Monday, April 21, 2014

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo, Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha mchakato wa Katiba kwa lengo la kunusuru amani ya Taifa.


 MCHUNGAJI LUSEKELO;

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo, Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha mchakato wa Katiba kwa lengo la kunusuru amani ya Taifa.

Lusekelo alisema siyo lazima Katiba Mpya ipatikane mikononi mwa Rais Kikwete kwa kuwa hatua iliyofikiwa kwa sasa ni kubwa, hivyo inaweza kuendelezwa na Rais atakayefuatia mwaka 2015.

Akizungumza jana katika ibada ya Pasaka, Lusekelo alisema hali inayoendelea kwa sasa inajenga hofu na kuwachanganya Watanzania kutokana na hofu ya Uchaguzi Mkuu ujao.

Alisema Bunge la Katiba kwa sasa limekuwa mfano wa klabu ya pombe za kienyeji kutokana na vurugu alizodai kuchangiwa na wajumbe wa CCM.

“Hakuna majadiliano ya kujenga hoja na badala yake tunasikia matusi tu yanarushwa... uamuzi wa Profesa Ibrahim Lipumba kutoka nje ulikuwa ni sahihi. Hata mimi iwapo ningekuwa mjumbe, ningekuwa wa kwanza kutoka,” alisema Lusekelo na kuongeza:

“Kwa hiyo ni vyema mchakato ukasitishwa kwa hatua iliyofikia ili Taifa litulie na wananchi wajiandae kwa Uchaguzi Mkuu ujao.”

(Chanzo Gazeti la Mwananchi Jtatu - 21/04/2014)


No comments: