa wamekuwa wakikuta vipeperushi kibao vimebandikwa kwenye nyumba zao zao, vikiwataka warudi kwao Pemba.

Akizungumza kwa uchungu mkazi mmoja wa Unguja ambaye hakujitaja jina amesema hali hiyo imewachosha na kwamba anaona ni bora warudi Pemba kwa kuwa watakuwa hawaishi Unguja kwa usalama.

Endelea kusoma kwa kubofya hapa.

No comments: