Friday, July 03, 2009

Malezi kwa watongozaji

wazoefu ni sawa na ujasiri

wa kuku mbele ya chatu




Kwa Waziri wa Mikiki na Makeke,
Uzitoni Street,
Bongo.

POLE sana, mpenzi!

Yaani siamini! Mdogo wako kajazwa mimba? Na alivyokuwa na bidii katika masomo! Haiyumkiniki kabisa. Pole sana mpenzi na mpe pole pia mdogo wako.

Lakini niliposoma barua yako, kwa kweli nilikasirika. Nilikasirika sana. Usinielewe vingine, sikumkasirikia mdogo wako. Wangapi tumepita umri huu kwa kudra za Mwenyezi Mungu tu. Na kadiri msichana alivyo mrembo, anapewa mateso zaidi hadi anaona urembo ni laana tu.

Ndiyo! Bora kukosa shepu hadi mtu anakuwa tayari kupambana na mbwa mwitu. Hivi, kwa nini wanaume wanaona wana haki ya kututongoza full time. Hawana mapenzi hata chembe. Ni kama mchezo kwao, washindane na wenzao nani ni mshenzi zaidi wa kuwarubuni wasichana wadogo. Wanatutongoza ili watutangaze tu.....bofya na endelea kusoma>>>>>

No comments: