Kama

si nchi,
Karume Mkuu
wa Mkoa?
MJADALA kuhusu hoja ya hadhi ya Zanzibar kama ni nchi au la, unazidi kupamba moto, na ni dhahiri kuwa hoja hii imewagawa Watanzania katika pande mbili. Wapo wanaoitaja Zanzibar kama nchi na dola kamili, na wapo wanaosema Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Tanzania, lakini bila kutuambia ni mkoa au wilaya ya Tanzania.
Hoja ya Zanzibar ni nchi au la ilianzia katika Bunge baada ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda, mara mbili kwa nyakati tofauti kusimama na kusisitiza kuwa Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Tanzania, majibu yaliyoibua mjadala na mvutano mkali kwa Watanzania wa kada mbalimbali.
Viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kimsingi wanaunga mkono matamshi ya Pinda huku wenzao wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wanampinga. Kupitia kwa Naibu Waziri Kiongozi Ali Juma Shamhuna, SMZ imesema: “Zanzibar itaendelea kuwa nchi hadi mwisho wa dunia…Na suala hili tuachiwe Wazanzibari wenyewe tulitolee maamuzi yetu, na huo ndio ukweli.”
No comments:
Post a Comment