
Waziri awamu ya
tatu na ya nne kortini
* Vigogo zaidi wachanganikiwa matumbo moto
* Tahadhari nzito zachukuliwa dakika za mwisho
Na Mwandishi Wetu, Dar Leo Jumanne jioni 18.11.2008
Habari za kuaminika kutoka kwa mmoja wa waendesha mashitaka katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisuti jijini Dar es Salaam zinasema kuwa alipata taarifa za kuletwa kwa waziri huyo(jina tunalo) mahakamani jana lakini suala hilo liliahirishwa dakika za mwisho.
Hata hivyo wakati tukienda mitambo, taarifa zinasema huenda waziri huyo akafikishwa mahakamani hapo mchama huu.
Taarifa hizo hazikufafanua zaidi kuwa waziri huyo atafikishwa mahakamani hapo kusomewa makosa gani.
Kufikishwa kwa kigogo huyo kutafungua sura mpya ya sakata hilo. Baadhi ya watu wamedai kwamba hatua hiyo inaweza kuwa mwanzo mbaya wa kuingia kwa msururu wa vigogo kwenye sakata hilo.
"Tunaamini akiletwa mengi yatafumka, sakata hili litachukua sura mpya, huenda ndio maana tahadhari kubwa inafanyika katika utekelezaji wake. Wengi matumbo moto" kilisema chanzo chetu.
No comments:
Post a Comment