Dakt. Ali Mohamed Shein
Rais wa Zanzibar 2010 - 2015
Dakt. Ali Mohamed Shein, Rais mteule wa Zanzibar.
Saa 19:00 – 19:300 CET
(21:00 – 21:30 EAT)
Tume ya uchaguzi Zanzibar imetangaza matokeo ya kura za Urais wa Zanzibar. Mgombea wa CCM wa Urais wa Zanzibar, Dakt. Ali Mohamed Shein ameshinda kwa asilimia 50.1% na Maalim Seif Shariff Hamad wa CUF kwa asilimia 49,1% Wagombea wote walikuwa pamoja wakati matokoa yakitangazwa na Maalim Seif amekubali matokeo hayo. Hii inaonyesha kukua na kukomaa kwa demokrasia kwenye visiwa vya Zanzibar na kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kijumla.
National Anthem of Tanzania
Kiswahili Lyrics
Mungu ibariki Afrika
1.
Mungu ibariki Africa
Wabariki Viongozi wake
Hekima Umoja na Amani
Hizi ni ngao zetu
Afrika na watu wake.
Wabariki Viongozi wake
Hekima Umoja na Amani
Hizi ni ngao zetu
Afrika na watu wake.
Chorus:
Ibariki Afrika
Ibariki Afrika
Tubariki watoto wa Afrika.
Ibariki Afrika
Tubariki watoto wa Afrika.
2.
Mungu ibariki Tanzania
Dumisha uhuru na Umoja
Wake kwa Waume na Watoto
Mungu Ibariki,
Tanzania na watu wake.
Dumisha uhuru na Umoja
Wake kwa Waume na Watoto
Mungu Ibariki,
Tanzania na watu wake.
Chorus:
Ibariki Tanzania
Ibariki Tanzania
Tubariki watoto wa Tanzania.
Ibariki Tanzania
Tubariki watoto wa Tanzania.
English Translation
God Bless Africa
1.
God Bless Africa.
Bless its leaders.
Let Wisdom Unity and
Peace be the shield of
Africa and its people.
Chorus :
Bless Africa,
Bless Africa,
Bless the children of Africa.
2.
God Bless Tanzania.
Grant eternal Freedom and Unity
To its sons and daughters.
God Bless Tanzania and its People.
Chorus :
Bless Tanzania,
Bless Tanzania,
Bless the children of Tanzania.

6 comments:
Yaani uzalendo kitu kibaya sanaaa!!!
Kuusoma tu wimbo wa taifa nikajisikia mwili mzima unasisimka, machozi yakataka kunidondoka!!!
Mimi yalinidondoka!!!
Mwandishi wa habari hii tafadhali fanya utafiti wa kina ndipo uandike habari. Matokeo ya mshindi wa urais si hayo uliyoyaandika.
Matokeo yalitolewa na Tume ya Uchaguzi zanzibar ni kwamba
Dk. Ali Mohd Shein asilimia 50.1
Maalim Seif Sharif Hamad asilimia 49
Ndg. Alwatan, shukrani kwa taarifa zako. Sisi tumeandika hizi asilimia wakati tukimsikiliza Dakt. Ali Mohamed Shein:
http://www.ustream.tv/channel/bbc-swahili
Kama matokeo ni mengine, tunaomba kumradhi.
Ndg. Alwatan,
unaweza sikiza mwenyewe kwenye kiungo hiki:
http://www.youtube.com/watch?v=pD4YPDVDoCM&feature=player_embedded
Siku njema
Ndg. Alwatan,
Shukran jazeel kwa masahihisho yako. Tutakuwa makini siku zijazo...
Siku njema!
Post a Comment