Friday, August 22, 2008



Walioiba mabilioni

ya EPA wafilisiwa


Serikali imekamata mali zote za wamiliki wa kampuni 13 kati ya 22 zilizothibitika kuhusika na uchotaji wa mabilioni ya shilingi kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), Rais Jakaya Kikwete aliliambia Bunge jana.

Alisema licha ya kuzuiwa hata kwa magari wanayomiliki watu hao, pasi zao za kusafiria pia zinashikiliwa wasikimbie nje ya nchi. Licha ya hatua hiyo, Rais Kikwete alisema ameiagiza Benki Kuu (BoT) kufunga akaunti hiyo ambayo kwa mujibu wake ina zaidi ya Sh bilioni 130 na fedha hizo ziwekwe katika mfuko mkuu wa serikali.

No comments: