Monday, August 12, 2013

Kwa nini Rais anyamazie siri hizi kuhusu dawa za kulevya?



 WIKI iliyopita, Rais Jakaya Kikwete aliendeleza utaratibu wake wa kulihutubia taifa takriban kila mwisho wa mwezi. Japo wakati mwingine hotuba zake huonekana kama maelezo tu ya masuala ambayo tayari wananchi wanayafahamu au pengine maelezo tu ambayo hayana majibu kwa maswali yanayowasumbua wananchi, ukweli kuwa Rais anathamini kuzungumza na taifa mara kwa mara ni jambo linalostahili pongezi.


No comments: