Sunday, August 17, 2008

Apple wanaweza

Kuingia kwenye

iPhone yako na

kufuta programu



Programu iliyo kwenye iPhone imetengenezwa kiasi kwamba Apple wanaweza kuingia kwenye simu yako ya iPhone kutoa programu wanayotaka kuitoa. Hayo yamesemwa na bingwa wa simu za iPhone, Per Jonathan Zdziarski, ambaye ameandika kitabu kiitwacho "iPhone Forensic Manual" Zdziarski anasema kuwa kuna vijimashine kwenye programu OS 2.X ambavyo vinatoa nafasi kwa iPhone kupiga kwenye seva ya Apple kupitia kwenye anwani-tovuti. Lengo la vijimashine hivyo ni kuwawezesha Apple kudhibiti program zao na kufuta program ambayo hawataki iwe kwenye iPhone..

Chanzo cha habari: http://technorati.com/tag/Jonathan+Zdziarski

No comments: