Thursday, April 26, 2007










Entrance: kr. 50,-

Time: from 20.00 til 03.30


Watanzania Mnataka Muungano wa aina gani?



LEO tunasherehekea miaka 43 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Pamoja na kula na kunywa, maadhimisho hayo yanatoa fursa nyingine kuthibitisha kuwa itakuwa vigumu sana kwa watu wenye nia ya kuuvunja Muungano huo kufanikisha azma yao.

Tumetoka mbali, tumevuka milima na mabonde. Yapo mabonde yaliyokuwa na nzige na asali, lakini kuna sehemu tumepita katika mabonde yenye miiba na mbung’o. Tumeshavuka huko, tupo hapa tulipo na la muhimu sana ni kutazama kule tuendako.

Tutalazimika pia kutazama tutokako kwa nia ya kuangalia tulipojikwaa, kwamba tulifanikishaje kuondokana na kikwazo kilichotukwaza.

Wakati tunasherehekea miongo minne hii na ushehe, ni vema kujiuliza kama si Watanzania wenyewe, Muungano utaimarishwa na nani? Kwa hakika, kila mmoja anafahamu kuwa hakuna mwenye jukumu hilo zaidi ya Watanzania.

Lakini wakati tunasherehekea miaka 43 ya Muungano, ni vema tukajiuliza nafasi ambayo Watanzania (hawa wa kawaida) wamepewa katika kuusuka Muungano huo. Na tunapoliangalia suala hilo, ni vema kuanzia mwanzo wa Muungano.

Lakini ni vema kuweka wazi kuwa, kufanikisha kuunganisha Tanganyika na Zanzibar wakati ule, tena katika mazingira ambayo wananchi wa kawaida hawakushirikishwa kikamilifu, ulikuwa ni uthibitisho tosha kuwa watu wa nchi hizo mbili walikuwa na udugu wa karibu mno. Ingekuwa ni ndoto kuweza kuwaunganisha watu ambao mahusiano yao si ya karibu.

Ukaribu huo bado ungalipo, na ndio silaha kubwa ambayo inaweza kutumika kuimarisha Muungano. Hofu isiwekwe juu ya kauli zinazotolewa na kuziona kana kwamba zinatishia au zinaashiria kutaka kuuvunja Muungano.

Kwa miaka hii yote, imejidhihirisha kuwa hakuna mwenye nia ya kuuvunja Muungano. Kama angelikuwepo, tayari angekuwa ameshajitokeza, au yale anayoyakusudia yangekuwa yameshaonekana waziwazi. Hata kama mtu kama huyo atajitokeza leo hii, tunajivuna kuwa tuna kila silaha ya kumdhibiti. Iwapo vyombo vinavyohusika vitashindwa kufanya hivyo, wananchi wa kawaida watamdhibiti, kwa sababu wanafahamu umuhimu wa Muungano huo.

Pamoja na matatizo yake, Muungano umedumu kwa zaidi ya miongo minne, na hakuna dalili kwamba utavunjika. Hivyo, ni upuuzi kudai leo kuwa, kuujadili Muungano ni kuleta chokochoko zenye lengo la kutaka kuuua.

Au kudai kwamba lipo kundi la watu ambao wana nia ya kuua Muungano. Kama kundi hilo lingekuwepo, lilikuwa na nafasi ya kufanya hivyo na kufanikiwa kirahisi katika miaka ya mwanzo ya Muungano, ambako ulikuwa haujapata mizizi ya kutosha na si leo ambako upeo wa uelewa wa Watanzania umepanuka sana.

Wakati leo tunatafakari na kujadili kile kinachoitwa kero za Muungano, tunapaswa pia kuangalia ushiriki wa Watanzania wa kawaida katika kuimarisha Muungano. Hili ni muhimu kwa sababu ili Muungano uwe imara na wa maana zaidi, unapaswa kuwa wa watu, hawa wa kawaida. Muungano unapaswa kuwanufaisha watu hao la sivyo, hautaonekana kuwa na maana yoyote na hakika hautadumu.

Ndio, watu ndio kiini cha Muungano huu. Tusipowaangalia vizuri, hawa ndio wanaoweza kuuvunja Muungano kwa sababu ni wao. Tusiwaangalie wanasiasa wala wapambe wao, tuwaangalie Watanzania wa kawaida na kuona ni jinsi gani Muungano umefanikisha kuboresha maisha yao, kwani hilo ndilo wanalolihitaji.

Tuangalie jinsi Muungano ulivyomnufaisha mwananchi wa kawaida kwa nia ya kufanya marekebisho katika sehemu ambazo zinaonekana kuwa ushiriki wa mtu wa kawaida haujawa mzuri.

Ni hatari sana kuwa na Muungano ambao hauna mashiko miongoni mwa watu ambao umekusudiwa kuwaunganisha. Tutakuwa na Muunganoi legelege ambao utadumishwa kwa nguvu za viongozi na si matakwa ya wananchi.

Na tunapofanya zoezi hilo, tujitahidi kuhakikisha kuwa mwananchi huyo anahusishwa ipasavyo. Tusirudie makosa yaliyopita ya viongozi kukaa na kuamua wamfanyie nini mwananchi huyo. Kufanya hivyo kunaweza kuwa kulifanikiwa mwaka 1964 kutokana na sababu zilizokuwepo wakati huo.

Kwanza inawezekana kuwa hatukuwa na rasilimali za kutosha kuwauliza Watanzania kuhusu aina ya Muungano wanaoupendelea. Pia inawezekana kuwa, upeo na uelewa wa Watanzania wakati huo, usingewawezesha kufanya kile Wazungu wanachokiita ‘informed decision’.

Hali ni tofauti leo hii. Kama tunaweza kuvumilia matumizi ya ziada yanayofikia sh bilioni 900, sidhani kama tunaweza kuumia iwapo tutaamua kwa makusudi kutumia bilioni chache kuwauliza Watanzania nini wanakitaka katika Muungano wao.

Leo hii uelewa wa Watanzania ni mzuri sana, hivyo wapo katika nafasi nzuri ya kufanya ‘informed decision’ kuliko ambavyo ilikuwa mwaka 1964.

Tusiogope kwamba watatoa mawazo ambayo utekelezaji wake utageuza aina ya Muungano tulionao, ambao baadhi ya watawala wanadhani kuwa ni aina fulani ya msahafu. Tuwape nafasi Watanzania hawa waeleze aina ya Muungano wanaoutaka na iwapo matakwa yao yatatimizwa, tutaibuka na Muungano imara ambao watawala hawatakuwa na kazi kubwa kuutetea kwa wananchi kama ilivyo sasa.

Kwa hakika, maoni ya Watanzania ndiyo yatakayotuwezesha kuboresha Muungano. Iwapo watawala watayaogopa maoni yao, watakuwa wanawalazimisha kufuata vile ambavyo watawala hao wanataka. Sidhani kama tutakuwa tunajenga Muungano wenye nguvu na mashiko.

Zipo hoja mbalimbali zimetolewa kuhusu Muungano. Nyingi kati ya hoja hizo, zimekuwa zikigusia matatizo yaliyopo katika Muungano huo. Yapo matatizo yanayotokana na hulka binafsi za viongozi, lakini kubwa ambalo linapaswa kupewa kipaumbele katika harakati za ujenzi wa Muungano imara, ni muundo na mfumo wa Muungano.

Muundo na mfumo ndio unaotoa dira ya namna Muungano utakavyofaa kuwa chombo cha kuwasaidia wananchi ambao wameamua kuungana. Kukwepa kulizungumzia hili, au kuwatisha wale ambao wanaliibua suala hili, ni sawa na kufagia uchafu ndani na badala ya kuuzoa na kwenda kuutupa jalalani, unauficha chini ya kapeti!

Hakuna hatari wala dhambi kujadili iwapo unaotufaa ni Muungano wa serikali mbili kama tulionao, au tuwe na serikali tatu, au tuwe na serikali moja. Tena mjadala kuhusu suala hilo unapaswa kuwa mpana sana.

Kama ilivyodokezwa awali, upeo wa uelewa wa Watanzania hivi sasa utatuwezesha kupata mawazo murua ambayop iwapo yatafanyiwa kazi bila kuangalia nani katoa wazo, tutafanikiwa kujenga Muungano ambao utakuwa bora kuliko huu tulionao.

Si kwamba Muungano tulionao si bora, lakini matatizo yaliyojitokeza, ambayo wengine wameyabatiza jina la ‘Kero za Muungano’, yanaonyesha wazi kuwa bado Muungano wetu haujakaa katika mstari ulionyooka.

Tutakuwa tunafanya dhambi kubwa sana iwapo tutaendeleza hali iliyoanza kujitokeza ya makundi mbalimbali, wanasiasa wakiongoza, kuanza kuutumia Muungano kama kete ya kushinikiza hoja zao.

Pamoja na siasa, Muungano utakuwa na maana sana iwapo utawasaidia Watanzania kujiinua kiuchumi na kijamii. Maendeleo katika nyanja hizo yatasaidia kuimarisha siasa na demokrasia kama tunavyolenga.

Ni vema kuonya kuwa mjadala huo hautamaanisha kuwa tunaachana na mfumo wa Muungano wa serikali mbili uliopo. Mjadala utatusaidia, iwapo tutaamua kuendelea na serikali mbili, kuibua mambo ambayo yanaufanya mfumo huo uzae matatizo ambayo yapo sasa.

Mjadala ulenge katika kuibua matatizo yaliyopo na mbinu madhubuti ya kukabiliana na kuyatatua matatizo hayo. Kuendelea kung’ang’ania kuwa mfumo wa serikali mbili ndio muafaka, bila kuangalia matatizo yaliyopo yanasababishwa na nini na tutawezaje kuyatatua, ni kuendelea kukalia bomu ambalo utambi wake unaendelea kuungua taratibu.

Kuna uwezekano mkubwa kuwa sababu zilizowafanya waasisi wa Muungano kuona umuhimu wa kuweka serikali mbili, hazipo tena leo hii, kwamba umuhimu wa serikali mbili katika Muungano umepitwa na wakati. Kuna dhambi gani kulijadili hili na kuliweka katika muktadha unaofaa?

Kama ilivyopatwa kuelezwa, asilimia kubwa ya Watanzania walio hai leo, wamezaliwa baada ya Muungano. Wamezaliwa wakiikuta Tanzania na si Tanganyika na Zanzibar kama ilivyokuwa kabla ya Muungano.

Lakini wameenda shule na huko wamefundishwa kuwa kabla ya kuwa Tanzania, kulikuwa na nchi mbili na viongozi wake wakakubaliana kuziunganisha ili kupata nchi moja. Kulikuwa na misingi ya makubaliano hayo na pia misingi ya Muungano huo. Wengi wanajua tu kwamba Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Karume walikubaliana kuunganisha nchi zao, lakini wachache sana wanajua misingi hasa ya makubaliano baina na Nyerere na Karume.

Watu wachache pia wanafahamu misingi ya Muungano na ndio maana leo hii, upotoshaji umekuwa mwingi kuliko ukweli halisi kuhusu Muungano.

Mjadala uliopanuliwa kuhusu Muungano, utasaidia kutoa fursa kwa ukweli kuhusu Muungano kuhubiriwa na kueleweka miongoni mwa Watanzania wengi ambao Muungano wamekuwa wanausoma tu kwenye vitabu na kuusikia katika masimulizi ya watu wachache ambao waliushuhudia.

Katika moja ya hotuba zake maarufu, Mwalimu Nyerere aliwahi kubainisha kuhusu hatari ya Muungano kuvunjika kutokana na uchoyo tu wa baadhi ya viongozi. Hali ya mambo inaonyesha kuwa, kauli ya Nyerere kuwa Wazanzibari wanaweza kujitenga tu kwa kuvutwa na Uzanzibari wao, bado haijafanyiwa kazi ipasavyo.

Lakini hali ya mambo inatulazimisha twende mbali zaidi ya hapo. Katika hotuba hiyo, Nyerere alisema kuwa watakapofanikiwa kujitenga kutokana na msukumo wa Uzanzibari wao, watakuja kubaini kuwa kumbe wao si wamoja kama walivyodhani na kwamba kilichokuwa kinawafanya wajione wamoja ni Muungano.

Tetesi za mipango ya kuundwa kwa Jamhuri ya Watu wa Pemba, inaweza kuwa ndio mwanzo wa utimilifu wa unabii wa Mwalimu Nyerere. Tunafanya nini kukabili hilo? Kuendelea kukaa na kusubiri matatizo yajisuluhishe yenyewe, au kutanguliza siasa wakati tunatafuta mbinu za kuyatatua, ni kujichimbia kaburi polepole.

Tunapouangalia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964, ni wakati muafaka kuangalia jinsi nchi inavyotishiwa na mmomonyoko kutokana na tofauti za kikabila, kidini na kadhalika. Hata kama tutaendelea kukataa, hayo yapo. Watanzania wa leo si wamoja kama walivyokuwa miaka michache iliyopita.

Ushahidi mojawapo ni kupanuka kwa pengo kati ya matajiri na masikini. Huu ni ufa ambao Mwalimu Nyerere aliwahi kuugusia pia, lakini tunajifanya vipofu na kushindwa kuuona kuwa ni moja ya matatizo yanayoukabili Muungano wetu.

Huu ushujaa wa kuyafumbia macho matatizo haya, ambayo yapo bayana, utakuja kutufikisha pabaya.

pnyanje@yahoo.com

Makala ya Peter Nyanje wa gazeti la Tanzania Daima.

Wednesday, April 25, 2007

Women to blame


Every other Norwegian man believes that flirtatious women have themselves to blame if they are raped.


The shock results appear in a report compiled by Amnesty in cooperation with Reform - resource center for men.

One in five men surveyed said that a woman known to have several partners is fully or partly responsible if sexually assaulted, and 28 percent believed that a woman who dresses sexily is wholly or partly responsible for a sexual assault.

"I think the results of this study are frightening. I am the father of a teenage girl. It is disturbing to see that Norwegian men believe she is responsible if she should be assaulted after flirting with a man," John Peder Egenæs, secretary general of Amnesty International Norway told newspaper VG.

Fully 48 percent of those surveyed believe that women are fully or partly responsible for a sexual assault if they openly flirt before the attack.

"It is unacceptable to blame women who have been exposed to sexual assault and violence. This confirms that female-hostile attitudes are alive and well," said victim's legal counsel Trine Rjukan.

Prime Minister Jens Stoltenberg said he was disappointed over Norwegian men's attitude towards women and found the study's results frightening.

"I had hoped and believed that we had come further than that in terms of men's view of violence against women," Stoltenberg said.

Source: (Aftenposten English Web Desk/NTB)


Tanzania beefs up anti-corruption law


NAIROBI, April 23 (Reuters) - Tanzania has passed a new anti-graft law giving corruption fighters in the east African country more power to target areas like government procurement and money laundering, a minister said on Monday. Stamping out graft has been among President Jakaya Kikwete's top priorities since he came to power in late 2005. The new legislation gives the state-run Prevention and Combating Corruption Bureau the power to seize assets from the guilty.

"The most weighted (crimes) deal with grand corruption like procurement, money laundering and corruption in auctions," Philip Marmo, minister of state for good governance in the president's office, told Reuters by phone from Dar es Salaam. The law, approved by parliament last week, will come into force with Kikwete's assent, he said, probably within a month. Denmark cut aid worth $3.16 million to Tanzania late last year over delays passing the new legislation. The government countered that it needed time to conduct public consultations.

Source: Reuters

Thursday, April 19, 2007

Rare journey underground


King Harald (left) and Austrian President Heinz Fischer seemed to enjoy their tour of the new underground train immensely.PHOTO: Håkon Mosvold Larsen / SCANPIX



Margit Fischer and Queen Sonja admiring the new underground train.
PHOTO: Håkon Mosvold Larsen / SCANPIX



King Olav, right, photographed trying to pay for his ticket on the Holmenkoll line to go skiing. King Olav traveled by T-bane in 1973 during the oil crisis, out of solidarity with the public.
PHOTO: Martinsen, Jan A.
___________________

King Harald took Austrian President Heinz Fischer on the maiden run of Oslo's new underground train (T-bane) at Stortinget (Parliament) station on Wednesday, 18th April.

This is the first time King Harald has taken a visiting head of state underground, and also marked the first official visit by the King himself on an underground train. The trip underground was to show President Fischer the new Porsche-designed carriages produced by Siemens in Austria. The president received the honor of christening the first train set, which was given the name Wien (Vienna).

Queen Sonja and the president's wife, Margit Fischer, were also present at the ceremony, which featured Viennese music and themed refreshments. The queen enjoyed herself so much that she said she wanted to travel by underground in the future. "The underground train is a symbol of a modern city. These elegant carriages can bring us from the center and out to unspoiled nature in a half an hour - this is what we call quality of life," said city council leader Erling Lae.

The Austrian president and King Harald appeared to have become good friends during the first days of the state visit, and the pair sat together and laughed and joked as they toured the station area. They were both presented with a model of the new underground train carriages.

The press finally got their long-awaited picture of King Harald on the T-bane - photos of both his father and his son on the underground already exist.

Source: (Aftenposten English Web Desk/NTB)

Wednesday, April 11, 2007










Entrance: Kr. 50,-

Time: 20.00 til 03.30


MANCHESTER UNITED pulled off one of the greatest triumphs of their rich European history - 7-1 against Roma


Cristiano Ronaldo (left) and Allan Smith flirted with a hat trick as Man Utd posted the second-largest win in the history of Champions League.

Euro glory for Blues and ManU.

MANCHESTER UNITED pulled off one of the greatest triumphs of their rich European history - 7-1 against Roma - while Michael Essien thumped Chelsea's stoppage-time winner in Valencia.

HOW ACTION UNFOLDED:

Michael Carrick needed just 11 minutes to put United level on aggregate at 2-2.

Cristiano Ronaldo jinked in from the right to slip a short pass that Carrick met with a flashing curler inside the near post from 25 yards. Stunned keeper Doni - yards off his line and perhaps responding a little slowly - could merely throw up his arms in despair as the ball dipped over him.

Gabriel Heinze and Ryan Giggs combined just five minutes later to put Alan Smith through for a thumping finish that defied the fact his last goal was in November 2005.

And it was 3-0 on 19 minutes when Wayne Rooney sidefooted Giggs' right-wing cross into the far corner.

Ronaldo fired the goal his performance deserved a minute before the break, surging in from way out on the right before hitting a firm right-footer inches inside the near post. Again, though, Doni's positioning was slightly dubious.

Brilliant winger Ronaldo poked home United's fifth on 49 minutes after Giggs slotted a deep centre from the left.

Carrick smashed the best goal so far on the hour, drilling a 25-yarder into the far top corner after Heinze retrieved Ronaldo's centre.

Daniele De Rossi volleyed a Roma response that was almost as good, albeit completely in vain, as he swivelled from 15 yards to drill in Fracesco Totti's 69th minute cross.

Twelve minutes later, though, Patrice Evra made it 7-1 12 minutes later, screwing his first ever goal in Europe inside the near post from the edge of the area.

ALEX FERGUSON'S REACTION

The United chief said: "It was a fantastic performance. The play, penetration, absolutely superb.

"Alan Smith deserved it more than anyone. He's been patient. He's trained like a beast.

"We can't wait for the semi-finals now."

Man U: Van der Sar, Brown, Ferdinand, Heinze, O'Shea, Ronaldo, Fletcher, Carrick, Giggs, Rooney, Smith. Subs: Kuszczak, Evra, Solskjaer, Dong, Richardson, Cathcart, Eagles.

Roma: Doni, Panucci, Mexes, Chivu, Cassetti, Wilhelmsson, De Rossi, Taddei, Pizarro, Mancini, Totti. Subs: Curci, Faty, Defendi, Ferrari, Vucinic, Rosi, Okaka Chuka.

Referee: Lubos Michel (Slovakia)

Sent in by Pwagu na Pwaguzi: pwagu.na.pwaguzi@oslo.online.no


Monday, April 09, 2007

Fishermen catch big, old Alaska rockfish


This March 2007 photo shows Dr. Chris Wilson of NOAA's Alaska Fisheries Science Center in Seattle, Wash., holding a ruler up to a giant shortraker rockfish.

44-inch, 60-pound female shortraker believed to be 100 years old

NCHORAGE, Alaska - A commercial fishing boat hauled in what may have been one of the oldest creatures in Alaska — a giant rockfish estimated to be about a century old.

The 44-inch, 60-pound female shortraker rockfish was caught last month by the catcher-processor Kodiak Enterprise as it trawled for pollock 2,100 feet below the surface, south of the Pribilof Islands in the Bering Sea.

The Seattle-based vessel, owned by Trident Seafoods, pulled up an estimated 75 tons of pollock and 10 bright-orange rockfish.

Scientists at the National Oceanic and Atmospheric Administration at the Alaska Fisheries Science Center in Seattle measured, photographed and documented the fish. They removed an ear bone, the otolith, which contains growth rings similar to rings in the trunks of trees.

They estimate the rockfish was 90 to 115 years old.

That's toward the upper end of the known age limit for shortraker rockfish, said Paul Spencer of the science center. Other estimates put the fish's maximum age at 157 years, Spencer said.

The contents of the rockfish's stomach were examined and scientists took tissue samples to measure her reproductive potential. "The belly was large," Spencer said. "The ovaries were full of developing embryos."

Scientists said the specimen is not the biggest on record. A 47-inch shortraker rockfish was recorded, according to the book "Fishes of Alaska."

Source: http://www.msnbc.msn.com/id/17979900/

Askofu adai orodha ya vigogo wa unga

MIEZI kadha baada ya vyombo vya habari kuripoti kuwepo kwa orodha ya wanaodaiwa kuwa ni wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya, kiongozi mmoja wa kidini nchini, ameitaka serikali kuiweka wazi orodha hiyo. Ombi hilo lilitolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam, Valentino Mokiwa, kupitia mahubiri yake katika Ibada ya Ijumaa Kuu, iliyofanyika kitaifa katika Kanisa la Mtakatifu Albano jijini Dar es Salaam, jana.

Askofu huyo alisema vita dhidi ya dawa za kulevya inapaswa kutiliwa mkazo kwa sababu ina madhara makubwa, si tu kwa watu binafsi, bali hata kwa uchumi wa nchi. Alisema taarifa za vyombo vya habari za kuwepo kwa orodha hiyo, ya watu wanaodaiwa kuwa ni vigogo wa biashara ya dawa za kulevya, ilikuwa ni sehemu nzuri ya kuanzia vita dhidi ya dawa hizo. Alisema kwa mujibu wa vyombo vya habari, orodha hiyo ilihusisha baadhi ya wabunge, maaskofu na wachungaji na ilidhaniwa kuwa mwisho wa siku itawekwa hadharani, lakini hadi leo majina hayo hayajawekwa hadharani.

“Vita ile imeishia wapi? Ina maana hatuwapendi wanaokufa na madawa hayo? Ina maana na sisi viongozi wa dini tunahusika? Mbona majina hayo hayatangazwi? Lakini imekuwa ni kawaida kutangaziwa kila dawa hizo zinapokamatwa viwanja vya ndege au katika maeneo mengine bila kuwataja wahusika wakuu,” alisema Askofu Mokiwa.

Askofu huyo alisema athari ya dawa hizo ni kubwa kwa watu wanaopata matatizo ya akili, ambao aliwaita ‘mazezeta’ wanaongezeka, familia zinaathirika. Alisema yeye kama kiongozi wa kidini, angefurahi iwapo taarifa hiyo ingeanikwa hadharani kabla hajafa. “Athari ya madawa haya ni kubwa kwa kuwa mazezeta wanaongezeka na aibu ni kubwa katika familia, hivyo nitafurahi kabla mimi sijafa nikaipata hiyo orodha. Hata ikiwa kesho nitafurahi,” alisisitiza Askofu Mokiwa.

Alisema Tanzania hakuna viwanda vya kutengeneza dawa za kulevya, hivyo ni dhahiri kuwa zinaingizwa kwa wingi hapa nchini kutoka nje. Askofu huyo alisema kwa kuwa serikali ina jicho kubwa na mikono mirefu, alidhani kuwa ingechukua hatua zinazofaa kisheria kulimaliza tatizo hilo kabisa bila hofu. Aidha, askofu huyo alizungumzia pia tatizo la ujambazi na uvunjaji wa sheria, ambalo alisema ni eneo linaloacha majeraha mengi kwa Watanzania.

Katika mahubiri yake, Askofu Mokiwa aligusia kuhusu taratibu za umilikaji silaha, akionyesha wasiwasi kuwa huenda silaha nyingi zinazotumika katika ujambazi, ni zile zinazomilikiwa kihalali. “Serikali ifikirie upya umiliki wa silaha hizo, ikiwezekana tunaiomba ifunge kabisa maduka yanayouza silaha,” alisema Askofu Mokiwa. Alizungumzia pia vurugu katika taasisi za kidini na kubainisha kuwa, kumekuwepo na vurugu katika jamii ya Wakristo nchini, jambo ambalo limekuwa likisababisha uvunjaji wa amani makanisani.

“Wakristo mara zote wametafuta punda wa lawama kwa kutaja dini fulani ndiyo chanzo cha migogoro. Wakristo tumekuwa tukijidanganya kwa hali ya sasa, viburi vya kiroho vimeongezeka, kugombea uongozi, uinjilisti wa kuibiana Wakristo, siasa chafu kanisani, kupiga viongozi wa kiroho hata kuvunja fimbo ya uchungaji,” alisema Askofu Mokiwa.

Awali, alisema kuwa kizazi cha sasa kimejaa ukaidi kwani katika historia ya uumbaji, kizazi cha sasa ndicho kinachojulikana kwa vituko na uasi. “Kinachotafuna kanisa hivi sasa ni roho ya unafiki ndani ya kanisa. Kanisa limejaa idadi kubwa ya mapadri, wachungaji na maaskofu ambao ndio chanzo kikubwa cha kuharibu kanisa,” alisema. Alibainisha kuwa, hali hiyo ndiyo inayorudisha nyuma maendeleo ya injili.

na Lucy Ngowi

By Habari Tanzania | Published 07/04/2007


Saturday, April 07, 2007

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 31 MACHI, 2007


Picha kutoka http://www.kikweteshein.com

Utangulizi

Ndugu Wananchi;

Leo katika hotuba yangu ya mwisho wa mwezi huu wa Machi, nitazungumzia mambo mawili. Nayo ni: Utoaji mikopo ya wajasiriamali wadogo wadogo na hali ya ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa na jitihada tunazozifanya kukabiliana nao.

Ndugu Wananchi;

Kabla ya kufanya hivyo, napenda kuitumia nafasi hii kutoa mkono wa heri na pongezi kwa ndugu zetu Waislamu na Wakristo hapa nchini. Kwa Waislamu nawatakia heri na fanaka tele katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa Mtume Muhammad S.A.W. Na kwa ndugu zao Wakristo nao nawatakia heri na fanaka tele katika sikukuu ya Pasaka ambayo ni kumbukumbu ya mateso, kifo na kufufuka kwa Bwana Yesu Kristo.

Wakati nikiwatakia heri katika sikukuu hizi muhimu kwetu sote Watanzania, napenda kusema kuwa naungana nanyi katika sherehe hizo। Ni matumaini yangu kuwa sherehe hizo zitakuwa tulivu na salama. Napenda kuwahakikishia kuwa vyombo vyetu vya usalama vitafanya kila linalowezekana kulinda usalama wa Watanzania na mali zao wakati wote wa sherehe hizi.

Mikopo ya Uwezeshaji Wajasiriamali

Ndugu Wananchi;

Mwezi Januari mwaka huu Serikali ilianza kutekeleza mpango wake wa mikopo ya uwezeshaji wa wajasiriamali wadogo wadogo nchini. Mpango huo unalenga kuwasaidia wananchi wa kawaida waweze kupata mikopo kwa masharti nafuu.

Shabaha yetu ni kuwa, kupitia mikopo hiyo wakopaji wataweza kuanzisha au kuendeleza shughuli za uzalishaji mali na huduma ambazo zitawapatia kipato zaidi na hivyo kuinua hali zao za maisha na kupunguza umaskini. Mikopo hiyo itawasaidia wananchi vijana na wanawake waweze kupata ajira kwa njia ya kujiajiri wenyewe.

Ndugu Wananchi;

Katika utekelezaji wa mpango huu, tuliamua kuwa kazi ya kutoa mikopo kwa niaba ya Serikali itafanywa na Mabenki ya Biashara, Benki za Wananchi na Asasi zinazotoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo. Kwa ajili hiyo Benki za Biashara za NMB na CRDB ziliteuliwa pamoja na Benki za Wananchi za Dar es Salaam, Mwanga na Mufindi na Benki ya Posta. Kadhalika asasi zinazotoa mikopo midogo midogo kwa wajasiriamali wadogo wadogo nazo zitahusishwa. Mpaka sasa shilingi bilioni 10.5 zimekwishatolewa kwa mabenki ya NMB na CRDB, kila moja ikipata shilingi bilioni 5.25. Shilingi bilioni 10.5 zilizosalia za kupewa Benki za Wananchi, Benki ya Posta na asasi zinazotoa mikopo midogo midogo kwa wajasiriamali wadogo bado hazijatolewa. Benki Kuu inaendelea kushughulikia suala hilo.

Kwa upande wa fedha zilizopokelewa benki za NMB na CRDB maelewano yalikuwa kwamba benki hizo zitatoa na kukopesha fedha yao ambayo itakuwa mara tatu ya zile walizopewa na Serikali। Kwa ajili hiyo basi benki hizo zitakopesha shilingi bilioni 31 badala ya zile shilingi bilioni 10.5 tu zilizotolewa na Serikali. Zile fedha za Serikali zitabakia kama dhamana kwa mikopo itakayotolewa na mabenki hayo.

Mafanikio Yameanza Kupatikana

Ndugu Wananchi;

Tayari Benki za NMB na CRDB zimeanza kutoa mikopo kwa wananchi mmoja mmoja na vyama vya kuweka na kukopa. Kwa mfano, hadi kufikia tarehe 23 Machi, 2007 benki ya NMB ilikwishatoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 1.419 kwa mikoa yote ya Tanzania Bara isipokuwa Ruvuma na Rukwa. Katika zoezi hilo waombaji 2,013 nchini kote wamepatiwa mikopo.

Kwa upande wa Benki ya CRDB kiasi cha shilingi 397,660,000 kilikuwa kimeshakopeshwa kwa SACCOS nane zenye wajasiriamali 1,160. Wakati huo huo shilingi 725,660,000 za kukopeshwa SACCOS tatu zenye wajasiriamali 1,441 zilikuwa zinasubiri kibali cha Makao Makuu ya Benki hiyo.

Ndugu Wananchi;

Watu wengi binafsi, vikundi vingi na SACCOS nyingi zimejitokeza kuomba mikopo. Benki ya NMB imepokea jumla ya maombi 59,974 yenye thamani ya shilingi bilioni 105.2. Benki ya CRDB nayo imepokea maombi yenye thamani ya shilingi 8,070,382,,000 kutoka SACCOS 42 zenye wajasiriamali 17,454.

Ni wazi kuwa thamani ya maombi yaliyopokelewa na Benki ya NMB ni kubwa zaidi, kwa takriban mara saba, ikilinganishwa na shilingi bilioni 15 zilizotengwa na benki hiyo kwa ajili ya mikopo ya uwezeshaji katika awamu ya kwanza ya utekelezaji.

Ndugu Wananchi;

Kutokana na maombi kuwa makubwa kuliko uwezo uliopo Benki hiyo imeamua kusitisha upokeaji wa maombi mapya ya mikopo. Wameamua kuwa kwa sasa wafanye kazi ya kushughulikia maombi yaliyokwishapokelewa ambayo nayo hawataweza kuyatosheleza yote.

Naamini sababu zao ni za msingi kabisa kwani hakuna maana kuendelea kupokea maombi mapya wakati hata yale waliyonayo yamekwishazidi uwezo wao. Benki ya CRDB ndiyo bado ina uwezo wa kuendelea kupokea mikopo. Wao hawajafikia ukomo wa fungu lao walilotenga.

Ndugu Wananchi;

Taarifa zinaonyesha kwamba baadhi ya mikoa imeweza kuwasilisha maombi mengi na kuna baadhi ya wilaya hakuna maombi yaliyowasilishwa kabisa. Wakati mabenki yanaendelea kupitia maombi waliyopokea Serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu zoezi hili ili kuhakikisha kuwa malengo yetu kwa kila mkoa kupata mgao wake wa mikopo yanatimizwa.

Vile vile, tutazungumza na mabenki ili kutafuta njia za kuhakikisha kuwa wananchi wa zile wilaya ambazo wanachelewa kuwasilisha maombi hawapotezi kabisa fursa hii। Serikali pia, itajaribu kuzungumza na mabenki ili kuona namna ya kuhudumia SACCOS katika wilaya ambazo benki ya CRDB haipo na NMB haitakuwa tayari kufanya hivyo.

Malalamiko na Matatizo

.Ndugu Wananchi;

Natambua kuwepo malalamiko na matatizo kadhaa kuhusu mikopo ya wajasiriamali ambayo ningependa kuyazungumzia leo. Kwa mfano, nilipokuwa wilayani Ngorongoro wiki chache zilizopita wananchi wa wilaya hiyo walitaka kujua hatima yao itakuwaje kwani watu wote wamechelewa kuwasilisha maombi ya mikopo wakati Benki ya NMB inasimamisha kupokea maombi mapya. Nilitoa majibu ambayo ningependa kuyarudia tena leo kwa manufaa ya wilaya zenye matatizo kama haya.

Ni makusudio ya Serikali kuona kuwa watu wa kila mkoa na kila wilaya nchini wanapata mikopo hiyo. Hivyo basi, pamoja na Benki ya NMB kusimamisha kupokea maombi kwa sasa, hapana budi utaratibu ufanywe ili, wilaya ambazo wananchi wake hawakuwahi kuwasilisha maombi ya mikopo nao wapate fursa hiyo.

Haiwezekani na wala haikubaliki kuwepo wilaya hata moja nchini ambayo watu wake hawatapata fursa ya kupata mikopo hii. Ikitokea hivyo dhamira ya kuanzisha mpango wa mikopo hii nchini itakuwa haikufikiwa.

Ndugu Wananchi;

Kumekuwepo pia malalamiko kuhusu utaratibu wa kupokea maombi, kuyashughulikia na kutoa mikopo. Zipo hisia kuwa utaratibu ni mgumu mno, mlolongo ni mrefu na kwa sababu hiyo kuna usumbufu na inachukua muda mrefu mno kwa mtu kupata mkopo.

Ni jambo jema kuwa na utaratibu wa kufanya mambo lakini ni vyema utaratibu ukawa rahisi na kwamba haichukui muda mrefu kutekeleza jambo. Hatuna budi basi kuuangalia upya utaratibu wetu wa sasa na kufanya marekebisho pale panapostahili ili mambo yaende vizuri. Yaani, iwe rahisi kwa waombaji kuomba na ichukue muda mfupi kwa waombaji kupata majibu na kupewa mikopo kwa wale watakaokubaliwa.

Ndugu zangu, Watanzania wenzangu;

Pamoja na kusema hayo sina budi kusisitiza kuwa baadhi ya taratibu zilizowekwa ni muhimu kuwepo. Zina manufaa yake. Kwanza, zinasaidia kuhakikisha kuwa mikopo inawafikia walengwa. Hii ni mikopo ya raia Watanzania na ni mikopo ya maskini ili kuwawezesha wainue hali yao ya maisha. Si mikopo ya matajiri, wao mabenki yapo, tena yamejaa mabilioni ya fedha zinazosubiri wakopaji kama wao wawapatie.

Pili, taratibu hizo zinasaidia kuhakikisha kuwa fedha zilizokopeshwa zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na mikopo inalipwa। Mathalan, itasaidia kuhakikisha kuwa mtu aliyeomba mkopo wa kulima bustani ya nyanya hatatumia pesa hizo kumalizia nyumba yake au kulipia ada ya mwanae. Ni mambo ya maana, lakini siyo makusudio ya mkopo. Kama watu wataachwa wafanye hivyo mikopo haitalipwa na mtaji huu wote utakufa. Tukifikia hali hiyo dhamira yetu ya kuwa na utaratibu endelevu haitafikiwa. Itakuwa ni hasara kubwa ambayo ni lazima tuhakikishe kuwa hatufiki hapo.

Utaratibu Uzingatiwe

Ndugu Wananchi;

Utaratibu wa kuomba na kutoa mikopo unasisitiza mambo makuu yafuatayo: Kwanza, sharti muombaji awe na mradi unaokopesheka. Mwombaji awe na shughuli ya uzalishaji mali au utoaji huduma anayoiombea mkopo. Shughuli hiyo lazima ithibitike kuwa inafaa kupewa mkopo kwa kupitia taratibu zilizowekwa.

Pili, muombaji apitishe fomu zake za maombi kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa au Kijiji atakapofanya hiyo shughuli ili wamtambue na wautambue mradi.

Tatu, maombi yachambuliwe na Kamati ya Maendeleo ya Kata. Kamati hiyo itatoa maombi yake kabla maombi hayo hayajawasilishwa Benki kwa uamuzi wa mwisho.

Kwa upande wa SACCOS wanachama wanatakiwa kuwasilisha maombi yao kwa uongozi wa SACCOS yao kwa uchambuzi. Uongozi wa SACCOS ukiridhika huwasilisha maombi hayo kwa Afisa Ushirika wa Wilaya ambaye huthibitisha uhai wa SACCOS hiyo. Baada ya hapo uongozi wa SACCOS huwasilisha maombi hayo benki kwa uamuzi.

Ndugu Wananchi;

Wamekuwepo pia watu wanaolalamika kuwa kiasi cha fedha kinachotolewa katika mikopo hii ni kidogo mno na kwamba riba ya silimia 10 ni kubwa mno. Ni kweli kiasi kinachokopeshwa, yaani kati ya shilingi 50,000 na 5,000,000 si kikubwa lakini imefanywa hivyo kwa makusudi. Hii ni mikopo ya watu wenye kipato cha chini ambao katika hali ya kawaida benki haziwakopeshi. Maskini hakopesheki benki. Hana dhamana ya kukubalika na benki na wala hana uwezo wa kulipia gharama za kuombea mkopo.

Ndugu Wananchi;

Kwa kutambua ukweli huo na kwa nia ya kutaka kuwawezesha wananchi wenye vipato vya chini kupata mikopo ili na wao waanze safari ya kuelekea kwenye maisha bora, ndipo Serikali ilipoamua kuanzisha mpango huu wa mikopo. Hakuna sharti la kuwa na dhamana kwa wakopaji na wala hawalipi ada ya kuomba mkopo. Serikali imebeba mzigo huo. Fedha iliyotolewa na Serikali kwa benki ndiyo dhamana, na ndiyo inayofidia gharama za kuchukua fomu za maombi na za kushughulikia maombi.

Ndugu zangu;

Ni kweli kabisa kwamba ingekuwa vizuri kama mikopo hii ingekuwa haina riba yoyote. Tena lingefurahisha wengi na hususan wale ambao kiimani riba ni jambo haramu. Suala la kutokuwepo riba, lilizungumzwa kwa kina lakini lilikuwa gumu kulitekeleza. Sababu ya msingi ni gharama nyingine za kibenki zilizobaki hata baada ya Serikali kubeba mzigo wa dhamana na gharama za kuomba mkopo.

Ndiyo maana mikopo hii ina riba. Hata hivyo, ndugu zangu, ukilinganisha na riba ambazo kwa kawaida huwa zinatozwa na mabenki haya kwa mikopo ya namna hiyo riba inayotozwa kwa mikopo hii bado ya chini.

Vile vile unapolinganisha na riba inayotozwa na asasi za fedha zinazotoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo wadogo, riba inayotozwa kwa mikopo hii bado ni nafuu sana. Nyingi ya asasi hizo hutoza riba ya zaidi ya asilimia 30 na nyingine hufikia hata asilimia 40 au zaidi.

Ndugu Wananchi;

Nimeyaeleza haya kujaribu kufafanua baadhi ya mambo yanayoleta utata katika utaratibu mzima wa mikopo ya wajasiriamali wadogo wadogo. Sikuyamaliza maswali yote waliyokuwa nayo wananchi, naamini tutapata fursa siku zijazo kuyafafanua. Lakini pia, viongozi wenzangu taifani, mikoani na wilayani watasaidia kuyafafanua. Waendeeni, waambieni. Watafurahi kuwasaidia kwani ni wajibu wao.

Ndugu Wananchi;

Nauona mpango wa mikopo ya wajasiriamali kuwa ukombozi wa wanyonge. Kila kitu kina changamoto zake. Kuwepo kwa changamoto kusitukatishe tamaa bali kutuongezee ari ya kutafuta mbinu na maarifa ya kuzishinda. Maombi yangu kwa wadau wote ni kuwepo na ushirikiano miongoni mwetu. Pawepo na mawasiliano ya urahisi miongoni mwa wadau ili tatizo linapotokea habari ziwafikie wahusika kwa wakati. Naomba sote tushirikiane na tushikamane kwa dhati katika kuhakikisha kuwa mpango huu unafanikiwa kutimiza malengo yake.

Tuhakikishe kuwa taratibu zilizowekwa zinafuatwa lakini urasimu na ucheleweshaji usiokuwa wa lazima unaepukwa. Pia tuhakikishe kuwa mikopo inatumika kwa shughuli iliyokusudiwa na inarejeshwa kwa wakati ili na wengine nao waweze kukopeshwa. Tukiyazingatia na kuyafanya haya tutakuwa tumejenga msingi mzuri wa kuwapatia Watanzania wa kawaida fursa ya kubadili maisha yao kuwa mazuri zaidi kuliko yalivyo hivi sasa.

Ndugu Wananchi;

Naomba nimalizie mazungumzo yangu kuhusu mikopo kwa kutoa wito kwa Watanzania wenzangu tunaotaka mikopo kuwa na moyo wa subira. Muda utahitajika tangu mtu awasilishe maombi mpaka atakapopata. Hatuna budi kulitambua hilo na kuwa na subira nalo.

Lakini, kubwa zaidi ni ule ukweli kwamba si kila mmoja aliyeomba mkopo atapata wakati huo huo. Kama tulivyoona maombi ni makubwa kuliko fedha iliyopo. Kwa vyovyote vile, wapo watakaopata mwanzo na wapo watakaopata baadaye baada ya wale wa mwanzo kuanza kulipa.

Nawasihi Watanzania wenzangu tuutambue ukweli huo na kuukubali, ndiyo maana nawasihi tuwe na moyo wa subira। Kutaka wewe uwe wa mwanzo ndiyo ubinadamu, lakini ni vyema kutambua kuwa kwa hali ilivyo unaweza usiwe wa mwanzo. Ikitokea hivyo kubali na endelea kusubiri. Utaratibu huu ni endelevu. Si wa mara moja.

Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa

Ndugu Wananchi;

Nchi yetu hivi sasa imekumbwa na tatizo la ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa yaani kwa Kiingereza Rift Valley Fever au kwa kifupi RVF. Ni ugonjwa hatari unaoua wanyama na binadamu pia.

Homa ya Bonde la Ufa ni ugonjwa wa mifugo na mwanadamu hupata maradhi hayo kwa kula nyama ya mnyama aliyeathirika.

Vile vile mnyama na mwanadamu wanaweza kupata maradhi kwa kuumwa na mbu wa aina ya Aedes mwenye wadudu wa maradhi hayo.

Mbali ya kuua mifugo mingi ugonjwa huu pia umesababisha vifo vya wananchi wenzetu katika baadhi ya mikoa hapa nchini. Hadi kufikia tarehe 28 mwezi huu watu 33 walikuwa wamepoteza maisha yao na wengine 119 walikuwa wameambukizwa.

Kwa upande wa mifugo mikoa ambayo imekumbwa na ugonjwa huu ni Dodoma, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Iringa, Singida na Mbeya. Mikoa ambayo watu wameathirika na hata baadhi yao kufariki dunia ni pamoja na Manyara, Tanga, Dodoma na Morogoro. Mikoa ya Dar es Salaam na Singida pia inao wagonjwa wachache wenye kuonyesha dalili za ugonjwa huo ambao wanaendelea kuchunguzwa.

Ndugu Wananchi;

Napenda kuchukua fursa hii kuwapa pole Watanzania wenzetu wote walioathirika na ugonjwa huu hatari. Kwa wale waliotangulia mbele ya haki, tunawaomba ndugu na jamaa zao wapokee mkono wetu wa rambirambi na pole zetu nyingi. Tunaelewa machungu ya kupotelewa na wapenzi wao. Tunajumuika nao na kuomboleza nao katika wakati huu mgumu wa machungu mengi na majonzi tele. Tuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu awape marehemu wetu hao rehema na azilaze roho zao mahali pema peponi.

Kwa wagonjwa wanaoendelea kupata matibabu tunawaombea wapone haraka ili wajiunge tena na familia zao na jamii nzima ya Watanzania katika ujenzi wa Taifa। Kwa wenzetu waliopoteza mifugo tunawapa pole kwa kupoteza rasilimali muhimu. Wasivunjike moyo, ndiyo mitihani ya dunia. Kuteleza si kuanguka.

Hatua Zinazochukuliwa na Serikali

Ndugu Wananchi;

Serikali inatambua uzito wa tatizo linalotukabili na inafanya kila iwezalo kutokomeza ugonjwa huu. Katika mkakati tuliouandaa hadi sasa tumechukua hatua zifuatazo:

Kwanza, tumezuia kufanyika kwa minada ya mifugo kote nchini. Hatua hii ni ya muda inayolenga katika kudhibiti kuenea kwa ugonjwa. Minada itaruhusiwa tena kufanya kazi pindi hali itakaporejea kuwa nzuri.

Pili, tumeimarisha utoaji wa chanjo za mifugo dhidi ya ugonjwa huu kwenye maeneo yote yenye mifugo. Hadi sasa tumeshatumia kiasi cha shilingi bilioni 1.7 kununulia chanjo na vifaa vingine vya kukabiliana na ugonjwa. Tayari tumeagiza dozi milioni mbili za chanjo ya RVF. Kati ya hizo, dozi 736,600 zimeshapokelewa na kusambazwa kwenye wilaya zilizoathirika na zile zilizo katika hatari ya kuambukizwa ugonjwa.

Tatu, tumeandaa chini ya usimamizi wa Mheshimiwa Waziri Mkuu, mpango wa dharura wa kitaifa wa kudhibiti ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa। Mpango huu utagharimu dola za Kimarekani takribani milini 12.3. Tunaendelea kuwasiliana na marafiki zetu wa nje kuhusu uwezekano wa kutusaidia kugharamia mpango huu mapema iwezekanavyo ili kunusuru mifugo yetu na maisha ya watu.

Wajibu wa Kila Mmoja Wetu

Ndugu Wananchi;

Jukumu la kupambana na ugonjwa huu ni letu sote. Kila mmoja wetu pale alipo anao wajibu wa kuhakikisha kuwa anachukua tahadhari zote muhimu zitakazosaidia katika kukabiliana na ugonjwa huu. Hivyo nawaomba tuzingatie mambo yafuatayo:

Kwanza, tuhakikishe kwamba mifugo yote inapata chanjo. Hii ndiyo kinga yetu ya kwanza ya kupambana na ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa. Serikali inafanya jitihada ili kuhakikisha kwamba dozi za kutosha za chanjo zinapatikana. Hivyo nawaomba watu wote wapeleke mifugo yao ikachanjwe mapema iwezekanavyo.

Pili, tuache tabia ya kuhamisha mifugo kutoka eneo moja kwenda eneo lingine kiholela. Uhamishaji holela wa mifugo unachangia katika kueneza ugonjwa. Aidha, unarudisha nyuma jitihada zetu za kudhibiti ugonjwa huu hatari.

Tatu, tuepuke kuchinja wanyama na kuchuna ngozi bila kuchukua tahadhari za kujikinga. Vile vile tujiepushe na kushika damu, majimaji na nyama ya mnyama anayehofiwa kuwa na ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa.

Nne, tusile nyama ya mnyama aliyekufa kwa ugonjwa huu. Inashangaza sana kusikia kuwa baadhi ya wenzetu wanadiriki kufukua mizoga iliyozikwa na kula nyama yake. Ndugu zangu, ni uchu wa kiasi gani huo unaotufanya hata tupuuze tishio kubwa kwa maisha ya mwanadamu kama hili la ugonjwa huu. Nawasihi tusikilize ushauri. Wahenga wamesema “asiyesikia la mkuu huvunjika guu”.

Tano, tuepuke kunywa maziwa yasiyochemshwa vizuri. Siku zote tuchemshe maziwa vizuri kabla ya kuyanywa.

Sita, wataalam na watendaji kwenye ngazi ya wilaya na vijiji wasimamie kwa ukamilifu utekelezaji wa Sheria ya Magonjwa ya Mifugo ili kudhibiti kuenea zaidi kwa ugonjwa huu.

Saba, wananchi watumie vyandarua hasa vile vilivyowekwa dawa ili kujikinga na mbu. Ndugu zangu, tukumbuke kuwa ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa unaenezwa pia na mbu aina ya Aedes. Hivyo kinga dhidi ya mbu ni jambo muhimu sana.

Na nane, tuongeze juhudi za kudhibiti mbu ili tupunguze kushamiri kwa mbu kwenye maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Watu wafukie mazalia ya mbu na pale inapowezekana wanyunyizie dawa.

Ndugu Wananchi;

Katika mapambano yetu dhidi ya ugonjwa huu, vyombo vya habari vinalo jukumu kubwa la kusaidia kuelimisha umma kuujua ugonjwa na jinsi ya kujikinga nao। Nawaomba mtimize wajibu wenu huo wa msingi kwa ukamilifu. Nawashukuru kwa hatua tuliofikia sasa naomba waendelee kufanya vizuri zaidi. Nawaomba wawe na ushirikiano na mawasiliano ya karibu na mamlaka husika na hasa wataalamu husika ili kuepuka kuandika au kutangaza habari ambazo hazijathibitika.

Hitimisho

Ndugu Wananchi;

Ni matumaini yangu kuwa kila mmoja wetu atazingatia mambo ya msingi katika mapambano yetu dhidi ya ugonjwa huu. Hususan naomba tuzingatie ushauri wa wataalam utakaoendelea kutolewa mara kwa mara. Mimi naamini kuwa kama tukiyazingatia hayo tutaweza kuzuia kuenea na hatimaye kuutokomeza ugonjwa huu hatari mapema iwezekanavyo.

Watanzania tunayo sifa moja kubwa. Nayo ni kuwa pale tunapokabiliwa na adui siku zote huwa wepesi sana katika kuunganisha nguvu zetu na kupambana nae.

Ndugu zangu, ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa ni adui hatari anayetaka kutudhalilisha na hata kutuangamiza. Naamini kama ilivyo kawaida yetu tutaunganisha nguvu zetu ili tuweze kumtokomeza adui huyu mapema iwezekanavyo.

Na, katika vita hii kila mmoja wetu analo jukumu lake la kufanya. Naomba basi kila mmoja wetu atekeleze jukumu lake ipasavyo ili tuweze kuushinda na kuutokomeza kabisa ugonjwa wa Homa ya Bonde la ufa. Inawezekana Timiza Wajibu Wako!

Mungu Ibariki Afrika!

Mungu Ibariki Tanzania!

Asanteni kwa Kunisikiliza!

Chanzo cha habari: Tanzanet mailing list (list@tanzanet.org), Ijumaa Aprili 6, 2007.

Friday, April 06, 2007

Kima Punjuni anapatikana Zanzibar tu


(Procolobus kirkii) Zanzibar Red Colobus

na Tina Mlonda

TUMEZOEA kuona wanyama jamii ya nyani wakizunguka kwenye mashamba yetu. Kwetu sisi wakulima, mara nyingi ni wanyama wanaoharibu mazao, hasa mahindi yakiwa shambani. Ndipo usemi wa “ukicheka na kima utavuna mabua” ulipoanza. Pamoja na yote mabaya, lakini kuna mengi ya kujivunia kuhusu wanyama hawa kwani ni urithi wetu. Pia kuna ambao hupatikana Tanzania ambapo watalii hulazimika kuja kwetu kuwaona. Wanyama hao jamii ya nyani ni pamoja na mbega mwekundu wa Iringa na kima punjuni au mbega mwekundu wa Zanzibar.

Leo nitazungumzia kima punjuni au mbega mwekundu wa Zanzibar. Kwa Kiingereza hujulikana kama “Zanzibar Red Colobus” au “Kirk’s Red Colobus”. Jina la Kirk ni la Mzungu aliyewahi kuishi visiwani Zanzibar miaka ya enzi za ukoloni, ambaye alimtambua mnyama huyu na kufanya wanasayansi nao watake kumjua.

Mzungu huyo alikuwa akijulikana kama Sir John Kirk. Mnyama huyu ana manyoya ya rangi nyekundu iliyoiva na nyeusi sehemu za mgongoni. Uso wake mweusi una taji la manyoya meupe. Ana alama za rangi ya pinki kwenye midomo na pua. Ana mkia mrefu ambao una rangi nyeusi kwa juu na nyeupe kwa chini. Hupatikana kwenye hifadhi za misitu ya Jozani, Ngezi huko Zanzibar. Kima punjuni huishi kwenye kundi la wanyama kati ya thelathini mpaka hamsini. Humo huwa kuna madume wanne na majike mengi na pamoja na watoto. Ni wanyama ambao huishi kijamii zaidi. Hupenda kucheza na kutoana chawa wakati wa kupumzika.

Utafutaji wa chakula hufanywa na kundi zima. Madume hutoa mlio fulani ambao huutumia kuita wenge kwenda kutafuta chakula. Chakula chao mara nyingi ni majani mabichi, vikonyo vya majani, maua na matunda mabichi. Ni aina ya wanyama ambao hawali matunda mabivu. Hii ni kwa sababu matumbo yao ambayo yamegawanyika sehemu nne hayawezi kumeng’enya sukari. Hula pia mkaa, ambao huaminika kuwa husaidia kwenye mmeng’enyo wa chakula. Mkaa huu huondoa sumu itokanayo na majani waliyokula.

Hubeba mimba kwa muda wa miezi mitano ambapo kawaida huzaliwa mtoto mmoja. Mtoto huyo hukaa na mama yake akinyonyeshwa kwa miezi mitatu. Tabia moja ya ajabu kwa wanyama hawa ni kuwa unaweza kukuta dume mkubwa akiwa ananyonya kwenye matiti ya jike. Wanyama hawa wana uzito kati ya kilo 5 na gramu 200 na kilo 11 gramu 300.

Watu wa Zanzibar huamini kuwa mnyama huyu ana sumu hivyo humuhusisha na imani za kichawi. Pia huaminika kuwa mnyama huyu anapokuwa sehemu fulani, basi miti na mazao ya sehemu hiyo hufa. Na ikitokea kuwa akaliwa na mbwa, basi mbwa huyo hunyonyoka manyoa. Wana harufu kali (ndio mwanzo wa neno punju), hivyo wanyama hawa hawafugwi. Wanyama hawa wako kwenye hatari kubwa ya kupotea na tayari Shirika la Kuhufadhi Wanyamapori Duniani (IUCN) limewaweka kwenye mstari mwekundu. Hii ni kutokana na makazi yao ya asili ambayo ni misitu kuharibiwa. Tabia za binadamu ambazo ni hatari kwa makazi yao ni pamoja na uvunaji wa miti kwa ajili ya mbao, uchomaji wa misitu na usafishaji wa misitu kwa ajili ya mashamba.

Inasadikiwa kuwa idadi ya wanyama hawa iko chini ya 1,500 tu.

Mradi wa kuhifadhi msitu wa Jozani, yaani Jozani-Chwaka Bay Conservation Project, uliokuwa kati ya mwaka 1995 mpaka mwaka 2003, ulimchagua mnyama huyu kuwa kwenye nembo ya utunzaji mazingira Zanzibar. Huyo ndiye mnyama aitwaye kima punjuni, ambaye anapatikana Zanzibar peke yake. Jamani tuamke Watanzania tuache tabia mbaya ya uharibifu wa mazingira kwani tukiendekeza tutampoteza mnyama huyo. Pia nakukumbusha kutembelea hifadhi zetu ili kujionea urithi halali tulioachiwa na Mwenyezi Mungu.

tcharles82@yahoo.co.uk

Chanzo cha habari: http://www.freemedia.co.tz

Thursday, April 05, 2007

Eritrea bans female circumcision


(photo: Graeme Robertson/Getty Images)

Eritrea has banned the life-threatening practice of female circumcision, the Eritrean information ministry has said. Anybody involved in female genital mutilation (FGM) would be punished with a fine and imprisonment, it said. The..

Read full article: http://news.bbc.co.uk/1/hi/world/africa/6527619.stm

Wednesday, April 04, 2007

Easter exodus empties cities


Norwegians settled down Wednesday for the country's annual five-day Easter vacation. Most stores and businesses were to be closed Thursday, Friday, Sunday and Monday, as folks flock to the mountains, the coast and other holiday retreats.

Many Norwegians have started taking the entire week off, and Oslo was noticeably quieter as early as Monday. Hotels in the mountains are packed, as are flights to warmer climes, and many businesses (including Aftenposten) were operating with severely reduced staffing.

Police were nonetheless bracing for lots of traffic out of the city on Wednesday, and railway NSB was reporting full trains. Traffic on the main E18 highway west of Oslo was due to be disrupted throughout the entire weekend, starting at 10pm Wednesday, because of construction projects around the Lysaker intersection and train station.

Those opting to stay in the city could look forward to no shortage of parking places, cinemas that now stay open during Easter and a generally more relaxed atmosphere in town. The weather in southern Norway remains unseasonably mild, so opportunities abounded for urban walks and strolls along the fjord.

Most museums close for the long Easter weekend, but the Norwegian Folk Museum on Bygdøy was staying open every day, from 11am-3pm on Thursday and Friday and until 4pm on Saturday, Sunday and Monday. The museum planned egg-decorating and pancake workshops for children in addition to its normal exhibits.

Boat enthusiasts have started viewing Easter as a fine time to get their pleasure craft back out on the water, and sunny weather also aided myriad boat maintenance projects around the Oslo Fjord.

While the vast majority of Norwegians still opt for traditional ski holidays in the mountains, many are using the holiday period on home remodeling projects and spring cleaning. Stores in the furniture and building business were reporting brisk sales earlier this week.

Many stores will re-open, albeit with shortened hours, on Saturday, for those failing to stock in enough provisions through Tuesday.

Aftenposten English Web Desk
Nina Berglund

Tuesday, April 03, 2007

Kiswaglish kwa chati na Wabunge


Uharibifu wa lugha yetu safi inayohitaji ufasaha wa kuitangaza ya Kiswahili, huanzia Bungeni na kisha huenea mitaani kwa Watanzania wengine.

Hayo yamedhihirika wazi tena wakati mwingine live katika luninga zetu za Bongo, kutokana na tabia yao ya kuchanganya lugha hii na kiingereza.

Ni katika vikao vya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utasikia Wabunge wakichangia, kukosoa au kufafanua kitu kwa mchanganyiko wa lugha hizi mbili (kiswahili na kimombo).

Mara nyingi utasikia.. ” Mh Waziri katika hotuba yake alijaribu kutuconvince, lakini maelezo yake juu ya ile project ya kuupgrade ile barabara ya kutoka Wilayani hadi kijijini hayakufanyiwa kazi’’

Pamoja na maelezo kuwa huo ni msisitizo wa jambo aka kukazia point, bado kiswahili kinafahamika na kinatosha kufanya haya yote.

Lawama sasa zinaelekezwa kwa Wabunge waliotarajiwa kuwa wasimamizi na watangazaji wa kiswahili fasaha ikitiliwa maanani kwamba kimeteuliwa karibuni kuwa lugha inayofaa kutumika Umoja wa Afrika.

Hadi mitaani lugha imekuwa ndiyo hiyo hiyo kwa maneno kama ’’haturuhusu short time, amenilima memo, jamaa hatamind na mengine mengi yanayofanana na haya.

Hivi sasa mbali ya kutoka na mkakati mpya wa kutibu kusambaa kwa gonjwa hili, kasumba ya Wabunge imetakiwa kubadilika ili kuokoa lugha yetu na virusi hivi.

Chanzo cha habari: http://www.darhotwire.com/dar/Habari/2007/04/02/31447.html

Heri Kulamba Miguu ya Kikwete Kuliko ya Mabeberu


By Salehe Mmoro

Mwanahabari wa HabariTanzania.com, Dar-es-salaam

Habari ilichapishwa kwenye Habari Tanzania, Oktoba 2006.

JUMAPILI, Oktoba Mosi mwaka huu, Gazeti la Sunday Nation la Kenya liliwakejeli waandishi wa habari wa Tanzania kwamba walikuwa wakikalia ‘kumlamba miguu’ Rais Jakaya Kikwete, na kukariri kila akisemacho, kama kasuku!

Kejeli hiyo kupitia katuni iliyochapwa ukurasa wa nane wa gazeti hilo, iliwaonyesha Waandishi wa TZ ( Tanzania) waliokuwa wakishangilia, na wengine wakiwa wamemsujudia Kikwete, huku wakimlamba miguu, kuonyesha kuwa waandishi wa nchi hii ni mbumbumbu wasioweza kufanya tafakuri tunduizi dhidi ya kauli za watawala, isipokuwa, kufagilia tu!

Naam, licha ya kumsujudia Kikwete, kumlamba miguu na kushangilia kila alichokuwa akisema, katuni hiyo ya mwaka, iliwaonyesha baadhi yao wakionyesha unyenyekevu kwa rais aliyeketi katika kiti cha enzi, huku akiwa kavalia kanzu, suruali na ‘mabuti’.

Japo ni ujumbe uliotumwa kwa njia ya kejeli kupitia katuni, lakini maudhui ya katuni hiyo yamebeba ukweli uliotiwa chumvi nyingi, dhana iliyowahi kupingwa na hata Yesu wa Nazareti; ya kutoa kibanzi jichoni mwa mwenzako, wakati kwako kuna boriti.

Ukweli mwanana uliomo katika katuni hiyo ni juu ya vyombo vya habari kuacha wajibu wa kuutumikia umma, na kugeuka kasuku; ili kuwasifia watawala.

Tatizo hili halipo Tanzania peke yake, limeota mizizi tangu Kenya, ambako hadi majuzi tu, kila sentensi katika kila Taarifa ya Habari ya Sauti ya Kenya (VOK) na baadaye KBC, ilikuwa ikianza na “Mtukufu!!”Binadamu atakuwaje mtukufu, kama si kulamba dole gumba la watawala? Mtukufu ni Mungu ambaye wengine hudai hayupo.

Mtukufu Rais husika alikuwa akiimbwa kwa takriban asilimia 80 ya muda wa taarifa ya habari, wakati habari zinazohusu maendeleo ya watu, kero zao na hata habari za wanaharakati wa Haki za Binadamu na zile za wapinzani ,zikibezwa!

Sijafahamu; kama habari hizo za kumwita mwanadamu mmoja, “Mtukufu !” kama Mungu, zilikuwa zikikusanywa, zikiandikwa na kuhaririwa na kina nani, kama si waandishi wa habari wa Kenya?

‘Mtukufu, Baba Moi’ alikuwa akiimbwa redioni tangu alfajiri KBC ilipokuwa ikifunguliwa hadi wakati wa kufungwa usiku wa manane.

Haki za wananchi kuzungumza kupitia vyombo huru vya habari, haukuwepo. Badala yake jamii isiyo huru ilikuwa ikichaguliwa wimbo gani waimbe; bila shaka kusifia harakati za serikali ya NYAYO katika kuwaletea watu wake Demokrasia na Maendeleo!

Si Kenya tu. Hata waandishi wa Marekani ambako kunadaiwa Demokrasia imekomaa, na vyombo vya habari viko huru hata kuandika habari za Hugo Chavez kumtukana Bush shetani, vimekuwa vikisambaza pumba na propaganda kwamba Iraq ilikuwa na silaha za maangamizi.

Waandishi wa habari wa Marekani waliokuwa wakiandamana na majeshi ya nchi hiyo Iraq na Afghanistan, hawakuacha kuandika habari za uongo, za upande mmoja, kwamba majeshi ya Washirika yalikuwa yakisonga mbele kwa kasi, huku yakishangiliwa, hata kama walikuwa wakipigwa na maiti za askari wao kuburuzwa mabarabarani na wenyeji.

Hata leo, vyombo vya habari vya Magharibi haviachi kumsifia Bush na Tony Blair na mikakati yao ya kutaka kuzivamia Korea Kaskazini, Iran na Syria, kwa sababu zozote za uongo. Wala hawajakoma kuudanganya umma kwamba Bush anapendwa ulimwengu mzima, wakati Chavez akimtukana Ibilisi, katika mkutano wa mataifa yote, mjini New York! Vipi kuhusu kipigo cha Israeli dhidi ya Hizibollah? Wanasema nani shetani, kati ya Israeli na Lebanon…ni politiki tu.

Kwa kusema hivi, sipendi kutetea uandishi wa upande mmoja; wala sipendi kuunga mkono ‘ukasuku’ wa vyombo vya habari vya ulimwengu mzima, ikiwemo Tanzania.

Ningeridhika, kama gazeti la Nation lingetoa mada kuhusu waandishi wote wa habari wa nchi zetu hizi, ili wafuate maadili ya uandishi na kukosoa watawala wanapokwenda kinyume cha matakwa ya watu.

Ni kichekesho magazeti ya Uingereza kumkosoa Robert Mugabe wa Zimbabwe, kwa kunyang’anya mashamba ya Wazungu na kuwapa Waafrika, wakati waki ‘mfagilia’ Tony Blair kushirikiana na Bush kutesa watu na kuwafunga jela bila kuwafikisha mahakamani huko Guantanamo Bay, Abu-Ghraib na jela za siri Ulaya! Wakati huo huo wakibomoa makazi ya mamilioni ya watu kwa mabomu Iraq, Afghanistan na Lebanon…na sasa wanatishia kwenda Syria, Iran na Korea Kaskazini.

Huku ni kutetea haki za binadamu wapi? Au ndio kama walivyosema wahenga, “nyani haoni nonino?” Tazama CNN, BBC, ABC,CBS,NBC au hata SKY NEWS, n.k. hutakosa kuona habari hasi kuhusu Bara la Afrika na Waafrika…makamasi, mapanki, ukimwi, njaa, vita na kila uchafu!

Hii ni kuonyesha kuwa si lazima sana vyombo vya habari vya kizalendo kupiga kelele nyingi zinazoweza kuivunjia hadhi nchi hiyo miongoni mwa mataifa. Vitakosoa watawala kwa namna ambayo haileti migogoro ya kisiasa inayosababisha “kelele nyingi” hadi masikioni mwa akina Bush, Marekani kiasi cha kutilia shaka ‘Political stability’ katika nchi hizo!

Ulimwengu haujasahau Desemba 30; dakika chache rais Mwai Kibaki wa Kenya akikaribia kuapishwa kuwa rais wa tatu wa Kenya. Katika uwanja wa Uhuru Park, Mtangazaji maarufu wa nchi hiyo (simtaji) ali ‘katwa mtama’ na wananchi waliokuwa wakimshangilia kwa nguvu rais Mpya, wakampokonya chombo cha kutangazia!

Sababu za Mtangazaji huyo wa siku nyingi VOK na KBC kupigwa mtama na wananchi, ni kutangaza habari za kujikomba sana kwa utawala uliopita, na kuwabeza wapinzani, ambao muda mfupi tu waliapishwa kuchukua dola. Hao ni waandishi wa Kenya.
Enzi ya Nyayo wasingethubutu kuwabeza ndugu zao wa Tanzania kuwa wanawafagilia watawala. Vipo vyombo vya habari katika nchi zote vinavyofanya kazi bila upendeleo, wala kujikomba.

Hapa nchini, Kikwete amekosolewa sana; hata sasa Mama Salma anakosolewa kwa kwenda kuhudhuria sherehe za Kimila huko Swaziland, ambako kila mwaka Mfalme Mswati II huchagua kigoli na kuoa.

Wala hatuhitaji kupiga kelele sana hadi akina Bush wasikie huko Washington hadi wafadhili wafikiri tutatoana ngeu! Kenya, katika Uchaguzi mkuu uliopita, watazamaji wa uchaguzi wakiwemo wa Umoja wa Ulaya (EU) walisema KBC ilikipendelea chama cha Kanu, hususan mgombea wake, Uhuru Kenyatta, kwa asilimia kati ya 32 na 33; wakati wapinzani hususan Narc wakitangazwa kwa asilimia 25 tu katika televisheni ya KBC.

KTN walimtangaza Kibaki kwa asilimia 45, Kanu wakatangazwa kwa asilimia38. Televisheni ya Nation ilimpa Kibaki ‘coverage’ ya asilimia 44, wakati Uhuru Kenyatta na Moi walitangazwa kwa asilimia 34 tu. Je, kuipinga serikali iliyoko madarakani na kuwapendelea wapinzani kwa jinsi hiyo, ndio kulinda maadili ya uandishi? Sio kuwa bias?

Wapi impatiality?
Umoja wa Ulaya walisema,ingawa Tume ya Uchaguzi ya Kenya ilitoa mwaongozo kwa vyombo vya habari, vyombo vya habari vya Kenya, likiwemo gazeti la Nation, walishindwa kuwapa wapiga kura habari sahihi.

Kwa upande mwingine vyombo vya habari vya Kenya, vilikuwepo wakati wa Utawala wa Moi. Lakini vilishindwa kufichua vyumba vya vya siri vya mateso dhidi ya wapinzani wa Kanu, katika jengo la makao Makuu, ya Kanu, Jogoo House, hadi utawala mpya wa Narc ulipoingia madarakani.

Vilishindwa kusema ukweli juu ya watu waliokufa katika mazingira ya kutatanisha enzi za Nyayo. Hawa ni pamoja na Dk. Robert Ouko, na mpiga picha wa Kiingereza, Julie Ward (28) aliyeuawa katika mbuga za wanyama za Masai Mara. Mauaji ya Julie yaliifanya serikali ya Kenya kuwa lawamani, kufuatia Uingereza kuwatuma Scotland Yard kupeleleza chanzo cha mauaji hayo, kufuatia serikali kusema aliuawa na wanyama wakali!

Kwanini Scotland Yard walikuja kufanya upelelezi wa mauaji ya msichana huyo Kenya, wakati wapo polisi wa nchi hiyo? Rushwa? Kwa nini vyombo vya habari vya nchi hiyo vimeacha nchi kufika huko, kama vyatenda kazi yao barabara?

Vyombo vya habari vya Kenya havikusema muuaji, hadi utawala wa Kibaki ulipoingia madarakani ndipo wakaanza kuandika haja ya kuchunguza vifo vya akina Julie, Dk. Ouko, J.M. Kariuki, Pio Gama Pinto, Tom Mboya na wengine ambao vifo vyao vilikuwa utata mtupu. Je, huu ni Uungwana?!

Na kwanini mahali ambapo vyombo vya habari haviwalambi miguu watawala, kuwe na mauaji ya siri na mawingu ya mashaka , jinsi mfumo mzima unavyofanya kazi… hadi waje Scotland Yard?

Nation waliandika nini kuhusu kifo cha Julie Ward?Waliikosoa serikali kwa asilimia mgapi?

Moi aliiongoza Kenya kwa miaka 24, tangu kifo cha mwasisi wa Taifa hilo, Jomo Kenyatta, 1978.Lakini hadi Kibaki alipoingia madarakani 2002 ndipo ‘siri’ za mauaji ya akina Dk.Ouko ya Feburuari 1990 na siri ya vita vya kikabila vya miaka ya 90 zikaanza kuvuja.

Nation walikuwepo Kenya, walifanya nini badala ya ‘kuulamba miguu’ utawala wa Moi? Kuhusu kashfa za Goldenberg na Anglo Leasing; vyombo vya habari vya Kenya havipaswi kujitazama kuwa viko juu katika kufichua ‘skandali’.Kinachoufikia umma wa Kimataifa, wakiwemo akina George W. Bush, ni fujo na makelele, kana kwamba nchi hiyo haina ‘political stability?’

Mtindo unaotumiwa na waandishi wa habari wa nchi hiyo, na ambao wanataka waandishi wa Tanzania wauige, ni kushambuliana kila kukicha. Vyombo hivyo na waandishi wake hawajapona majeraha ya kikabila, kimajimbo na hata kidini. Bila shaka waandishi wa kabila fulani huwatetea wanasiasa wa kabila lao hata kama wanaleta mgawanyiko.

Waandishi wa itikadi fulani hudumu kuipinga serikali hata kama haijafanya makosa, mradi tu watu wao washinde uchaguzi. Huu si uhuru wa vyombo vya habari wala kufuata maadili; bali fujo tu zinazo dunda kwa fujo masikioni mwa akina Bush, Washington.

Kuhusu udini, katuni ya Nation imekosa hoja kutaka kuwaambia Watanzania waliokwisha sahahu ukabila na udini, kwamba Kikwete aliyekalia kiti cha enzi ni Muumini wa Madhehebu fulani, ambao hutambulishwa kwa vazi la kanzu!

Kikwete, awe Muislamu, Mkristo, Budha, Baniani, Mpagani au hata asiye na dini yoyote, Watanzania hawajali!

Nijadili kidogo waandishi wa nchi hii kumfagilia Kikwete. Kama udhaifu huu upo hapa Tanzania kama Kenya na Marekani, si wajibu wa waandishi wa Kenya kutufundisha maadili ya kazi. Zaidi sana kila nchi ina maadili yake ambayo hata vyombo vya habari huyafuata.

Kwanza Watanzania hawajazoea fujo; hawajawahi kupigana; wa kabila moja dhidi ya lingine kiasi cha kuathiri nyanja mbalimbali hadi kuanza kushambuliana kwa ukali na kuzua mtafaruku.

Tatizo la vyombo vyetu vya habari kumfagilia Kikwete halina tofauti na vyombo vya Magharibi kutoona uvunjaji wa Haki za Binadamu wa Marekani na washirika wake Iraq na Afghanistan, na badala yake kukalia kumlaani Osama bin Laden, Wataleban, Magaidi, Mullah Muhammad Omar na wengineo wanaopinga ubeberu kwa staili ya kujitoa mhanga.

Pengine, kuipinga serikali iliyoko madarakani na kuwaunga mkono wapinzani bila kujiondoa katika upendeleo wa upande mmoja, si kipimo sahihi cha utendaji kazi au kutimiza wajibu.

Nani asiyejua kuwa kelele za vyombo vya habari vya nchi hiyo juu ya harakati za wanasiasa wa nchi hiyo kupendelea ukabila na migawanyiko ndizo zinazoifanya Kenya kuonekana haijatulia?

Katika nchi ambayo vyombo vya habari hufanya kazi vizuri hakuna rushwa ya kutikisa kama Goldenberg na Anglo Leasing; na wananchi wananeemeka kwa amani inayowaletea uchumi mzuri, potelea mbali utulivu usiwepo.

Ubora wa vyombo vya habari haupimwi kwa picha nzuri za televisheni na magazeti, na mbwembwe za watangazaji wa redio,bali hupimwa kwa amani na ustawi walionao wananchi au jamii inayotumikiwa na vyombo hivyo.

Kipimo cha uandishi bora hakiji kupitia mashambulizi yasiyo na sababu dhidi ya serikali, bali kuutafuta ukweli mkamilifu, bila mashaka, wala shinikizo la wanasiasa wa upande fulani kwa maslahi yao…uandishi bora uliotukuka huwatumikia wananchi wanyonge, makabwela; wala siyo wanasiasa wa upinzani tu.

Bob Woodward na Carl Bernstein au kama walivyokuja kujulikana, “ The Woodstein” ni waandishi wa gazeti la Washington Post, waliofichua kashfa ya Watergate, iliyomfanya Rais Richard Milhouse Nixon kujiuzulu Agosti mwaka 1974.

Waandishi hao wa kitabu maarufu cha All The President’s Men, waliweka bayana matumizi ya fedha haramu kwa maharamia waliovunja makao makuu ya kampeni ya chama cha Democrat, (wapinzani wa Nixon), yaliyoitwa Watergate.

Nixon alikabiliwa na mashitaka ya uhaini kutoka Baraza la Congress, baada ya waandishi hao kulipua skandali la Watergate.Akajiuzulu, na makamu wake wa Rais Gerald Ford, akachukua mahali pake. Ushahidi ulikuwepo, na ungeweza kutolewa mahakamani dhidi yake.

Naam, kuandika habari nzito hakujitengi na ushahidi wa dhati; na wala siyo dhana na kusingizia kusikowanusuru waandishi na mashitaka,kama waandishi wa Kenya wanavyotaka tuanze kumfanyia rais wetu!

Hatuna ugomvi mkubwa na serikali ya Kikwete. Wala Mama Salma hajawahi kuvamia chombo chochote cha habari na kuwapiga bakora waandishi, kubomoa makompyuta na kutupa magazeti.

Kwa kusema hivyo, hatuna maana kuwa tunamlamba miguu au kutowajibika kwa umma, kulingana na wajibu na maadili na uhuru wa vyombo vya habari. Umma wa Tanzania unawajibika kuwa mashahidi, na wala si waandishi wa Kenya.

Tunatambua kuwa serikali na vyombo vya habari ni maadui wa tangu enzi, lakini wenye majukumu tofauti, lakini kila mmoja apaswa kumheshimu mwenzake na majukumu yake.

Kwa misingi hii waandishi wa Tanzania hawaachi kuiheshimu serikali yao hata kama watafichua uoza, rushwa na kutowajibika dhidi yake. Kuheshimu si kulamba miguu. Na kusababisha vita si kufuata maadili yoyote. Ni ushenzi, uchochezi na unyama mkubwa.

Tunakiri; vipo vyombo vya habari au mwandishi mmoja-mmoja waliojibatiza ukasuku. Lakini si wote. Hata Kenya na Marekani wapo kama tulivyoona, wala hatuhitaji nyapara toka Kenya kuwapigia kelele! Sisi wenyewe twatosha.

Nani aliwachagua waandishi wa Kenya kuwa nyapara na walimu wetu? Wanalipwa na nani kwa kazi hiyo? Kwa kujitia mafundi, wanaipa nguvu serikali yao au ugoigoi? Wanapata faida gani kwa kuidhoofisha serikali ya Narc, ili ODM iingie madaearani?

Tunaingia katika Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC) tunahitaji upendo na utulivu kwa nchi zetu na si chokochoko na uchochezi toka upande mmoja. Ule umoja uliokuwepo ulivunjika kwa sababu za ubinafsi toka hukohuko; na sasa dalili zimeanza kuonekana hata kabla ya wakati!

Tunarudia, tunathamini maoni ya kila mtu, yakiwemo ya waandishi wa Kenya, lakini kamwe si kudhalilishwa na mtu kwa sababu tu ya kusigana kwa mawazo na mtindo wa kuendesha mambo yetu.

Biblia inasema, “u-mimi” ni chanzo cha vita, bali tunda la roho ni upendo, utu wema, upole, uvumilivu na tafakuri tunduizi isiyo na vita na kuwapenda maadui hata kuwashangilia kwa mema wanayofanya. Wala hatuhitaji nyapara toka Kenya kwa hili la upendo, umoja, amani na utulivu.`

Baruapepe: omybabu@yahoo.com

Chanzo cha habari, HabariTanzania, Jumanne 03.04.2007:

http://www.habaritanzania.com/articles/1231/1/
Heri-Kulamba-Miguu-ya-Kikwete-Kuliko-ya-Mabeberu