Kama

si nchi, Tanganyika
ilijiunga na wilaya?
BABA wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alikuwa mtu mwenye kanuni ya kujikosoa. Nadhani ni kanuni hiyo iliyomfanya afe akiwa kipenzi cha wote wakiwamo hata wale ambao kwa namna moja au nyingine walibanwa na wadhifa wake.
Alikuwa akiyakiri makosa aliyoyafanya maishani mwake kama binadamu, lakini bila kukosa kuyatolea mambo yaliyosababisha kutokea kwake, sababu ambazo mara nyingi zilimlinda kwa kuonyesha kwamba hakufanya makosa husika kwa kuinufaisha nafsi yake, bali katika kujaribu kuinusuru jamii yake kulingana na hali iliyochochewa na wakati uliokuwapo.
Mara nyingi Mwalimu alikuwa anasisiza kwamba kinapoangaliwa kitu au maamuzi ni lazima kipimwe kulingana na wakati uliopo, akisema kwamba maamuzi kama ya miaka 30 au zaidi iliyopita si lazima yaendelee kuwa sahihi baada ya muda wote huo, si lazima yaendelee kusimama na uthabiti leule wakati dunia ikibadilika.
No comments:
Post a Comment