Saturday, October 26, 2013

Tunaingia majira ya theluji (Wintertime) kuamkia Jumapili, 27.Oktoba 2013



Saa 9 usiku kuamkia Jumapili, 27 Oktoba 2013, hapa Norway (Skandinavia) tumebadili majira na kuingia majira ya theluji (Wintertime). Kufuatia na mabadiliko ya majira, tunarudisha saa moja nyuma. 

Tuna tofauti ya masaa mawili na saa za Afrika Mashariki (East African Time = EAT) kwenye majira ya theluji. 

Mfano:

Hapa Norway ikiwa saa 4 za asubuhi,
Tanzania (Afrika Mashariki) ni saa 6 za mchana... 

Mabadiliko ya saa hufanyika mara mbili kwa mwaka.



Jumapili ya mwisho ya Machi, kuingia majira ya Kiangazi (Summertime). Tunasogeza saa moja mbele. Tofauti ya saa moja na Afrika Mashariki.


Jumapili ya mwisho ya Oktoba, kuingia majira ya theluji (Wintertime). Tunarudisha saa moja nyuma. Tofauti ya masaa mawili na Afrika Mashariki.

Friday, October 25, 2013

National Social Security Fund for Tanzanians Living Abroad


Freeman Mbowe, William Ngeleja na Rostam Aziz, wamehojiwa kuhusu kuwa na utajiri mkubwa nje ya nchi



MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja na Mfanyabiashara maarufu, Rostam Aziz, wamehojiwa kuhusu kuwa na utajiri mkubwa nje ya nchi.

Wanasiasa hao wamehojiwa na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na serikali hivi karibuni kwa ajili ya kutafuta mali mbalimbali zilizofichwa nje ya nchi na watu mbalimbai wenye nyadhifa kubwa.

Ingawa watendaji wakuu wa kikosi kazi hicho wamekataa kuthibitisha au kukana kuhusu kuhojiwa kwa wanasiasa hao, Raia Mwema limeambiwa wanasiasa hao ni sehemu tu ya watu zaidi ya 100 wanaochunguzwa na vyombo vya dola.

Kikosi hicho kiliundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na kinaongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hoseah na wawakilishi kutoka Jeshi la Polisi, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na waatalamu wa masuala ya kibenki.

Chanzo cha kuaminika cha kilisema Mbowe ambaye pia ndiye Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alihojiwa kutokana na maelezo kuwa alinunua jumba la kifahari nchini Dubai, Desemba mwaka 2011.

"Kutokana na wadhifa wake kwa umma, Mbowe ilibidi achunguzwe kutokana na ununuzi wa nyumba alioufanya nchini Dubai, Desemba mwaka 2011.

Uchunguzi wake ni mahususi kwa sababu tumefuatilia akaunti zake na ikaonekana hakuwahi kutumia njia ya benki kufanya malipo.

"Hii maana yake ni kwamba kama alifanya malipo, basi alifanya kwa kutumia fedha taslim (cash).

Sasa ni lazima ichunguzwe maana si kawaida kwa kiongozi kama yeye kusafiri na mamilioni yote ya kununua jumba kule Dubai na kulipa cash. Ndiyo maana yeye anafanyiwa uchunguzi mahususi," kilisema chanzo cha kuaminika cha gazeti hili.

Rostam ni miongoni mwa wafanyabiashara maarufu hapa nchini na Raia Mwema limeelezwa kwamba alihojiwa kutokana na kumiliki jumba katika nchi hiyo ya Mashariki ya Kati na imeelezwa pia kuwa ana akaunti kadhaa nje ya nchi.

Dubai ni kimbilio la wafanyabiashara wengi kutokana na nafuu ya kodi inayotolewa na serikali ya nchi hiyo na pia uwepo wa biashara na usalama mkubwa uliopo.

Zaidi ya kuwa mfanyabiashara maarufu, Rostam aliwahi kuwa mbunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na alipata pia kuwa Mweka Hazina wa chama hicho.

Hadi tunakwenda mitamboni, gazeti hili lilikuwa halijafahamu ni kwa sababu ya mali zipi hasa ambazo Ngeleja anazo lakini wakati akiwa Waziri wa Nishati na Madini, kulikuwa na minong'ono kwamba alikuwa miongoni mwa mawaziri vijana wenye ukwasi mkubwa alioukwaa ndani ya muda mfupi.

Alipoulizwa na Raia Mwema kuhusu alichohojiwa alipoitwa na kikosi kazi, Ngeleja alijibu kwa ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu yake ya mkononi; "Samahani, mimi si msemaji wa suala hilo." Hata alipoombwa na mwandishi walau kukanusha au kukataa kuwa alihojiwa – Ngeleja alijibu kwa ufupi, "Ahsante."

Kwa sasa, waziri huyo wa zamani wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete yuko safarini nje ya nchi.

Alipotafutwa wiki hii kueleza upande wake kuhusu alichohojiwa, Rostam hakujibu simu wala ujumbe mfupi wa maneno aliotumiwa na mwandishi.

Mbowe hakuwa tayari kueleza kuhusu kuhojiwa huko ingawa Ofisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene, aliyeeleza kuwa ameagizwa kujibu kwa niaba ya mkuu huyo wa upinzani, alisema; "si jambo la ajabu kwa Mbowe kuwa na mali nje ya nchi kwa vile ni mfanyabiashara na ana biashara hadi nje ya nchi."

Kikosi kazi kinafanya kazi zake katika mazingira ya usiri na tangu kilipoanza kazi mapema mwaka huu, hakijawahi kutoa taarifa rasmi kuhusu shughuli zake.

Mmoja wa wajumbe wa kikosi kazi hicho, Dk. Hoseah alikataa kuzungumza chochote kuhusu watu waliowahoji kwa maelezo kuwa msemaji wa shughuli yao ni Werema.

Werema hakutaka kukana wala kuthibitisha taarifa hii isipokuwa katika mazungumzo ya nyuma na vyombo vya habari aliwahi kusema kwamba ni kinyume cha maadili kwa tume hiyo kutoa taarifa kuhusu watu iliowahoji.

Novemba mwaka jana, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe, alitoa hoja binafsi bungeni akitaka ufanyike uchunguzi wa fedha na mali haramu kutoka Tanzania zilizofichwa katika nchimbalimbali duniani.

Kwa mujibu wa sheria za Tanzania, raia wake hawaruhusiwi kufungua akaunti katika nchi za kigeni pasipo ruhusa ya ofisi ya Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania.

Katika hoja yake binafsi, Zitto alitaka Bunge lipewe nguvu ya kuunda Kamati Teule ambayo itachunguza na kubaini ni akina nani wanamiliki akaunti na mali ughaibuni lakini serikali iliamua yenyewe kuwa ndiyo itafuatilia kwa kutumia vyombo vyake.

Chanzo: Raia Mwema


Wednesday, October 23, 2013

Jicho Pevu: Zilizala La Westgate na Mohammed Ali



Hayawi hayawi hatimaye yamekuwa, zimekuwa siku nyingi za kubashiri, na siku nyingi za kunongonezana kuhusu kilichojiri wakati taifa lilitekwa nyara na magaidi kwa siku nne mtawalia. Wakenya zaidi ya sitini walipoteza maisha yao katika jumba la Westgate lakini hadi sasa Wakenya hawajajua ukweli kuhusu yaliyojiri katika jumba la Westgate. Je ni kweli kuna waliokuwa wametekwa nyara na magaidi na kuzuiliwa katika jumba hilo? Je ni kweli kuna magaidi waliouawa na wanajeshi? Meza ya upekuzi ya Jicho Pevu na Inside Story usiku na mchana wamekuwa wakidurusu kila ukurasa na, kufanya mahojiano na kupitia hatua kwa hatua video za cctv kutoka jumba la Westgate na sasa wako tayari kukusimulia kilichojiri bila kuficha lolote. Meza hii ilifanikiwa picha za pekee kuhusu matukio ya Westgate. Usiambiwe tena tizama makala haya yatakayokujia katika muda usiokuwa mrefu ukiwanaye mwanahabari mpekuzi Mohammed Ali.


Sunday, October 20, 2013

VACANCY - ACCOUNTING & FINANCE MANAGER AT SAPA GROUP IN OSLO

Sapa is the world leader in aluminium solutions – a new company that has joined the aluminium extrusion businesses of Sapa and Hydro. Together, we are shaping a lighter future through a global reach and local presence within extrusions, building systems, and precision tubing. We have 23,000 employees in more than 40 countries, and our headquarters are located in Oslo, Norway.

RESPONSIBILITIES
• Legal accounting and closing in the parent
company (Sapa shared service is doing all
accounting, invoice handling and payments)
• Social charge and other reporting
• Management fee
• Annual reports
• Pension accounting in the group
• Follow up and liquidity forecast
• Group accounting & consolidation
• Special projects

ORGANIZATION
• Accounting and Consolidation

REPORTS TO:
• VP Accounting and Consolidation

WORK EXPERIENCE
• 5 years experience from larger groups
• Closing the books independently
• Preferably experience from one of the
big four audit firms
• Local GAAP and IFRS experience
• Experience from ERP systems preferable

ORACLE
EDUCATION & SPECIFIC SKILLS
• University degree in finance
• English language

PERSONAL CHARACTERISTICS
• Demand strict attention to rules and
procedures, easy to communicate with,
always look for working more efficient

LOCATION
Oslo, Biskop Gunnerusgate 14a

HOW TO APPLY
Please submit your written application no later
than October 31, to Marit H. Engh, HR Manager

If you are interested in the position or if you
have questions, please contact Magnus
Wennersten, Vice President Accounting &
Consolidation, phone: +46 732 57 62 57 and

More vacancies:


Wednesday, October 16, 2013

Norway yapata serikali mpya Jumatano 16.Oktoba 2013 ikiongozwa na Waziri Mkuu, Bi.Erna Solberg wa chama cha Conservative


Waziri Mkuu wa Norway, Bi. Erna Solberg 
Kiongozi wa Conservative Party

Bi.Siv Jensen, Kiongozi wa Progress Party (Waziri wa fedha)


Leo Jumatano, 16 Oktoba 2013, Norway imepata serikali mpya ya mseto ya chama cha Conservative Party (Høyre = H) na Progress Party (Fremskrittspartiet = FrP). Serikali hii inaongozwa na Waziri Mkuu, Bi. Erna Solberg (wa The Conservative Party).

Ifuatayo ni orodha ya baraza lake la mawaziri:

Tord Lien (38, Frp) Waziri wa mafuta na nishati.

 Ketil Solvik-Olsen (41, Frp) Waziri wa uchukuzi.

 Sylvi Listhaug (35, Frp) Waziri wa kilimo na masuala ya vyakula.

 Siv Jensen (44, Kiongozi wa Frp) Waziri wa fedha.

• Solveig Horne (44, Frp) Waziri wa watoto, usawa, ushirikishwaji.

 Anders Anundsen (37, Frp) Waziri wa sheria.

 Robert Eriksson (39, Frp) Waziri wa kazi na ustawi wa jamii.

 Monica Mæland (45, H) Waziri wa biashara na viwanda.

• Vidar Helgesen (45, H) Waziri, Ofisi wa Waziri Mkuu.

 Ine Eriksen Søreide (37, H) Waziri wa ulinzi.

 Thorhild Widvey (57, H) Waziri wa utamaduni na masuala ya makanisa.

 Børge Brende (48, H) Waziri wa mambo ya nchi za nje.

 Bent Høie (42, H) Waziri wa afya.

 Jan Tore Sanner (48, H) Waziri wa serikali za manispaa.

 Elisabeth Aspaker (52, H) Waziri wa masuala ya samaki.

 Torbjørn Røe Isaksen (35, H) Waziri wa elimu.

• Tine Sundtoft (46, H), Waziri wa mazingira.


Tuesday, October 15, 2013

Operation Kimbunga Tanga - Wilayani Mkinga imebaini kuwepo kwa kisiwa cha maficho ya wahamiaji haramu




Kisumo: CCM inaweza kung’oka madarakani


Mzee Peter Kisumo.

Mwanasiasa na kada mkongwe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Peter Kisumo ameonya kuwa chama hicho kinaweza kuondolewa madarakani kutokana na kunyamazia vitendo vya ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za umma vinavyotokea nchini...

Bofya na soma zaidi: Mwananchi


Monday, October 14, 2013

Leo ni kumbukumbu ya Baba waTaifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Waziri Mkuu na Rais wa kwanza wa Tanzania (13 Aprili 1922 – 14 Oktoba1999)




Vacancies




Faculty of Natural Sciences and Technology
Department of Biology

Associate Professor in Biology
(population genetics)

For further information:
Professor Eivin Røskaft
Department of Biology
E-mail: roskaft@ntnu.no
phone: +47 73 596291

or Head of Department
Else Berit Skagen
E-mail: else.berit.skagen@ntnu.no
phone: +47 73 59 60 73

The position reference number is NT-71/13


Associate Professor in Biology
(aquaculture-relevant fish physiology)

For further information:
Professor Elin Kjørsvik
E-mail: elin.kjorsvik@ntnu.no
phone: +47 73 59 63 13
phone: +47 91 89 75 78

or Head of Department
Else Berit Skagen
E-mail: else.berit.skagen@ntnu.no
phone: +47 73 59 60 73

The position´s reference number is NT-72/13

More information about the department can be found on
http://www.ntnu.edu/biology

The application with attachments must be sent electronically through

www.jobbnorge.no

Closing date: 01.12.2013

Please see the full announcement at
www.jobbnorge.no 
or
http://www.ntnu.edu/vacancies

Vacancy



Faculty of Natural Sciences and Technology
Department of Material Science and Engineering

Professor/Associate Professor
in material science and engineering
(aluminium electrolysis)

More information about Department of Material and Engineering and the open position can be obtained from
Professor Geir Martin Haarberg
E-mail: geir.martin.haaberg@ntnu.no
phone: +47 73 59 40 61

or Head of Department
Jostein MÃ¥rdalen
E-mail: mardalen@ntnu.no
phone: +47 73 59 49 15
phone: +47 98 28 39 10

The application should be sent electronically through

The position´s reference number is NT-73/13

Closing date: 22.11.2013

Friday, October 11, 2013

Malawi's President Joyce Banda has sacked her cabinet amid allegations of widespread corruption in government.


President Joyce Banda of Malawi.

Several officials have been caught allegedly with money hidden under their beds and in their cars, reports the BBC's Raphael Tenthani from Malawi. Last month, top finance ministry official Paul Mphwiyo, who was seen as an anti-corruption crusader, was shot and wounded, our reporter says.

Western donors have been urging Ms Banda to tackle corruption.
Malawi is a poor African state, heavily dependent on financial aid from the European Union (EU) and other foreign powers.

'High levels of fraud'
Ms Banda's office said a new cabinet would be appointed in due course, without elaborating.
She called a crisis meeting of the cabinet before her office announced that it had been dissolved, our reporter says.
At a news conference on Wednesday, Ms Banda said she had appointed a special team, made up of police and government officials, to do a financial audit across all government departments.
Our reporter says the shooting of Mr Mphwiyo opened a can of worms with the media awash with reports of unscrupulous civil servants conniving with businessmen to fleece the government of million of dollars through dubious contracts.

Mr Mphwiyo, the budget director in the finance ministry, was shot as he drove into his residence in the upmarket Area 43 suburb of the capital, Lilongwe, on 13 September.

The shooting was "attack aimed at silencing him and the government in the fight against high levels of corruption and fraud", Ms Banda's office said at the time.
Four suspects were arrested over the shooting, our reporter says.
About 10 junior government officials have been arrested so far for suspected corruption, Reuters News agency reports.

Courtsey of BBC News


Tuesday, October 08, 2013

Høyre (The Conservative) na Fremskrittspartiet (Progress Party) zakubaliana kuunda serikali ya mseto. Wanachukua madaraka wiki ijayo.


Waziri Mkuu mteule wa Norway, Bi. Erna Solberg (kulia) na Bi. Siv Jensen, kiongozi wa Progress Party (kushoto) jana usiku kwenye hoteli ya Sundvolden.


Waziri Mkuu mteule wa Norway, Bi. Erna Solberg wa chama cha Høyre (The Conservative) na Bi. Siv Jensen, kiongozi wa chama cha Fremskrittspartiet (Progress Party) jana usiku kwenye hoteli ya Sundvolden wametoa tamko la pamoja kuwa wamemaliza mazungumzo yao na wamekubaliana kuunda serikali ya mseto. Makubaliano hayo yako kwa Kinorwejiani: Politisk plattform for en regjeringutgått av Høyre og Fremskrittspartiet. Hii ni mara ya kwanza kwa Progress Party kuingia madarakani hapa Norway toka kilipoanzishwa mwaka 1973.

Bi. Solberg na Bi. Jensen, wamezungumzia nini watafanya wakiingia madarakani ili kuleta mabadiliko makubwa hapa Norway. Yafuatayo ni baadhi yaliyomo kwenye makubaliano hayo:
  • Umri wa mtu atakayetaka kumleta mke au mme mwenza utakuwa kuwa miaka 24 kuendelea. Kiwango cha chini cha mwaka cha kuonyesha kama mtu anaweza kumudu kumleta mwenza kitaongezwa toka kroner laki moja na nusu kwa mwaka.
  • Muda wa mtu mwenye asili ya kigeni kuomba kibali cha kudumu cha kuishi utaongezwa toka miaka 3 hadi miaka 5.
  • Kabla mtu hajakubaliwa kupewa uraia wa Kinorwejiani, lazima mwombaji afaulu mtihani wa kuzungumza Kinorwejiani na kufaulu mtihani wa uraia.
  • Sheria za uhamiaji zitakazwa kamba. Pale penye nyufa patazibwa. Watu wanaokuja kuomba hifadhi za kisiasa na watakuwa wanachujwa kama tui la nazi. Wale watakaoonekana kuwa wanapaswa kupewa hifadhi watawekwa kwenye kambi za aina yake na wale ambao wataonekana hawafai kupewa hifadhi wataweka kwenye kambi zenye ulinzi tayari kurudishwa walikotoka.
  • Uwezekano wa kumchungulia rafiki, ndugu, jamaa au jirani kuwa amepata kiasi gani cha mapato ya mwaka kwenye orodha ya kodi, sasa basi. Watakaopata nafasi hiyo ni watu na taasisi maalumu zinazoruhusiwa kumwangalia mtu hata pale anapoomba mkopo toka benki.
  • Wataruhusu maduka ya vyakula na masupa maketi kufunguliwa Jumapili. Maduka ya kawaida ya chakula na masupa maketi hayaruhusiwi kufunguliwa Jumapili hapa Norway. Yanayofunguliwa na maduka ya vyakula yasiyozidi mita za mraba 100.
  • Watahakikisha watu ambao hawana kazi na wanapokea msaada wa serikali wa kujikimu na kuweza kuishi wanafanya kitu cha kutolea jasho huo msaada pale inapobidi.
  • Wataimarisha, watakarabati na kujenga haraka njia za mawasiliano na barabara. Moja ya hatua hiyo ni kuanzisha kampuni ya taifa ya ujenzi.
  • Wataimarisha ulinzi na usalama wa raia na nchi. Watahakikisha kuwa wote wanaomaliza chuo cha polisi wanapata kazi kwenye jeshi la polisi. Tofauti na serikali iliyopita ambayo iliongeza idadi  ya wanaoingia kuchukua mafunzo ya upolisi lakini kushindwa kuwaajiri wote waliomaliza.
  • Wataruhusu polisi wa nchi hii kubeba silaha wakiwa kazini. Norway ni nchi chache zilizobaki hapa duniani ambapo polisi wanatembea bila silaha. Wanaruhusiwa kubeba silaha pale tu panapokuwa na shughuli za hatari.
  • Wadau wa elimu wataruhusiwa kuanzisha shule za binafsi na kupata ruzuku kutoka serikalini.
  • Watapunguza urasimu uliokisiri kuanzia ofisi za manispaa hadi za serikali.
  • Watapunguza idadi za manispaa 428 za Norway. Hawajaamua zitakuwa ngapi.
Nawapongeza Høyre na Fremskrittspartiet na namtakia kila la heri Waziri Mkuu Mteule, Bi.Erna Solberg na serikali yake ya mseto.


Semboja, Mwamedi Juma4

Sunday, October 06, 2013

Vacancy - Chief Financial Officer


AVANCE GAS


Avance Gas is eeking an experienced and ambitious Chief Financial Officer (CFO) to lead all fiscal and fiduciary responsibilities for the organization. 

Reporting to and partnering with the Chief Executive Officer (CEO), the CFO will play a critical role in developing and implementing the financial governance framework for Avance Gas and support the growth and eventual public listing of the company.

For more information about the position, 
contact: 

Christian Andersen

at telephone: +47 22 00 48 05.

Application with resume should be sent to:


as soon as possible.


Friday, October 04, 2013

UGANDA 51st INDEPENDENCE CELEBRATION By UGANDA ASSOCIATION IN NORWAY



Venue: Nordberg Kirke Kringsjågrenda 1, 0861 Oslo Norway (A few minutes from Kringsjå or Holestein Tbane Number 3).

Date: Saturday, October 12th, 2013

Time: 07:30P.M. – 03:00A.M. Prompt 

Entry Fee: kr. 100 ( free for children) 

Music By Dj. Erycom. He doesn't just play music, He Keeps the crowd guessing, educated and inspired. 

Join our fellow East Africans for a great evening filled with cultural programmes.


Oslo, Norway



Afrikan History Week ønsker velkommen til årets INDABA FAGSEMINAR - et heldags foredrags- og arbeidsseminar med fokus på teori og metode innen psykologi,flerkulturalitet, atferd og endring.

TEMA: Psykologiske perspektiver på flerkultur, atferd og endring.

INDABA FAGSEMINAR er et årlig fagforum for nye perspektiver på teori og metode. Indaba Fagseminar representerer et ?innenfra-perspektiv? hvor erfarne fagpersoner med afrikansk bakgrunn gir deltakerne et innblikk i teoretisk analyse og praktiske metoder forankret i afrikansk kulturforståelse. Innholdet er relevant og overførbart også i arbeid med andre kulturbakgrunner.

PROGRAM

- Foredrag ved Professor i psykologi, Wade W. Nobles, San Fransisco State University

- Respons-innlegg ved representanter fra norske fagmiljøer

- Spørsmålsrunde og debatt om faglige perspektiver

- Arbeidsgrupper med fokus på metodisk arbeid

HVEM KAN DELTA?

Indaba-seminaret er spesielt tilrettelagt for teoretikere, praktikere og studenter innen akademia, humanistiske fag, forskning, offentlig forvaltning, skoleverk og pedagogikk, barnevern, sosialt arbeid, psykiatri, helsevesen, kultursektor, forebyggende tiltak og organisasjonsliv.

Språk: Hovedforedrag og spørsmålrunde til dette vil foregå på engelsk, mens i andre programposter vil norsk bli anvendt.

PÃ…MELDING: Alle deltakere mÃ¥ melde seg pÃ¥ i forveien. GÃ¥ inn pÃ¥ www.deltager.no/indabafagseminar
 og meld deg pÃ¥ online. PÃ¥meldingsfrist: 14. oktober

INFORMASJON: For mer info om Indaba Fagseminar og andre arrangementer under Ã¥rets Afrikan History Week, se: www.afrikanhistoryweek.com



KONTAKT OSS: Kontakt sekretariatet pr e-post: indaba@afrikanhistoryweek.com


Tuesday, October 01, 2013

NORWAY - Høyre (The Conservative Party), Fremskrittspartiet FrP (The Progress Party), Kristelig Folkeparti KrF (Christian Democratic Party) na Venstre (The Liberal Party) vyashindwa kuafikiana kuendelea na mazungumzo ya kuunda serikali ya Mseto. Høyre na FrP kuendelea na mazungumzo




Baada ya uchaguzi mkuu Norway wiki mbili zilizopita, Høyre (The Conservative Party), Fremskrittspartiet (The Progress Party), Kristelig Folkeparti (The Christian Democratic Party) na Venstre (The Liberal Party) vilipata ushindi wabunge 96 jumla na kuwa na wingi wa Wabunge kwenye Bunge la Norway Stortinget lenye wabunge 168.

Kwa wiki mbili vyama hivyo vimekuwa na mazungumzo ya kuona kama pana uwezekano wa kuunda serikali ya mseto ya vyama vinne.

Viongozi wa vyama hivyo vinne, Bi. Erna Solberg (Waziri Mkuu mteule toka Høyre, H), Bi.Siv Jensen wa Fremskrittspartiet (FrP), Bi. Trine Skei Grande wa Venstre (V) na Bw. Knut Arild Haraide wa Kristelig Folkepartiet (KrF), jana usiku kwenye mkutano wa vyombo vya habari, wamesema; wamekubaliana na kutia saini kuwa Høyre na Fremskrittspartiet waendelee na mazungumzo ya jinsi gani wataunda serikali ya mseto ya vyama viwili kati ya Høyre na FrP, huku KrF na Venstre vibaki nje ya mseto huo, lakini wawe wanawaunga mkono wenzao kwenye masuala ya kila siku Bungeni ili kwamba mseto huo uweze kudumu angalau kwa miaka minne ijayo hadi uchaguzi mkuu mwaka 2017.

Kiitikadi FrF na Venstre vinafanana fanana lakini viko mbali sana na FrP. Hizo tofauti za kiitikadi ndizo zilizofanya KrF na Venstre kushindwa kukubali kuwa kwenye serikali ya mseto na FrP. (Angalia: 


Masuala kadhaa yakiwemo la haki za binadamu wote, wahamiaji na misaada kwa nchi zinazoendelea (KrF) na la mazingira (Venstre) na muhimu kwa vyama hivyo na wako tofauti sana na FrP. FrP kimepata lebo ya kuwa chama kisichopenda watu wenye asili za nchi zingine wanaoishi Norway na kingependa kuziba vyufa zote zinazowafanya wageni na watu wanaokuja kuomba hifadhi za kikimbizi kuja na kuingia kirahisi hapa Norway.

Licha ya kuwa kuna masuala kadhaa yamefanya KrF na Venstre kuamua kukaa nje ya mseto utakaoundwa, lakini kuna mambo mengi tu yao wamekubaliana na Høyre na FrP kuwa japo watakuwa nje ya mseto, lakini serikali ya mseto iyashughulikie.

Kwenye makubaliano hayo (yako kwenye Kinorwejiani: Avtale mellom mellom Venstre, Kristelig Folkepartiet, Fremskrittspartiet og Høyre), vyama hivyo vimekubaliana mengi, baadhi ni haya:

  • Kuhakikisha kuwa serikali ya mseto ya Høyre na Fremskrittspartiet inadumu angalau kwa kipindi hadi uchaguzi mkuu ujao.
  • Kushauriana kwa lolote lile kabla serikali ya mseto kuliamua.
  • Kupunguza urasimu kwenye ofisi za manispaa na za serikali.
  • Kuona kama pana uwezekano wa kupunguza manispaa 428 za Norway
  • Kuongeza ubora wa matibabu kwa wanaotumia madawa ya kulevya na kuona uwezekano wa kununua nafasi za matibabu kwenye hospitali na taasisi binafsi.
  • Kuhakikisha ubora wa elimu mashuleni na vyuoni.
  • Kujenga kwa kasi na kurabati njia za mawasiliano na usafiri.
  • Kuongeza uwezo wa usafiri wa umma kwenye miji mikubwa.
  • Kuongeza askari kwenye jeshi la polisi.
  • Kuona kama pana uwezekano wa kuongeza matumizi ya nchi kutoka kwenye mfuko wa mali asili ya mafuta.
  • Kina baba kuongezewa mapumziko ya wiki 10 kama wakizitaka, mama wazazi anapojifungua.
  • Kuacha kuendelea na utafiti wa kuangalia kuwepo kwa mafuta na gesi kwenye ukanda wa kaskazini ya Norway.
  • Hela za mara moja anazopewa mama mzazi akijifungua kuongezeka.
  • Somo kwenye shule za msingi lililokuwa linaitwa RLE (religion, livssyn og etikk = Religion, Lifestyle and Ethics) litabadilishwa na kuitwa KRLE (Kristendom, religion, livssyn og etikk = Christianity, Religion, Lifestyle and Ethics)

Wamekubaliana kuwa watu wote wanaokuja kuomba hifadhi ya kisiasa na kikimbizi hapa Norway watakuwa wanawekwa kwenye kambi za aina mbili.

Moja: Kwa wale ambao wataonekana kuwa wana nafasi ya kukubaliwa hifadhi watawekwa kwenye kambi zao.

Mbili: Wale wanaonekana hawana nafasi ya kupewa hifadhi watawekwa kwenye kambi za aina yao, tayari kwa kurudishwa walikotoka.

Sheria za uhamiaji zitakazwa kamba na kuzibwa nyufa pale patapoonekana pana nyufa.

na
Mwamedi Semboja.
Oslo.