Sunday, February 03, 2008




Hi folks...
Do you remember Puls Pub at Dronningensgate 22, Oslo?
It´s previous owner, Amjid has bought a new place at
Trondheimsveien in Oslo (Norway).
An opening party in two weeks time. Stay tuned!


For mo´info:

Amjid: mobilephone: +47 96 65 12 65

Hassan: mobilephone: + 47 47 26 21 81


Afunguliwa kesi kwa kumuuliza

swali Waziri Mkuu.....???!!!



Na Reuben Kagaruki

STAILI ya Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa anapokuwa katika ziara mikoani ya kuruhusu wenye kero waulize maswali sasa imezidi kuwa mzigo kwa wananchi, uchunguzi wa kina wa gazeti hili umebaini.

Uchunguzi huo katika ziara kadhaa za Waziri Mkuu umebaini kuwa wananchi wengi wanaomuuliza maswali hasa yanayoonekana kuwa na changamoto za msingi kwa viongozi, wamekuwa wakikumbana na madhila mbalimbali baada ya hapo.

Wakati Watanzania wakiwa hawajasahau sakata la mwanafunzi Allan Shella wa wilayani Ukerewe, Mwanza aliyemhoji Bw. Lowassa juu ya viongozi kuwa na vyeo viwili kwa wakati mmoja na Waziri Mkuu kuahirisha kumjibu na ikaripotiwa kuwa baada ya hapo mwanafunzi huyo alisumbuliwa sana na watu wa Usalama wa Taifa, mwananchi mwingine amejikuta katika hali tete zaidi kiasi cha kuburutwa kortini huku mlalamikaji akiwa kiongozi mwandamizi Serikalini na mteule wa Rais.

Aliyekumbana na balaa hilo safari hii ni mkazi wa Mbeya Bw. Ilonga Elonga (56) ambaye chanzo cha matatizo yake kinaanzia katika ziara ya Bw. Lowassa jijini Mbeya iliyofanyika Oktoba mwaka jana.

Chanzo cha yote

Akieleza kilichotokea, Bw. Elonga aliyeonekana kuwa na simanzi, aliliambia gazeti hili Dar es Salaam wiki hii kuwa anakumbuka ilikuwa ni Oktoba 17 mwaka jana, wakati Bw. Lowassa akiwa ziarani mkoani Mbeya, yeye na wananchi wengine walihudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Makongosi ambapo Waziri Mkuu alihutubia.

Bw. Elonga anaeleza zaidi kuwa kabla ya Bw. Lowassa kuhutubia alitoa nafasi kwa wananchi wenye kero au swali kujitokeza mbele na kutoa dukuduku lao.

Anasema yeye pamoja na wananchi wengine walipopewa nafasi hiyo kila mmoja alihoji juu ya kero aliyoona inawasumbua. Anakumbuka kuwa yeye alihoji ni kwa nini kwa kipindi cha miaka minne tangu 2004 wananchi wa kata hiyo hawakuwa wameomewa mapato na matumizi ya fedha za ujenzi wa sekondari yao ya Kata ya Makongorosi.

Baada ya kuuliza swali hilo, Waziri Mkuu Lowassa alitoa nafasi kwa viongozi husika kujibu swali hilo lakini waliposimama walishindwa kutoa majibu ya kumridhisha Waziri Mkuu kiasi cha kumfanya atoe maagizo ya haraka.

Anasema mwananchi huyo kuwa Waziri Mkuu alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. John Mwakipesile kwenda kijijini hapo Novemba 6, 2007 ili kuhakikisha wananchi wanasomewa mapato na matumizi na kusikiliza kero zao kwa undani zaidi.

Bw. Elonga anakumbuka kuwa hata hivyo, Mkuu huyo wa Mkoa alifika kijijini hapo mwezi Desemba mwaka jana na kabla ya kuitisha mkutano wa hadhara alianza na kikao cha ndani kilichowashirikisha viongozi wenzake akiwemo Mkuu wa Wilaya.

Matatizo yaanza

Anasema kuwa bila kujua kilichojadiliwa na uamuzi uliofikiwa, akiwa kwenye shughuli zake, siku moja alifuatwa na gari la Mkuu wa Wilaya likiwa na askari watatu na kuamrishwa afuatane nao kwani alikuwa akitakiwa kwenye kikao cha Mkuu wa Mkoa.

"Nilipofika waliniuliza kama mimi ndiye Bw. Ilonga Elonga, nikajibu ndiye mimi," alisema na kuongeza kuwa walimuuliza pia kama ni yeye aliyeandika barua ya wasomaji katika gazeti la Majira akilalamikia wananchi kutosomewa taarifa za mapato na matumizi ya fedha za ujenzi wa shule.

Bw. Elonga anaeleza kuwa baada ya kuoneshwa nakala ya gazeti hilo alikiri. "Nilikiri kuandika barua hiyo na nikawaambia pia kuwa hicho ndicho nilichohoji mbele ya Waziri Mkuu," aliongeza.

Baada ya kuwaeleza hivyo alisema Mkuu wa Wilaya alimuuliza iwapo anafahamu alichokiandika au anajikaanga mwenyewe?

"Aliniuliza ni wapi nilipata takwimu hizo na kama ninaweza kuzithibitisha," anaeleza Bw. Elonga na kuongeza kuwa alianza kupata vitisho kwa kueleza kuwa atafungwa. "Niliwaambia kuwa nipo tayari kufungwa lakini haki ya wananchi itajulikana," alisisitiza.

Mbele ya wananchi

Baada ya kutoa msimamo wake huo waliondoka kwenye kikao hicho na kwenda kwenye mkutano wa hadhara huku akishinikizwa na baadhi ya viongozi hao akiri kuwa maelezo aliyoyatoa mbele ya Waziri Mkuu yalikuwa ni ya uongo na kuwaomba radhi wananchi lakini, Bw. Elonga anadokeza kuwa alikataa.

Hata hivyo anasema badala ya kufuata maelekezo waliyokuwa wakimshinikiza yeye alipopanda jukwaani aliwahoji wananchi waliohudhuria mkutano huo kama waliwahi kusomewa mapato na matumizi na wakajibu hapana hivyo akaamua kuendelea na msimamo wake wa kutokuomba radhi huku wananchi wakiamua kususia mkutano baada ya kuona wanazidi kulazimishwa.

Desemba 12, 2007

Siku hii, Bw. Elonga ansema ndipo alipofuatwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi Makongorosi aliyemtaja kwa jina moja tu la Bw. Deus na kumweleza kuwa anatakiwa ofisini kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Chunya, naye akitajwa kwa jina moja tu la Bw. Kombo.Alipofika huko alikuta ameshafunguliwa jalada la kesi ya jinai ya kutoa taarifa za uongo.

Kesho yake alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya Chunya na kusomewa shitaka hilo. Anasema alikana shitaka na kwa sasa yuko nje kwa dhamana lakini anaendelea kupokea vitisho kuwa lazima afungwe.Alisema kuwa baadaye alibaini kuwa mlalamikaji katika kesi hiyo ni Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Bibi Fatuma Kimario.

RC: Sijamfungulia mtu kesi

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. Mwakipesile alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu sakata la mwananchi huyo alisema yeye aliitisha mkutano baada ya kero hiyo kutolewa kama alivyokuwa ameagizwa na Bw. Lowassa na akasema wananchi walisomewa taarifa waliyokuwa wakiilalamikia. Hata hivyo hakuwa tayari kuzungumzia zaidi kesi aliyofunguliwa mwananchi huyo.

"Mpigie simu mama Fatuma (Mkuu wa Wilaya ya Chunya ambaye pia ni mlalamikaji) umuulize jambo hilo mimi sijawahi kumfungulia mtu mashitaka," alisema.

DC:Kesi ipo ila awaeleze ukweli

Naye DC Fatuma alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu malalamiko ya mwananchi huyo alijibu:

"Mwambie akueleze ukweli wa mambo, mtu hawezi kufunguliwa kesi kwa kuhoji ukweli...muulize akueleze vizuri, mbane hakuna mtu anayeweza kuuliza swali akapelekwa mahakamani hii nchi iko huru hakuna Mtanzania anayeweza kuuliza swali akafikishwa mahakamani."

Alipoelezwa kuwa Bw. Elonga alipoona wananchi hawasomewi mapato na matumizi ndipo alipoandika barua ya wasomaji akikumbushia yale aliyoyaeleza mbele ya Bw. Lowassa DC Fatuma alisisistiza:

"Mwambie akupe barua hiyo utaelewa matatizo yake...muulize ni kwa nini ashitakiwe? Mtanzania aliye huru hawezi kuuliza swali akafunguliwa mashitaka."

DC Fatuma pia akahoji kitendo cha mwnanchi huyo kuzungumza na waandishi akiwa Dar es Salaam badala ya Mbeya lilikotokea tukio.

"Ilikuwaje afunge safari hadi huko kwenu (Dar es Salaam)? Hivi huku Mbeya hakuna waandishi wa habari hadi atoke Chunya hadi Dar es Salaam" Kwa nini hakufuata taratibu zinazohusika," alihoji DC huyo na kumshauri mkazi huyo kama kuna vitisho anavipata akatoe taarifa polisi au aende mahakamani.

"Hakuna anayemtisha, kama anapata vitisho afungue kesi nyingine ya kumshitaki huyo anayemtisha," alisema na kuongeza:

"Kama kesi ipo mahakamani yeye anaogopa nini? Mahakama haiongozwi na mtu, inasimamia haki...Tungoje sheria ichukue mkondo wake." Hata hivyo DC huyo alishindwa kuweka bayana iwapo yeye ni mlalamikaji katika kesi hiyo na ni suala gani hasa lililomfanya ahusike katika kumfungulia mashtaka mwananchi huyo.

Mambo yamezua jambo..........



Makundi ya vijana Kenya sasa
yawageukia wanawake
wavaa suruali

NAIROBI, Kenya

HALI ya machafuko nchini imezidi kuchukua sura mpya baada ya kutoka katika siasa na kuingia katika ukabila sasa hali hiyo imebadilika tena na kuingia katika jinsia. Hali hiyo ya kijinsia imekuja baada ya kundi la vijana kupiga marufuku wanawake wote kuvaa suruali kwa kile wanachodai mwanamke wa kiafrika hapaswi kuvaa suruali zaidi ya sketi na gauni.

Hawa vijana hawataki hii...

Wanataka hii

Tukio hili lilitokea jana katika mji wa Naivasha baada ya kundi la vijana kuanza kuwasakama wanawake wote waliokuwa wamevalia suruali na kuwalazimisha wazivue huku likitangaza kuwa litahakikisha wanawake wanavaa sketi na magauni tu. Katika kituo cha mabasi cha mjini Naivasha wanawake ambao walikuwa wamevalia suruali walijikuta katika hali ngumu baada ya kundi hilo la vijana kuwalazimisha washuke kwenye matatu na kuwaamuru kuwa hadi wavae vizuri ndio waendelee na safari zao.

Mmoja wa wanawake ambaye alikumbwa na dhahama hiyo, Miriam Wairimu ameelezea jinsi alivyonusurika kuvuliwa nguo hizo hadharani baada ya kundi hilo kumteremsha kwenye matatu huku likimlazimisha avue nguo hiyo. Nililazimishwa kushuka kwenye matatu na nilikuwa sijafika mjini kwa muda wa wiki moja iliyopita ndio nikakutana na kundi hilo la vijana likinilazimisha kwamba nivue suruali, alisema Miriam ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha kompyuta katika mji huo.

Mwanamke wa kiafrika hapaswi kuvaa suruali na tunaka kuhakikisha jambo hilo linabaki hivyo hivyo hapa Naivasha, alisema mmoja wa vijana katika kundi hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe. Nilitimua mbio huku kundi hilo likinifukuza hadi nilipookolewa na mama moja ambaye alinipatia sketi katika duka la kushona nguo, aliongeza dada huyo. Amelalamika kwamba hali hiyo ni ya unyanyasaji kwa mwanamke.

Nilitimua mbio huku kundi hilo likinifukuza hadi nilipookolewa na mama moja ambaye alinipatia sketi katika duka la kushona nguo, aliongeza dada huyo. Amelalamika kwamba hali hiyo ni ya unyanyasaji kwa mwanamke.
Wasanii nchini wa kike wana bifu
wenyewe kwa wenyewe


Ushirikiano baina ya wasanii wa kike umekuwa ni hafifu sana. Maneno haya yanazungumzwa na wengi sana hapa nchini. Inakuaje wasanii wa kike hawapendani wenyewe kwa wenyewe? Inawezekana ni wivu unaowasumbua au kila mmoja anajiona bora kuliko mwenzake?

Habari hii imefanyiwa uchunguzi wa kina na timu nzima ya Dar411 na kubainika ya kwamba ni ukweli kabisa kwamba kuna sababu maalumu zinazowafanya wasanii wa kike nchini wasiwe kitu kimoja lakini habari hizi hazikuweza kutambulika zaidi.

Kuna sababu ya kwamba kila mtu anajiona bora kuliko mwenzake na hivyo kumsikilizia mwenzake. Inawezekana wazi ya kwamba hakuna anayemvutia pozi mwenzake lakini. Mdau mmoja wa muziki wa nyumbani anayetambulika kwa jina la Safina Kassanga aliidhibitishia Dar411 ya kwamba alishawahi kuwaona wasanii fulani wa kike wakiliana pozi laivu na wakapishana bila ya hata salamu bila ya sababu yeyote.

Mdau huyu kwa maoni yake na timu ya dar411 alisema ni wivu tu unaowasumbua wanamuziki wa kike kwani kila mmoja anajiona bora kuliko mwenzake. Naye mwanamuziki wa kutoka kundi la Wakali Kwanza, Makamua alisema ya kwamba yeye haelewi kwanini wasanii wa kike hawana ushirikiano kama walivyo wao, ila ameshashuhudia wasanii wa kike wakiliana mikausho. Msomaji wa safu hii, je unaweza ukasema ni kwanini wasanii wa kike nchini wana chuki za wenyewe kwa wenyewe bila sababu malumu?



Sifikirii kuwa na mume sasa

Sifikirii kuwa na mume sasa
Huyu si mwingine bali ni Hawa, mwanamitindo anayeipeperusha vyema bendera ya Tanzania huko nchini China. Ni msichana mrembo na mwenye haiba yenye mvuto. Dar411 iliweza kumbamba mrembo huyu na kuweza kuzungumza naye machache.

Hawa alichonga na Dar411 na kusema tangu awasili nchini kwa likizo yake amekuwa akisumbuliwa sana na wanaume na ahadi kemkem bila kujua lengo lake kuu ambalo la kutotaka kusikia neno kuolewa. Mwanamitindo huyu alisema amekuwa akitumia muda wake mwingi kwenye masuala ya umodo hivyo kuweka mambo ya mapenzi benchi kwakuwa muda wake bado haujamruhusu kuwa mke wa mtu.

"Sifikirii kuolewa siku za karibuni kwakuwa fani yangu hairuhusu kabisa mtu aliyeolewa kabisa, na kwa upande wangu naona ni sahihi kabisa kuolewa wakati huu ambao nang'aa kwenye fani hii. Mwanamitindo huyu ametokea mkoa wa Dodoma kwenye familia ya wasichana wanne na shoo yake ya kwanza kufanya catwalk ilikuwa ni Golden Tulip na baada ya hapo alipata mkataba wa kufanya kazi huko nchini China ambapo mpaka sasa anafanya kazi zake nchini humo.

Kutoka Dar 411

Post office closures loom

Norway's postal service has won government approval to shut down more than 120 of the country's remaining 300 post offices. Postal services will be moved into retail stores in areas hit by closures.

Norway's postal system says it's "modernizing" by moving postal services into retail stores.

PHOTO: ERLEND AAS / SCANPIX


It's the latest in a series of post office closures nationwide that began in 2001. The closures have been spurred by declining demand and attempts to cut costs.

The new closures will leave Norway with 179 traditional post offices and 1,280 "post in boutique" locations.

Customer surveys, according to postal officials, show that postal customers like being able to send or collect packages in the same place where they buy bread and milk. "We’re glad the government is supporting continued modernization," said Dag Mejdell, spokesman for Posten Norge.

The stores where the postal service leases space and has set up postal counters also tend to be open later than traditional post offices have been.

The post office shutdown will affect 650 employees, but they'll either be offered new positions within the postal service or retraining and help to find a new job.

Aftenposten English Web Desk/NTB


Saturday, February 02, 2008


Jakaya Kikwete awakuna wengi

waandishi wetu, dar, dodoma


WABUNGE, wasomi na wananchi wa kawaida, wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hotuba yake ya mwishoni mwa mwezi uliopita, hasa kwenye kipengele cha kuwataka matajiri kuchagua moja — biashara au uongozi.

Wasomi kadhaa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wamesema maadili ya uongozi yamevurugwa kwa kiasi kikubwa na kueleza kwamba Rais Kikwete hapaswi kuongojea sheria mpya ya maadili, badala yake anapaswa kuchukua hatua sasa.

Wakizungumza na MTANZANIA katika majengo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mlimani, baadhi ya wasomi wa fani ya sheria walisema Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1985 haijafanyiwa kazi, hivyo hakuna haja ya maboresho ya sheria hiyo.

Mwanaharakati maarufu ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, alisema Rais Kikwete ametangaza vita ngumu, hasa pale inapoaminika kuwa mawaziri wake wengi ni wafanyabiashara.

Profesa Baregu alisema katika vita hiyo, Rais Kikwete hana mbinu nyingine za ushindi zaidi ya kuamua kung’ata jongoo na kuamua kuvunja urafiki uliopo na wasaidizi wake.

“Mimi sioni sababu kwa nini Rais asubiri sheria mpya, sheria iliyopo bado haijafanyiwa kazi— imelazwa usingizi. Ninachokiona hapa Rais ametangaza vita na marafiki zake, sasa ili ashinde vita hii, hana choice (hiari) zaidi ya kufumua Bazara lake la Mawaziri.“Suala la viongozi wetu kukiuka maadili ya uongozi limepigiwa kelele sana, huwezi kuwa wewe rais wa nchi, kisha ukafanya biashara Ikulu. Waziri wa Miundombinu ndiye anayesimamia usafiri wa anga, hapo hapo waziri huyo anashirikiana na waziri mwenzake kuanzisha shirika la ndege, kama si kutaka kuua ATC, ni nini?” Alihoji.

Profesa Baregu aliongeza: “Hawa viongozi ambao ni wafanyabiashara, wamekuwa wakijigamba kuwa rais ni wa kwao, wamemweka madarakani kwa fedha zao. Wananchi nao wanasema wao ndiyo waliomchagua rais kwa kura zao. Sasa Kikwete aamue kuwa Rais wa wafanyabiashara au Watanzania,” alisema.

Kwa upande wake, Dk. Sengondo Mvungi, msomi na mwanasheria, alisema: “Tatizo la nchi hii kuna kudharauliana, suala hili la watu kuchanganya biashara na uongozi, wapinzani wamelisema siku nyingi, lakini wamekuwa wakionekana malofa.“Mimi nafurahi Rais alivyosema kuwa suala hili wamekubaliana katika vikao vyao vya NEC, nasema hivi kwa sababu CCM ndiyo waliopuuza na kudharau maadili ya viongozi. Walipolitosa Azimio la Arusha baharini kule Zanzibar, walitupilia mbali na masharti ya maadili ya uongozi, kitu ambacho Mwalimu Nyerere alisikitika sana.

“Kama Rais kazinduka leo, tunamwambia Rais ana kazi ngumu, kama kweli ana dhamira ya dhati ya kurejesha maadili ya uongozi, afumbe macho, afute urafiki na watendaji.

“Suala la uongozi na biashara ni suala la mgongano wa maslahi, sheria ya sasa inakataza mgongano wa maslahi sasa suala la kusubiri sheria mpya halipo, unasubiri sheria ipi wakati iliyopo hujaitumia.

“Watu waliohusika na ufisadi wa BoT wanajijua wawajibike. Tatizo la mawaziri wa serikali hii, hawataki kujiuzulu wakamwachia Rais apumue. Hawataki kujiuzulu hadi wafukuzwe you have to kick their butts ndipo wajue kwamba hapa hatutakiwi,” alisema kwa sauti ya juu.Katika hatua nyingine, wananchi wameunga mkono wazo la Serikali kuanzisha mchakato utakaowazuia viongozi wa siasa kujihusisha na shughuli za kibiashara wakati wawapo kwenye utawala wa kuwatumikia wananchi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Dar es Salaam jana, baadhi ya wananchi walisema uamuzi huo umechelewa na hauna budi kushughulikiwa na kutekelezwa mara moja

Mkazi wa Mwenge, Plasduce Kahaya, alisema hatua hiyo ni nzuri kwani itapunguza wanasiasa kuwa na tabia ya kujilimbikizia mali kama baadhi yao wanavyofanya sasa.

“Utakuta mwanasiasa anapokea mshahara na posho nyingi, na ni mfanyabiashara, kitendo kinachoziba nafasi za watu wengine,” alisema.

Mkazi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Ester alisema hana imani kama sheria hiyo inaweza kupita endapo itapelekwa bungeni kutokana na wabunge wengi kuwa wafanyabiashara.

“Nahisi haitafika po pote maana wabunge karibu wote ni wafanyabiashara, sasa sidhani kama watakuwa tayari kujihukumu pale bungeni,” alisema Ester.

Naye, mwanasheria ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema hatua hiyo ni nzuri, kwani itatoa viongozi wa kweli, wawajibikaji na wenye nia ya kuwatumikia wananchi.

Akizungumza juzi katika hotuba yake ya kila mwisho wa mwezi, Rais Kikwete, alisema serikali inatarajia kuanzisha mchakato wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili viongozi wachague kufanya jambo moja, kati ya biashara, ubunge au uwaziri.

Kikwete alisema, upo ushahidi wa kuwapo kwa migongano ya masilahi kwa baadhi ya mawaziri au wabunge katika suala hilo. Alisema hata pale pasipokuwapo na dalili za wazi, hisia za kupata manufaa yanayotokana na nafasi zao, matokeo yake ni kupoteza imani na kutilia shaka uadilifu wa viongozi.

Mjini Dodoma, wabunge kadhaa wameipokea hotuba ya Rais Kikwete kwa hadhari.

Miongoni mwao ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (CUF), ambaye pamoja na kuunga mkono, alishauri kuwapo kwa utafiti wa kina katika marekebisho hayo.

Akizungumza na MTANZANIA ofisini kwake bungeni mjini Dodoma jana, Rashid, ambaye ni Mbunge wa Wawi, alisema ni jambo zuri kwa Rais kutambua kuwa kiongozi wa kisiasa anayetumikia umma anatakiwa ashiriki kikamilifu kutimiza wajibu wake.

Alisema marekebisho hayo hayapaswi kuhusisha Sheria ya Maadili ya Viongozi pekee, bali hata sheria nyingine, akisisitiza kuwa marekebisho lazima yazingatie hatima ya kiongozi mhusika baada ya kustaafu, kwa kuwa uzoefu unabainisha kuwa viongozi wengi waadilifu huishia kuwa na hali duni kimaisha.

“Lazima kuwepo na tafsiri ya neno biashara katika marekebisho hayo kwa kuwa zamani katika miaka ya 1960 na 1970 kiongozi alikuwa hata akifuga kuku haruhusiwi, sasa tuelezwe ni biashara gani hizo?” Alihoji.

Mbunge huyo alisema sheria ya sasa si mbaya kama kungekuwapo na utashi wa kutosha wa kisiasa katika utekelezaji wake.

Akitoa mfano alisema yupo kiongozi aliyeingia madarakani akiwa hana kampuni wakati akitangaza mali zake, na akatoka katika uongozi akiwa anamiliki kampuni, tena bila kutoa maelezo ameipataje.Naye, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), aliunga mkono moja kwa moja uamuzi wa Rais Kikwete.

“Najisikia furaha sana kumsikia Rais akisema hivyo. Binafsi Spika wa Bunge aliwahi kunituma Canada, katika Bunge lao upo utaratibu unaomtaka mbunge kutojihusisha na biashara. Niliporejea niliandika muswada binafsi ambao naruhusiwa- nikamkabidhi Katibu wa Bunge nikipendekeza sheria ya maadili ibadilishwe ili mawaziri wabunge waepuke kuingia katika mtego wa mgogoro wa maslahi, ilikuwa Machi 27, mwaka jana.

“Lakini Katibu wa Bunge alinijibu suala hilo haliwezi kushughulikiwa kwa sababu linahitaji mabadiliko ya Katiba. Lakini kwa sasa baada ya kumsikia Rais, wasiwasi wangu ni kwamba utekelezaji na hatimaye kukamilika kwa suala hili utachukua muda mrefu mno, mfano ni ahadi ya Rais bungeni Desemba 30, 2005, alipoahidi kufanyia kazi suala la udhibiti wa fedha za kampeni,” alisema.

Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni (CCM), alisema hatua hiyo ya Rais kutaka marekebisho ya Sheria ya Maadili ya Viongozi ni muhimu, na akasisitiza kuwa ni lazima taifa lifike mahali liwe na viongozi wanaowajibika kwa wananchi.

“Chanzo cha sehemu kubwa ya ufisadi ni viongozi kutumia madaraka yao ya ki-uongozi kufanya maamuzi ambayo yanawanufaisha. Sasa marekebisho ni vizuri zaidi yakatazama kwa kina suala hili kwa ajili ya kudhibiti,” alisema.

Hata hivyo, alisema katika marekebisho hayo kazi ya ubunge ni lazima ikatambuliwa kuwa ni ‘kazi kamili’ yenye kipato kamili na kusisitiza kuwa mara kwa mara ubunge si kazi yenye mazingira ya kuwapo na mgongano wa maslahi.

Wakati huo huo, Marekani imempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU).

Akizungumza na MTANZANIA jana, Balozi wa Marekani hapa nchini, Mark Green, alisema Marekani imefurahishwa na uchaguzi huo, na ana imani katika uongozi wake kutakuwapo mabadiliko makubwa.

“Nina imani na Kikwete, ni mtu makini asiyeyumbishwa, na mwenye kufanya uamuzi wa busara, hivyo kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa AU kutasaidia kuleta maendeleo barani Afrika,” alisema Balozi Green na kuongeza:

“Kikwete ni mtu anayeheshimika ndani na nje ya Afrika, kwa kuwa anaheshimika inaweza kusaidia katika utatuzi wa migogoro inayoendelea ndani ya bara hili.”

Rais Kikwete alitangazwa kuwa mwenyekiti mpya wa AU juzi baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa umoja huo, John Kufuor ambaye ni Rais wa Ghana, kumaliza muda wake.

Wakati Kikwete anaingia kwenye madaraka hayo ya kuliongoza bara la Afrika, anakabiliwa na changamoto mbalimbali yakiwamo machafuko ya kisiasa nchini Kenya na mapigano yanayoendeshwa na vikundi vya waasi katika nchi za Sudan, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC.

Mbali ya migogoro ya kisiasa, changamoto nyingine zinazomkabili Rais Kikwete ni kukuza uchumi na kupambana na magonjwa kama malaria, ukimwi, kifua kikuu na vifo vya watoto wachanga na wajawazito.

Ripoti hii imeandaliwa na waandishi Khamis Mkotya, Primtiva Pancras, Thomas William na Godfrey Dilunga.




Ofisa Usalama wa Taifa

atumbukia ufisadi BoT


Waandishi Wetu, Dodoma


KAMPUNI mbili ambazo zimetumiwa kuchota mabilioni Benki Kuu (BoT) zimegundulika kuwa zinamilikiwa na Ofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa mwenye cheo cha juu kabisa. Kampuni hizo ni Clayton Marketing Ltd na Excellent Services Ltd ambazo ni miongoni mwa kampuni 22 zilizotumiwa kuiba Sh bilioni 133 za BoT kupitia Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Habari zimeeleza kuwa ofisa mmoja wa ngazi ya juu ndani ya idara hiyo ndiye anatajwa kama mmoja wa wakurugenzi. Habari za uhakika ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa kampuni hizo zilitumiwa kuchota kiasi kikubwa cha fedha kwa kisingizio cha kazi maalumu ya kitaifa.

Kampuni ya Clayton inatajwa kuchota kwa wakati mmoja dola za Marekani 500,000 kutoka Benki Kuu. “Nyaraka tu iliandikwa kwenda Benki Kuu kwamba tafadhali lipa hizo pesa kwa kazi maalumu, unajua wakati huo hatukujua hizo fedha zinakwenda wapi, sasa tunafahamu,” kilidokeza chanzo kimoja cha habari.

Kampuni hizo mbili ni miongoni mwa kampuni zilizolipwa Sh bilioni 42.9 na hakuna nyaraka yoyote iliyowasilishwa kuthibitisha malipo hayo. Kampuni zingine katika kundi hilo ni G&T International Ltd, Mibale Farm, Liquidity Service Ltd, M/S Rashtas (T) Ltd, Kiloloma and Brothers, Karnel Ltd na Malegesi Law Chambers (Advocates) inayomilikiwa na Bedery Malegesi.

Pia gazeti hili limebaini kuwa ofisa huyo kutokana na nafasi yake, ni miongoni mwa watu ambao idara yake imehusishwa katika kuundwa kwa tume maalumu iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza tuhuma hizo. “Kwa kazi yake yeye ni mtu mkubwa katika kamati ile kwani ndiye anayeshughulikia masuala yote ya kigaidi, kiuhalifu wa kimataifa ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa,” kilidokeza chanzo chetu cha habari.

Mwenyekiti wa kuchunguza ufisadi huo, John Mwanyika alipofuatwa na gazeti hili mjini Dodoma aeleze uhusiano wa Ofisa huyo wa Usalama wa Ikulu na kamati yake alisema kwamba hamfahamu huyo mtu na kamati yake inahusisha watu watatu na wala haihusishi watu wa Usalama wa Taifa.

“Sina taarifa za hizo kampuni unazoniuliza na wala huyo mtu simfahamu,” alisema Mwanyika wakati akizungumza na gazeti hili ambalo lilitaka ufafanuzi kama ofisa huyo anahusika kwenye kamati yake. Tume ya kuchunguza suala hilo inaongozwa na Mwanasheria Mkuu kwa kushirikiana na Mkuu wa Polisi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Lakini vyanzo vya habari vilithibitisha kuwa Ofisi ya Usalama wa Taifa imeombwa kuhusishwa katika kuchunguza suala hilo kama ambavyo imekuwa inashiriki katika matukio mengine ya uhalifu. Kampuni ya Excellent Service Ltd ambayo imesajiliwa kama inashughulika na masuala ya upokeaji na usafirishaji wa mizigo, wakurugenzi wake wakati huo walimiki asilimia 100 kila mmoja akiwamo Ofisa Usalama huyo.

Kampuni hiyo ofisi zake zinaelezwa kuwa ziko Mtaa wa Sokoine kitalu namba 11649. Oktoba 5, 2004 mwenzake alijiuzulu na akateuliwa mtu anayeitwa Massimo Fanneli kuwa Mkurugenzi. Hisa za Sabbas ambazo ni 100 zilihamishiwa kwa Fannel baada ya kulipwa Sh milioni 5. Kampuni hiyo hadi kufikia Desemba 19 mtaji wake uliongezeka kutoka 500,000 hadi kufikia milioni 5.

Alipotakiwa kuzungumzia kama kampuni zilizoanzishwa na Ofisa Usalama huyo zilikuwa ni kwa ajili ya shughuli za Serikali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Philip Marmo alisema jana kuwa Serikali haijafikia hatua ya kuanzisha kampuni katika idara yake nyeti ya kama ya Usalama wa Taifa.

Alisema kutokana na hali hiyo ni wazi kuwa kampuni anazodaiwa kuanzisha ofisa huyo mwandamizi zilizotajwa katika ubadhirifu wa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) hazihusiani na Idara ya Usalama wa Taifa.

"Mimi sifahamu kama ana kampuni lakini kwa mujibu wa Azimio la Zanzibar, anaruhusiwa kuwa na kampuni, lakini zisiingiliane na nafasi yake kwa maana asitumie nafasi yake katika uendeshaji wa kampuni zake. Sasa hivi suala hilo la kampuni zilizohusika na ubadhirifu linashughulikiwa na vyombo vya sheria, mimi siwezi ku comment kitu hapo, tusubiri sheria ifanye kazi," alisema.



Kenya ya leo hivi,

ya kesho itakuwaje?

na Abdul Mohammed

MATUKIO ya mauaji, ubakaji, uporaji mali na kila aina ya vurugu, zinazotawala nchini Kenya kwa sasa, zinanifanya nikumbuke mwaka 2005.

Mwaka huo wa 2005, nilikuwa nikiishi Kenya, katika mji wa Kisumu, nikifanya kazi na taasisi moja binafsi, ya Vigiha Community Development Organisation (VCDO).

Kwa kuwa taasisi hiyo haikuwa na shughuli nyingi za kila siku, nikiwa katika mji huo, nilikuwa nafanya kazi katika magazeti ya Nation, katika ofisi zake za Kisumu.

Nilikuwa nikifurahia hali ya mji mdogo wa Kisumu, ulioko karibu kabisa na Ziwa Victoria, na ambao ni ngome kuu ya kiongozi wa upinzani, Raila Odinga.

Naukumbuka mji wa Kisumu ambao pia unajulikana kwa jina la Lake Side City (yaani mji ulio pembezoni mwa Ziwa), kwa namna ulivyokuwa umetulia, ukiwa hauna aina yoyote ya ghasia wala vurugu nyingi, kama ilivyo katika mji wa Nairobi, ambako habari na hisia za hofu ya wizi na vurugu nyingine, zilikuwa zikituogopesha wageni kama sisi.

Nikiendelea kuukumbuka mwaka 2005, kumbukumbu zangu nyingi bado ziko nchini Kenya, na hususan katika mji wa Kisumu.

Naikumbuka hoteli ya Kimwa, hoteli maarufu kwa wageni watumiao mabasi ya Akamba, wanaoelekea Uganda. Hiyo ilikuwa ni sehemu ya kukutana na Watanzania wenzangu, hususan wanafunzi wanaokwenda masomoni Uganda, na hata wafanyabiashara.

Kiswahili chao wakati wa kuagiza chakula, kilitosha kunifanya nibaini kwamba hawa ni Watanzania. Utawasikia wakisema: “Naomba kuku na chipsi.” Huna sababu ya kuhoji. Unajua huyo ni Mtanzania, kwa kuwa kama angekuwa Mkenya, ungemsikia akisema: “Nipe kuku na chipsi”, na kama ni Mganda, basi ungemsikia akizungumza Kiingereza.

Kimwa ni hoteli ambayo nilikuwa nimezoea kunywa kahawa, kiasi cha wahudumu wa hoteli hiyo kunizoea, na mara nyingi walikuwa wakisema: “Yule Mtz anayependa kahawa,” kila wanapotaka kunitambulisha kwa wengine.

Nakumbuka, maduka makubwa maarufu kama ‘Super Markets’ ya maeneo ya Ukwala na Nakumatt, ambayo yalikuwa yakiupendezesha mji mdogo huo wa Kisumu, na wakati mwingine nilikuwa nikiingia kwa ajili ya manunuzi.

Nikiendelea kuikumbuka Kisumu, napakumbuka Mon-Amii, sehemu ambayo tulikuwa tukikutana kwa ajili ya kuangalia mechi za soka, hususan Ligi Kuu ya England.

Naikumbuka Mon-Amii, kwa mambo mengi, kwa kuwa mbali na kuwa klabu maarufu ya usiku, kina dada nao hujazana mahali hapo kwa ajili ya biashara zao. Nawakumbuka kina dada hao, wataagiza soda na kusogea karibu na alipo mwanamume, na wakati mwingine, akitoka nje tu, watamsalimia na kumkonyeza na kadhalika.

Naikumbuka pia hoteli ya Kimwa Annex iliyopo maeneo ya Manyatta. Nakumbuka marafiki zangu walivyokuwa wakinichukua kwa ajili ya burudani ya muziki wa Ohangla, dansi maarufu la Wajaluo.

Namkumbuka Tony Nyadundo, msanii ambaye alikuwa maarufu kwa ngoma ya Ohangla, na namna alivyojizolea umaarufu katika mji wa Kisumu na nyimbo zake kusikika kila kona, na hata ndani ya mabasi ya daladala, ambayo wenyewe wanayaita matatu.

Nakumbuka nilivyoweza kupata marafiki wa makabila mbalimbali, ingawa Wajaluo ni wengi Kisumu, wako watu wa makabila mengine ambao nilizoeana nao.

Nilikuwa na marafiki wa makabila ya nje ya Kisumu, kama vile Waluhya, Wakisii, Wakikuyu na hata Wasomali, ambao hawakusita kunialika kula nao futari katika mwezi wa Ramadhan, na kunichukulia kama mwenzao.

Nikiwa Kisumu, nilijiona kama niko nyumbani. Nilikuwa nakwenda kucheza mpira na Wajaluo ambao mazungumzo yao uwanjani, yalikuwa ni Kijaluo kitupu, huku Kiswahili kikizungumzwa mara chache, lakini mpira ulitosha kuniongezea marafiki.

Haikuchukua muda, nilijiona kama mwenyeji, kwa kuwa mitaani, nilikuwa nasalimiwa mara kwa mara na watu ambao nilikuwa nacheza nao mpira.

Nawakumbuka Wasomali ambao niliwahi kucheza nao mpira, lakini pia naikumbuka timu ya Victoria FC, ambayo pia nilikuwa nakwenda kufanya nao mazoezi pale kwenye Uwanja wa Railway. Nakumbuka nilivyojionea utamaduni mpya katika timu hiyo.

Kila baada ya mazoezi, tulijikusanya pamoja na kufanya maombi tukiwa tumeshikamana. Maombi hayo yaliyokuwa yakiendeshwa kwa lugha ya Kiingereza, yalilenga kumshukuru Mwenyzi Mungu, kwa kumaliza mazoezi salama bila hata mmoja wetu kuumia.

Aidha, maombi hayo yalilenga kumuomba Mungu atuwezeshe kufika nyumbani salama na pia kufanya mazoezi salama siku inayofuata.

Ingawa yalikuwa maombi yenye mtazamo wa dini ya Kikristo, nami nikiwa Muislamu, bado nadiriki kusema kwamba yalinivutia, na nikiri hapa nilifarijika wakati wote kwa namna tulivyoonyesha kumnyenyekea Mungu.

Nakumbuka pia marafiki ambao mara zote walinifanya nikae kijiweni na kuzungumza nao hadi usiku nikiwa Kisumu, na hasa maeneo ya Railway, na kurudi nyumbani kwangu eneo la Milimani saa tatu, na wakati mwingine saa nne usiku, bila hofu.

Nilipapenda sana Kisumu. Hata siku zangu za mwisho za kutaka kuondoka zilipowadia, nilipowaambia marafiki zangu kuhusu Kisumu, waliniambia Kisumu ni rahisi kuingia, lakini kutoka tabu. Kwa hiyo, kama unaondoka, bila shaka kuna siku utarudi au unaweza usiondoke kabisa.

Nikiwa Tanzania, kwa sasa nasoma habari za kusikitisha nchini Kenya, na hasa za wanawake kubakwa, raia wasio na hatia kuuwa, nyumba na maduka kuchomwa, hali ambayo inanifanya niwasiliane na wenzangu kujua hali ikoje huko kwao.

Naanza kuambiwa kwamba hoteli ya Kimwa, niliyokuwa nimezoea kunywa kahawa, imechomwa moto, na kwamba ipo katika hali mbaya. Nikiuliza sababu, naambiwa mmiliki ni Mkikuyu.

Naambiwa Kimwa Annex, mahali palipokuwa na ukumbi wa muziki, nilipowahi kupelekwa kwa ajili ya Ohangla, nako hakufai hata kidogo, hoteli imechomwa moto. Nauliza sababu, naambiwa mmiliki ni Mkikuyu!

Naambiwa zaidi kwamba ile Super Market ya Ukwala, kwa sasa haitamaniki. Imevunjwa na watu kuingia ndani na kuondoka na bidhaa walizoweza kuzibeba.

Pale Mon-Amii, naambiwa kwa sasa hapakaliki, na hata zile shamrashamra za usiku, zimepungua na siku nyingine hazipo, watu wametawaliwa na hofu.

Mji wa Kisumu naambiwa umekuwa si ule wa 2005 niliouzoea, bali umekuwa tofauti kabisa na ile hali ya urafiki na undugu niliyoizoea haipo tena, hofu imetawala.

Wale marafiki Wakikuyu niliokuwa nao Kisumu, nakumbuka mmoja nilipenda kumtania kwa kumwambia ‘A Kikuyu in the Luo land’ (Mkikuyu katika ardhi ya Wajaluo), leo hii nikiwauliza vipi, wananiambia wamekimbia Kisumu. Kisa, Wajaluo hawawataki na wao wana hofu ya kuuwawa.

Katika kuishi kwangu Kisumu na Kenya kwa ujumla, nilitambua kuwapo kwa tatizo la ukabila, lakini niliona kama ni jambo la kawaida na si kubwa kama nilivyosikia na hali ilivyo kwa sasa.

Niliona baadhi ya watu wakisakama makabila mengine lakini si katika hali ambayo ingeweza kuzaa balaa na kuna wakati mwingine nilifurahi kuona kama ukabila ilikuwa ni sehemu ya kufanyiana dhihaka za kawaida.

Kwa mfano nakumbuka Wakikuyu walikuwa wakihusishwa na tabia ya kupenda sana fedha na hiyo ikanikumbusha namna Wachaga wanavyotaniwa hapa Tanzania.

Nilizoea sana kuwasikia Wajaluo wakizungumza lugha yao na mara chache sana Wakikuyu, nakumbuka mara yangu ya kwanza kumsikia Mkikuyu akizungumza kwenye simu nilibaki nashangaa nikamwambia nini hicho unaongea.

Nilimtania kwa kumwambia kwamba lugha yao ni ya ajabu na haifai kuzungumzwa kwenye simu, nilimwambia wanavyoongea ni kama vitu vinagonganagongana, mwenyewe alicheka akaniambia umezoea sana Kijaluo.

Leo hii Kenya nasikia kabila limekuwa ni jambo kubwa na mwanzo wa balaa kiasi cha kufikia hatua ya watu kuuana, watu kuhama makazi yao na kuwa wakimbizi ndani ya nchi yao.

Ukabila imekuwa chanzo cha wasichana kubakwa na wengine kuzikwa wakiwa hai.

Ukabila umehusishwa moja kwa moja na matokeo ya uchaguzi wa Desemba 27 mwaka jana, ambao aliyetajwa kuwa mshindi, Mwai Kibaki inaaminika kwamba hakushinda kihalali.

Badala yake wafuasi wa mshindi anayeaminika kuwa ndiye aliyeshinda kihalali, Raila Odinga hawakupewa ushindi wao na Tume ya Uchaguzi Kenya, na hivyo wameamua kupambana na Wakikuyu.

Wakikuyu nao wamechoka na kuamua kupambana na makabila mengine yaliyoungana dhidi yao, nao wanafanya uharibifu na vurugu kadri inavyowezekana.

Hadi hivi sasa zaidi ya watu 1,000 wameripotiwa kufariki dunia, idadi ambayo inaweza kuongezeka kama juhudi hazitafanyika katika kuleta amani.

Watoto na raia wengine wasio na hatia wamejikuta katika wakati mgumu kwa sababu tu wanatoka kabila Fulani, licha ya ukweli kwamba hawahusiki kwa namna yoyote na wizi wa kura unaodaiwa kufanywa.

Unasoma habari ya waumini wa dini fulani wakiwa wamechomwa moto wakiwa ndani ya Kanisa, sababu tu wanatoka kabila fulani. Baada ya hapo, unasoma habari za watu wa kabila fulani kuhamishwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi ili tu wasidhuriwe na watu wa kabila fulani.

Unaendelea kupata habari ya kusikitisha kwamba hata kama wewe ni Mkikuyu umefunga ndoa na Mjaluo, kama mkeo anaishi eneo la Wakikuyu au Wajaluo basi atalazimika kuhama na kurudi kwao, vinginevyo atauawa na watu wa kabila lako ambao hawamtaki.

Wakati nasoma habari hizo zote naanza kufikiria mambo mengi. Nafikiria kwamba hali ya aina hiyo itaendelea hadi lini, kwa watu ambao mwaka 2005 niliwaona kama ndugu wanaoishi pamoja.

Nafikiria kwamba hali Kenya ni mbaya, lakini naamini haiwezi kuachwa ikawa hivyo na kwamba juhudi ni lazima zifanyike kukomesha mauaji haya, hususan ya raia wasio na hatia.

Naifikiria Kenya ya sasa na hali itakavyokuwa siku zijazo, najenga hisia kwamba watu hawa 800 na zaidi waliokufa na wanaoweza kuendelea kufa wanaweza kuwa mwanzo wa tatizo kubwa kwa Kenya ya miaka ijayo kuliko hivi sasa.Najaribu kufikiria namna watu wanavyokufa na kuziacha familia zao katika wakati mgumu. Nafikiria watu wanaokufa na kuacha watoto wadogo, na wake zao wakiwa katika hali ya huzuni.

Nafikiria hali ikiendelea hivi miaka 15 au 20 ijayo hali itakuwaje? Vipi mtoto ambaye leo hii ana miaka mitatu au mitano, ambaye miaka 15 au 20 ijayo, atakuwa anahangaika na maisha.

Hapa namfikiri mtoto ambaye mama yake atashindwa kumlipia ada kwa ajili ya masomo ya sekondari, mtoto ambaye atakuwa na shauku ya kusoma na kumuuliza mama, baba yangu yuko wapi.

Nafikiri kuna mama ambaye ataona tabu kumhadithia mwanaye, lakini kuna jasiri ambaye atamwambia kwamba baba yako aliuawa na Wajaluo, Wakikuyu na au Wakalenjin.

Naifikiria hali atakayokuwa nayo baada ya kuambiwa kwamba watu hao hawakuishia kumuua tu, bali walichoma moto nyumba, waliua mifugo na kuzika watu wengine wakiwa hai.

Namfikiria mtoto huyu atakavyokuwa katika hali ya unyonge na masikitiko, namfikiria namna ambavyo atakubali yaishe na kuanza kujitafutia maisha bila elimu, elimu ambayo pengine angeweza kuipata kama baba yake angekuwa hai, kwani baba yake alikuwa na mipango na malengo mazuri ya kumsomesha.

Hata hivyo ameshindwa kupata elimu kwa sababu tu Wajaluo au Wakikuyu au Wakalenjin walimuua baba yake.

Namfikiria mtoto mwingine ambaye mara baada ya kumuuliza mama yake alipo baba, mama yake akaanza kwa kumwambia baba yako aliuawa na Wakikuyu au Wajaluo au Wakalenjin, naufikiria unyonge atakaokuwa nao.

Namfikiria mama huyo ambaye hatosita kumwambia kwamba watu hao walimuua baba yako, wakawauwa na ndugu zako wote na kuwabaka ovyo wasichana na kisha kupora mali na ndio maana wametuacha katika hali ya umasikini.

Nafikiria hali itakuwaje mtoto huyu akiwa tofauti na yule wa kwanza, nafikiria huyu akiamua kusema maadui zangu toka leo ni Wajaluo au Wakikuyu au Wakalenjin.

Naendelea kufikiria hali itakuwaje miaka 15 au 20 ijayo iwapo kutakuwa na watoto wa aina hii mmoja mmoja katika familia 800 ambazo wazazi wao wameuawa kinyama.

Natafakari hali itakavyokuwa iwapo watoto hawa wote wataamua kulipa kisasi cha kuuawa kwa baba zao, mali zao kuporwa na dada zao kubakwa.

Hapa naifikiria Kenya ya kesho. Nazungumzia miaka 15 au 20 ijayo, kama vurugu hizo zinazoendelea na kuandamana na mauaji zisipokomeshwa, hali katika Kenya ya miaka hiyo itakuwaje? Je; hali haiwezi kuwa kama Rwanda? Tusubiri!


Housing prices pick up



Average sales prices for houses and flats rose 3 percent nationwide from December to January. Real estate brokers weren't as happy with the monthly year-on-year figures, though.

Related stories:

Average prices were just 0.3 percent higher in January than they were in January 2007. That's the lowest level of annual growth measured since 2003.

Prices for detached houses were up 3.9 percent from December to January, and 5.8 percent from January 2007.

Prices for attached row-houses and duplexes were up 2.6 percent from December to January and 4 percent since January of last year.

Average sales prices for condominiums (leiligheter), which make up the vast majority of sales, brought the real estate market down. They were up 2.1 percent from December, but down 2.5 percent from January of last year.

Norway's robust real estate market first started showing signs of cooling off last summer, possibly a result of rising interest rates and high prices that kept would-be buyers out of the market.

Housing demand remains high in the Oslo area, however, prompting some brokers to speculate that prices will start moving up again.

The price survey was conducted by research firm Econ for Norwegian real estate brokers' associations (Norges Eiendomsmeglerforbund (NEF) and Eiendomsmeglerforetakenes forening (EFF) and online sales site Finn.no.

Aftenposten English Web Desk
Nina Berglund/NTB


Royal family won’t

boycott Olympics

Despite Prince Charles of England joining in the growing boycott of the Olympic Games in Beijing, the Norwegian Royal Family has no plans to cancel its trip to China this summer.

Prince Charles has long shown sympathy for Tibetan human rights and has decided to stay away from the Olympic Games in China.

PHOTO: AP/MATT DUNHAM

Related stories:

Earlier this week, it was revealed that Prince Charles would stay away from the Beijing Olympics this summer, reportedly as a demonstration of his concern for the human rights situation in Tibet and China.

Tibetan rights organizations have been pressuring the Norwegians to drop the Olympic Games as well, but Aftenposten.no reports that King Harald, Queen Sonja and Crown Prince Haakon will attend the summer games.

"The Royal Highnesses, the King and Queen, and the Crown Prince will represent Norway at the Olympic Games in Beijing, but the programme is not set yet," said an e-mail sent to Aftenposten.no from the Royal Palace.

"Respect for Human Rights is important, and the Norwegian authorities are dealing with the problem through an ongoing dialogue with the Chinese," it continued.

The leader of the Norwegian Tibet Committee, Chungdak Koren, responded with an appeal to the Royal House to follow suit after Prince Charles.

Koren said he was "disappointed", and urged the Royal family to stay way from the opening ceremony.

He also expressed his extreme disappointment that the International Olympic Committee (IOC) will not allow Tibet to send its own athletes to the games.

"We’ve done all the formalities correctly and cannot understand why the IOC won’t let Tibet participate with its own athletes, along the same lines as Palestine, Taiwan and Hong Kong," Koren said.

Tibet has been under Chinese control since 1951.

Tibet’s spiritual leader, the exiled Dalai Lama, received the Nobel Peace Prize in Oslo in 1989.

Aftenposten's reporter
Joacim Lund

Aftenposten English Web Desk
Catherine Stein



Friday, February 01, 2008

Kikwete tells public leaders to:

CHOOSE:

Politics or private business?



-States far-reaching plans to tighten existing leadership code of ethics

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

PRESIDENT Jakaya Kikwete has announced plans for sweeping reforms to the existing leadership ethics legislation that would make it illegal for cabinet ministers and members of parliament to be involved in politics and at the same time hold supervisory positions in private companies doing business with the government.

In a surprise move, the president declared yesterday that the planned review of the Public Leadership Code of Ethics Act of 1995 would in effect compel cabinet ministers and MPs to make a choice between politics and private business.

Currently, there are no distinct laws in the country which guard against such conflict of interest, with politicians often known to also hold key positions in private companies that do business with the government.

In his end-of-the-month address to the nation last night, Mr Kikwete said: ’’I would like to talk about political leaders such as ministers and MPs being also directly involved in business dealings. There is evidence of conflict of interest among some of them.’’

Without naming any names, he continued: ’’Even where there is no clear evidence, there is a general perception that such public leaders are using their administrative positions for personal gain. This leads members of the public to lose confidence in and question the integrity of our leaders.’’

He described the planned move for reforms to the current ethics laws as one of national interest, ’’which should help a lot in restoring the public’s respect of their leaders.’’

He said the matter had been discussed during the CCM central committee in Dodoma on Tuesday this week, ’’and we reached a common understanding.’’

According to Mr Kikwete, even capitalist countries of the West have clearly defined boundaries that separate national public leadership duties from private business undertakings.

’’Such countries have a system that requires anyone with business interests to stop engaging in those businesses once he or she becomes a member of parliament or cabinet minister, and place those business interests in the hands of trustees until such a time as they cease to be public leaders.’’

’’It is my intention to introduce such a system to our country. Our leaders must now choose between doing business or becoming an MP or cabinet minister. Therefore, I plan to start a process for the review of the Public Leadership Code of Ethics Act so that it incorporates such a system,’’ the president explained in his national address broadcast on radio and television.

The announcement by President Kikwete is in sharp contrast to the stance taken by his predecessor, Benjamin Mkapa, who it has been established was actively engaged in various private business activities during his tenure at State House stretching from 1995 to 2005.

It is understood that Mkapa and the then first lady, Anna Mkapa, established a private company (ANBEM Limited) in 1999, with themselves registered as sole directors, shareholders and ’entrepreneurs’, and the company’s listed physical address located within the official State House walls in Dar es Salaam.

In 2002, ANBEM Ltd went on to obtain hefty loans totalling over 750m/- from both the National Bank of Commerce Limited and CRDB Bank. Although timely repaid, the NBC loan to ANBEM Ltd was granted at a time of heated national debate over the privatization process surrounding the once state-owned bank - which the government had sold off to South Africa´s ABSA Group for a reported total price of just 15bn/- for 70 per cent majority shares in 2000.

It has also been established that in December 2004, Mkapa teamed up with his then senior cabinet minister, Daniel Yona, to form another private company, Tanpower Resources Limited, which was then given ownership of the previously state-run Kiwira Coal Mine after another dubiously ’fast-tracked’ privatisation process.

All this happened when Mkapa was still serving as president and Yona as minister for energy and minerals, respectively.

The reports of the ex-president’s apparent business dealings have triggered much social commentary and debate, especially with regard to the ethical considerations therein of his actions.

While one school of thought argues that he did not break any laws, another contends that the actions - being mainly geared at ensuring personal gain - could well be interpreted as blatant abuse of office.

Issues of possible conflict of interest and undue influence, on the part of a sitting president endeavouring to balance official responsibilities and private business affairs, have inevitably been brought up in the Mkapa debate. However, the ex-president has maintained a steadfast silence, preferring to respond when pressed with the simple refrain that he is now a ’retired politician’ and would not like to be dragged into public debates.

HOTUBA YA MHESHIMIWA,

JAKAYA MRISHO KIKWETE,

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO

WA TANZANIA, KWA WANANCHI,

31 JANUARI, 2008



Ndugu Wananchi;

Ninayo furaha kwa mara nyingine tena kuzungumza nanyi kupitia utaratibu huu mzuri wa mawasiliano baina ya Rais na wananchi wa nchi yetu.

Jambo la kwanza ninalopenda kulizungumzia linahusu uzingatiaji wa sheria na taratibu za uhamiaji na kuishi nchini.

Ndugu Wananchi;
Tarehe 23 mwezi huu, nilimaliza ziara ya siku kumi Mkoani Kagera. Jambo moja nililoliona kwenye ziara hiyo ambalo sikufurahishwa nalo, ni ukiukwaji wa sheria na taratibu za uhamiaji na uingizaji mifugo nchini.

Kwa muda sasa, raia wa nchi jirani zinazopakana na Mkoa wa Kagera wamekuwa wakiingia na kuishi nchini mwetu kwa vibali vya viongozi na watendaji wa vijiji na kata. Baadhi ya watu hao pia wamekuwa wakiingiza mifugo kwa vibali vya viongozi hao hao.

Wageni hao wamekuwa wanaingia na kuishi nchini isivyo halali. Sheria na taratibu za uhamiaji zinatoa mamlaka hayo kwa Maafisa Uhamiaji tu na si vinginevyo. Viongozi na watendaji wa vijiji na kata hawana mamlaka hayo. Hivyo basi, vibali vyote walivyotoa viongozi hao si halali na havitambuliki. Napenda kurudia kauli yangu niliyoitoa Mkoani Kagera kwamba ni marufuku kwa kiongozi au mtendaji wa ngazi yoyote ile nchini kutoa kibali cha mgeni kuingia au kuishi nchini kama siyo Afisa wa Uhamiaji.

Ndugu wananchi;
Wageni wanaoishi nchini kwa kutumia vibali ambavyo havikutolewa na Idara ya Uhamiaji wanaishi isivyo halali. Wenzetu hawa wanatakiwa kufanya yafuatayo. Kwanza wajitokeze na kutoa taarifa kwa Maofisa Uhamiaji, Wilayani au katika vituo vya mpakani. Pili, iwapo watachagua kuishi nchini, wafuate taratibu zilizowekwa kuomba kibali cha kuishi nchini. Idara ya Uhamiaji ndiyo itakayoamua. Tunawapa siku sitini za kufanya hivyo. Baada ya hapo, hatua zipasazo za kisheria zitachukuliwa kwa wale ambao watakuwa hawakufanya hivyo. Nilipokuwa Mkoani Kagera niliwaagiza Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya kufuatilia utoaji wa vibali unaofanywa na viongozi na watendaji wa vijiji na kata katika maeneo yao. Nimewataka wawachukulie hatua zipasazo za kinidhamu watumishi hao wa umma pamoja na kuwabana wahamiaji haramu kufuata sheria za uhamiaji za nchi yetu au warudi makwao. Napenda kusema kuwa maagizo hayo ni kwa Wakuu wote wa Mikoa na Wilaya nchini kwani inawezekana matatizo haya yanaweza kuwepo katika mikoa mingine.

Najua kwamba kuna Watanzania wenzetu wanaohifadhi wahamiaji haramu kwa kuwa wananufaika kwa kuwafanya vibarua au wafanyakazi wao. Ukweli unabaki pale pale kwamba wanatakiwa waingie na kuishi nchini kwa kufuata taratibu zinazotambulika kisheria. Sheria za nchi, na sio manufaa ya mtu au watu binafsi, ni lazima zizingatiwe.

Ndugu Wananchi;
Jambo lingine baya linalofanyika katika mpaka wetu na nchi jirani Mkoani Kagera ni kuruhusu mifugo kuingia nchini holela. Hiki ni kitendo ambacho kinakiuka taratibu zinazotawala uingizaji wa mifugo kutoka nchi za nje. Pia ni kitendo cha hatari kwani kinaweza kupelekea mifugo yenye maradhi kuingia nchini bila kudhibitiwa na kusababisha maafa makubwa nchini. Kanuni na taratibu zimewekwa kisheria kutawala mifugo kuvuka mipaka na kuepusha hatari za namna hiyo zisitokee.

Jambo linalonishangaza ni kwa nini viongozi wetu hawa hawajifunzi kutoka kwa majirani zetu. Wakati wote tulipofanya zoezi la kurudisha makwao wakimbizi au wahamiaji wasiokuwa halali na mifugo yao wenzetu waliweka sharti la mifugo hiyo hiyo iliyotoka kwao ichanjwe kwanza kabla ya kuvuka mpaka hata kama mifugo hiyo ilitokea nchini kwao na kuja kwetu. Nilidhani hili lingekuwa fundisho kwa viongozi wetu hawa kuwa thabiti kuhakikisha kuwa mifugo kutoka nchi jirani inachanjwa kabla ya kuvuka mpaka kuja Tanzania. Lakini, hawajali kufanya hivyo. Mkuu wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi Watendaji wa Wilaya na viongozi na watendaji wa vijiji na kata kuhakikisha kuwa hakuna mifugo inayoingia nchini holela. Lazima sheria na kanuni husika zizingatiwe.

Aidha, nimeelezwa juu ya kufahamika kuwepo vivuko haramu kadhaa mpakani. Nimesema nilipokuwa Kagera na narudia tena leo kwamba, maadamu vivuko hivyo vimejulikana lazima tuvidhibiti. Kadhalika tuanzishe vituo mpakani vya kupokelea mifugo na kila anayeingia na mifugo lazima apitie hapo na kupata idhini husika. Nimetaka viongozi wenzetu hao wasimuonee haya mtu yeyote anayeingiza mifugo nchini kinyume cha sheria na taratibu zilizopo. Kadhalika viongozi na watendaji wanaozembea wachukuliwe hatua kali za kinidhamu mara inapobainika kuwa mifugo imeingia kinyume na taratibu katika maeneo yao.

Kama ilivyo kwa uhamiaji usio halali, tatizo la kuingiza mifugo kinyume na utaratibu linaweza kuwepo mikoa mingine nchini. Hivyo, maagizo haya ni kwa mikoa yote na wilaya zote nchini. Pia yanaihusu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo. Lazima Wizara itoe uongozi katika jambo hili muhimu kwa usalama na maendeleo ya mifugo yetu nchini. Napenda kuwakumbusha Watanzania wenzangu kuwa hakuna nchi yoyote duniani inayoruhusu mifugo kuingia holela. Si vizuri Tanzania kuwa ndiyo nchi pekee inayofanya hivyo. Wenzetu na hata hao majirani zetu wanatustaajabu.

Ndugu Wananchi;
Jambo la pili ninalopenda kulizungumzia ni matatizo yanayoukabili uchumi wa dunia hivi sasa. Bado bei ya mafuta iko juu sana na kuathiri uchumi wa nchi zote duniani tajiri na maskini ingawaje nchi maskini zinaathirika zaidi. Hili si jambo geni kwetu. Napenda kurudia kauli zangu za siku za nyuma kwamba, hatuna uwezo mkubwa wa kujikinga na athari za bei za mafuta. Hata hivyo, hatuna budi tuendelee kuwa waangalifu na hasa wabanifu katika matumizi ya mafuta. Tuepuke matumizi yasiyo ya lazima.

Wakati huo huo tunaendelea na juhudi za kuzalisha nishati mbadala kutokana na mimea hususan miwa, mawese na mbono-kaburi (jatropha). Juhudi hizo zikifanikiwa zitatusaidia kupunguza mzigo wa mafuta tunayoyaagiza kutoka nje. Nafurahi kwamba juhudi zetu zina muelekeo mzuri na katika miaka michache ijayo tutaanza kunufaika na matunda yake. Pamoja na hayo tunaendelea na juhudi za utafutaji wa mafuta na gesi asilia hapa nchini. Mpaka sasa leseni 22 za utafutaji mafuta na gesi asilia zimetolewa na kazi inaendelea katika hatua mbalimbali. Tuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu atujaalie rehema zake na sisi tujaaliwe kugundua mafuta mengi hapa nchini yatakayotosheleza mahitaji yetu na ziada ya kuuza nje.

Ndugu Wananchi,
Tatizo lingine kubwa linaloukabili uchumi wa dunia sasa linatokana na matatizo yanayoukabili uchumi wa Marekani. Uchumi wa taifa hilo ambao ndiyo mkubwa kuliko wowote duniani umekuwa unapita kwenye misukosuko kwa miezi kadhaa na katika wiki chache zilizopita hali ikawa ngumu zaidi. Kasi ya ukuaji wa uchumi imepungua na thamani ya dola imeshuka. Serikali ya nchi hiyo imeanza kuchukua hatua za kukabiliana na matatizo hayo. Lakini, kwa kuwa uchumi wa Marekani ndiyo uchumi mkubwa kuliko wowote duniani na uchumi wa nchi nyingi duniani una uhusiano nao, matatizo ya uchumi wa nchi hiyo huathiri nchi nyingi. Na sisi Tanzania hivyo hivyo.

Nimeelekeza wachumi wetu wafanye uchambuzi wa kina juu ya athari hizo na kushauri hatua za kuchukua kupunguza makali yake. Moja ya jambo ambalo liko wazi ni lile la kushuka kwa thamani ya dola ya Kimarekani. Sisi tunaweka sehemu kubwa ya akiba yetu ya fedha za kigeni katika dola za Kimarekani. Ni dhahiri kwamba kushuka kwa thamani ya dola za Kimarekani kunatupunguzia uwezo wetu wa kuagiza bidhaa nchi za nje.

Uchunguzi wa Akaunti ya EPA

Ndugu Wananchi;
Jambo la tatu ambalo nimepanga kuliongelea leo ni hili suala la ukaguzi wa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje na hatua zinazoendelea kuchukuliwa baada ya taarifa ya ukaguzi kutolewa.

Ndugu Watanzania wenzangu;
Kwa mara nyingine tena nawapongeza na kuwashukuru wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young kwa kazi nzuri waliyoifanya na kutoa taarifa ya kina kuhusu matatizo yahusuyo matumizi ya fedha za Akaunti hiyo. Nawashukuru pia Watanzania wenzangu kwa kuunga mkono hatua tulizochukua na tunazoendelea kuchukua kuhusu suala la Benki Kuu. Hata hivyo, nasikitishwa na taarifa ninazozipata kuhusu kuwepo uvumi mwingi unaoenezwa na baadhi yetu kuhusu suala hili. Baadhi ya uvumi huo umekuwa unapotosha ukweli na kuwachanganya wananchi. Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba wanaoeneza uvumi na uongo kuacha kufanya hivyo. Aidha, nawasihi wananchi wawe watulivu na wavumilivu.

Napenda kuwahakikishia kuwa, Serikali inayo dhamira ya dhati ya kulifuatilia suala hili mpaka mwisho wake ujulikane. Mwisho ambao utakuwa na maslahi kwa taifa letu. Pamoja na yote yatakayofanywa, tunataka kuhakikisha kuwa fedha zilizolipwa kinyume cha utaratibu zinarudishwa. Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wenzake, yaani Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU wameanza kuchukua hatua. Nimewataka watoe taarifa kwa wananchi mara kwa mara kadri inavyowezekana pamoja na haja ya kuwa waangalifu kutokutoa mengi yahusuyo uchunguzi wanaoufanya ili ushahidi usiharibike.

Nawaomba Watanzania wenzangu tuwe na subira. Naamini kazi hii itakamilika ndani ya kipindi cha miezi sita tuliyowapa. Napenda kurudia ombi la Serikali kwa wananchi wenye taarifa zitakazosaidia katika uchunguzi na hatua katika suala hili waisaidie kamati yetu hiyo.

Ujio wa Rais Bush

Ndugu Wananchi;
Natumai mmesoma na kusikia taarifa katika vyombo vya habari kuhusu ziara ya Rais George W. Bush wa Marekani katika nchi yetu kunako katikati ya mwezi Februari, 2008. Tunaendelea kukamilisha ratiba na itakapokuwa tayari tutawapeni taarifa. Hilo ndilo jambo langu la nne leo.

Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba Watanzania tumpokee mgeni wetu huyu kwa mujibu wa mazoea na desturi za ukarimu wa Kitanzania. Huu ni ugeni mkubwa na wa heshima kubwa kwa nchi yetu. Rais Gerorge Bush ameipa heshima kubwa nchi yetu kwa kuamua kutumia sehemu kubwa ya ziara yake ya Bara la Afrika hapa kwetu. Ameonyesha upendo mkubwa kwetu nasi tumuonyeshe hivyo hivyo. Nawaomba Watanzania tujitokeze kwa wingi siku hiyo kumpokea mgeni wetu huyo mashuhuri.

Ziara hii ni uthibitisho wa kuimarika kwa mahusiano kati ya Marekani na Tanzania. Mahusiano hayo mazuri yameinufaisha nchi yetu. Marekani sasa ni moja ya nchi zinazoongoza kwa kutoa misaada ya maendeleo kwa Tanzania. Tangu mwaka 2003 kwa mfano, imekuwa inatoa msaada mkubwa ambao umetusaidia sana katika mapambano yetu dhidi ya maradhi ya UKIMWI nchini Tanzania. Kadhalika, Marekani imetusaidia sana katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria nchini.

Ndugu Wananchi,
Wakati wa ziara yake hapa nchini, Serikali ya Marekani inatarajia kutiliana sahihi msaada mkubwa wa maendeleo unaoelekezwa katika kuboresha miundo mbinu ya barabara, umeme na maji. Kwa msaada huo utakaotolewa kupitia Programu ya Mfuko wa Changamoto ya Millenia utatusaidia kutatua baadhi ya matatizo yaliyoonekana sugu katika baadhi ya maeneo hapa nchini.

Pamoja na hayo, ziara ya Rais George Bush nchini mwetu itasaidia kuitangaza nchi yetu na kuinufaisha sana utalii na uwekezaji hasa kwa soko la Marekani na marafiki zake. Tayari katika miaka miwili hii tumeshuhudia ongezeko kubwa la watalii wa Kimarekani kutembelea nchi yetu. Hivi sasa Wamarekani ndiyo wanaoongoza kwa idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi za Ngorongoro na Serengeti. Naamini baada ya ziara ya Rais wao watalii wengi zaidi wa Kimarekani watakuja. Hali kadhalika, wawekezaji wengi wa kutoka Amerika watajenga imani ya kuja kuwekeza nchini.

Ndugu Wananchi,
Wapo watu miongoni mwetu na hata nje wanajaribu kueneza uvumi wa uongo na kuihusisha ziara hii na masuala ya Makao Makuu ya Kamandi ya Afrika ya Jeshi la Marekani. Ni uongo na uzushi mtupu. Ziara hii haihusu hayo. Masuala hayo si agenda na wala Marekani haijaiomba Tanzania kuwa mwenyeji wa Kamandi hiyo. Nawasihi Watanzania wenzangu tupunguze hii tabia ya kuzusha na kueneza uongo. Tunajitia hofu wenyewe na wenzetu bila sababu. Haina tija yoyote. Nawaomba tujitokeze kwa wingi kumpokea mgeni wetu huyu. Aondoke nchini salama na arejee kwao akiwa na kumbukumbu nzuri ya nchi yetu na watu wake.

Hali ya Kenya

Ndugu Wananchi;
Jambo la tano ninalotaka kulizungumzia ni hali ya kisiasa na kiusalama ya nchi jirani na rafiki ya Kenya. Kwa kweli inatusikitisha na kutuletea simanzi kubwa. Mioyo yetu inauma kuona na kusikia yanayotokea nchini humo. Jitihada yangu ya kuzungumza na pande zote zinazohasimiana pamoja na zile zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa na wenzetu wengine bado hazijazaa matunda. Sisi hatutachoka na wala hatutaacha kuzungumza na pande zinazohusika kuhusu kuacha uhasama, kuacha na mapigano na kutafuta maridhiano kwa njia ya mazungumzo.

Tunaahidi kuendelea kuiunga mkono Kamati ya Mhe. Kofi Annan (Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa), Rais Mstaafu, Mhe. Benjamin Mkapa na Mama Graca Machel. Viongozi wetu hao wanaifanya kazi hiyo kwa niaba ya Umoja wa Afrika wanastahili msaada wetu na kuungwa mkono nasi. Aidha, tutaendelea kushirikiana na viongozi wenzetu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kusaidia juhudi za upatanishi. Napenda kutumia nafasi kurudia tena yale maombi yangu kwa viongozi wa PNU na ODM na wananchi wote wa Kenya kuyapa mazungumzo nafasi ya kumaliza tofauti zao. Mapanga, marungu na hata bunduki zisipewe nafasi, kamwe hazitasaidia.

Tutenganishe Uongozi na Biashara

Ndugu Wananchi;
Jambo la mwisho ninalotaka kulizungumzia linahusu maadili ya uongozi nchini. Hususan napenda kulizungumzia suala la viongozi wa siasa Mawaziri na Wabunge kuwa pia watu wanaojihusisha na shughuli za biashara moja kwa moja. Upo ushahidi wa kuwepo migongano ya maslahi kwa baadhi. Lakini, pia, hata pale ambapo hakuna dalili za wazi, hisia za kupata manufaa yanayotokana na nafasi zao hutawala. Matokeo ya yote hayo ni watu kupoteza imani na kutilia shaka uadilifu wa viongozi wetu.

Ndugu Wananchi;
Nchi za wenzetu hasa zile za kibepari zinazo taratibu nzuri za kushughulikia hali hizo. Wenzetu wanao utaratibu unaomtaka mtu mwenye shughuli za kibiashara anapokuwa Mbunge au Waziri kuacha kujishughulisha na biashara zake. Unakuwepo utaratibu rasmi unaotambuliwa kisheria wa wadhamini wanaoendesha hizo shughuli bila ya yeye kujihusisha nazo. Anapoacha uongozi wa siasa kama atapenda atachukua tena mali yake na kuendelea na shughuli zake.

Ni makusudio yangu kuwa utaratibu huu tuuanzishe hapa nchini. Viongozi wetu wachague kufanya jambo moja kwa wakati mmoja ama biashara au Ubunge na Uwaziri. Kwa ajili hiyo ni makusudio yangu kuanzisha mchakato wa kufanya marekebisho ya Sheria ya Maadili ya Uongozi ili tuingize utaratibu huo.

Ndugu wananchi;
Ni jambo lenye maslahi kwa nchi yetu na litasaidia sana kujenga heshima ya viongozi wa umma mbele ya macho ya wananchi. Nafurahi kwamba suala hili tumelizungumza katika kikao maalum cha Kamati Kuu ya CCM tulichofanya Dodoma juzi tarehe 29 Januari, 2008 na tumeelewana. Ni matumaini yangu kuwa sote tutaunga mkono.

Mwisho, nawatakia kila la heri kwenye shughuli zenu. Tuendelee kushirikiana kuijenga na kuiendeleza nchi yetu.

Asanteni sana kwa kunisikiliza

Air Tanzania Corp.Ltd

yakodisha dege bovu


Ni Airbus ya kampuni ya Liberia,
inayofanyiwa ukarabati El Salvador

KAMA vile kashfa ya mahujaji haikutosha, na kama vile mlolongo wa kashfa za manunuzi mengine ya asasi mbalimbali za serikali hazijaitosheleza Serikali ya CCM, Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) nalo limeanza kukumbwa na kashfa kubwa ya ukodishaji wa ndege nzee kutoka kampuni ya Liberia.

Ukodishwaji huo wa ndege kubwa aina ya Airbus 320 MSN 630 (pichani) kutoka kampuni ya Wallis Trading Inc. ya Liberia, umezua maswali mengi ndani na nje ya shirika hilo. Ndege hiyo kubwa ina uwezo wa kuchukua abiria zaidi ya 150.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa Raia Mwema, Shirika la ATCL, mnamo Oktoba 5, 2007, liliingia mkataba wa dola milioni 30 wa kukodisha ndege hiyo ya Airbus 320 ambayo wakati mkataba huo unaingiwa ilikuwa nchini El Salvador ikizeeka na kuota kutu.

Habari zinasema ya kwamba kabla ya ATCL kukubali kuikodisha, ndege hiyo ilikuwa inatumiwa na Shirika la Ndege la Jamaica ambalo baada ya kuitumia waliiacha katika hali hiyo mbovu iliyohitaji matengenezo makubwa.

Ingawa ndege hiyo imekodiwa na Tanzania kutoka kampuni ya Liberia, mkataba wake unaongozwa na Sheria za Uingereza. Mdhamini wa ununuzi wa ndege hiyo ni Serikali ya Tanzania ambayo kwa sasa inaongozwa na Chama cha Mapinduzi.

Uchunguzi unaonesha kuwa ndege hiyo mbovu ilikuwa El Salvador ikisubiri kuuzwa au kukodishwa kwa mdau mwenye kuja na bei nzuri. Mwanzoni wakati wa kutafuta ndege ya kukodi, memo moja ya viongozi wa juu wa ATCL ilisema kuwa shirika hilo linahitaji ndege ambayo itakapoletwa nchini “lazima watu wageuze vichwa vyao” kuiangalia inavyoruka.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari ndani ya shirika hilo, ambavyo kwa sababu ya wazi vimekataa kutajwa, ndege hiyo ilitakiwa iingizwe nchini Desemba 18 mwaka jana na kuanza safari zake tarehe Desemba 28. Ndege hiyo - A320-214 MSN 630 ndiyo inatarajiwa kufanya safari zake kati ya Dar-es-Salaam na Johannesburg, Afrika ya Kusini.

Habari zinasema, hata hivyo, kwamba kutokana na lile sakata la mahujaji na zaidi kutokana na matengenezo makubwa ya kuficha uchakavu wake, ndege hiyo imecheleweshwa kuingizwa nchini na sasa inatarajiwa kuingia nchini wakati wowote kuanzia sasa na kuanza safari zake katikati ya mwezi ujao.

Ndege hiyo imehitaji kufanyiwa matengenezo makubwa ambayo yamefanyika kwenye hanga ya kampuni ya Aeroman huko huko El Salvador.

Mara baada ya ATCL kukubali kuingia mkataba huo, ukaguzi ulifanyika ili kuangalia hali ya ndege yenyewe ilivyo. Uchunguzi huo ulifanywa kwa kuangalia nje na kutembea ndani ya ndege hiyo.

Taarifa ya ukaguzi huo siyo tu ilishtua vigogo wa ATCL bali pia ilionesha ni kwa kiasi gani ndege hiyo ilikuwa inahitaji matengenezo makubwa kinyume na mkataba na Wellis Trading Limited ulivyosema, lakini hawakuwa na cha kufanya kwani mkataba ulikuwa umeshaingiwa kati ya ATCL na kampuni hiyo yenye makazi yake huko Monrovia, Liberia.

Taarifa zinasema uchunguzi ulionesha kuwa ndege hiyo ilikuwa na matatizo mengi ambayo yanahitaji matengenezo makubwa. Kwa kuangalia taarifa hiyo kuna mambo hamsini (50) ambayo yanahitaji uangalizi wa karibu na matengenezo ya haraka kabla ya ndege hiyo kuweza kuruhusiwa kuruka.

Baadhi ya matatizo hayo ni pamoja na uchakavu wa vitu mbalimbali ambavyo imebidi ATCL iingie gharama ya kuvibadilisha kwani mkataba wao na Wellis Trading Inc. unasema wazi kuwa ndege inakodishwa kama “ilivyo” ukiondoa yale mambo ambayo yanasimamiwa na mtengenezaji wa ndege hiyo; yaani Airbus au mambo menginee yanayotajwa wazi.

Baadhi ya vitu ambavyo vilikuwa na uchakavu mkubwa ni pamoja na vyoo, milango, sehemu ya kuwekea mizigo, mazuria na chumba cha marubani. Hata hivyo, sehemu kubwa ambayo ilihitaji matengenezo makubwa ni uchakavu usiokifani wa viti vya abiria ambavyo licha ya kuchakaa karibu vyote vilikuwa vimenyofoka nyofoka na vilikuwa vimelegea na kutoa sauti kila mtu anapokalia.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya ukaguzi, viti vya marubani navyo ni vivyo hivyo huku chumba chenyewe cha marubani kikiwa ni kichafu ambacho mchunguzi mmoja aliyeangalia kwa karibu alisema “viti vyake vinatoa vumbi”.

Tatizo la viti kwa kiasi kikubwa limechangia ucheleweshaji wa ndege hiyo hasa kutokana na ukweli kuwa viti hivyo ni maalum na ilihitajika kuweka viti vipya kabisa kwenye ndege hiyo, gharama ambayo mwanzoni ATCL haikuwa tayari kuingia wakidai Wallis “haikuwaambia” kuhusu kiasi cha uchakavu huo.

Mmoja waliohusika na ukodishaji wa ndege hiyo alisema kuwa “Wallis hawakuweka kila kitu wazi kuhusu hali ya ndege”. Hata hivyo, haijajulikana kama viti vyote vimebadilishwa na kuwekwa vipya au ndio vimepakwa rangi tu na kufunikwa na vitambaa vipya tu.

Pamoja na hali hiyo chakavu, ATCL imeshaanza kulipia ndege hiyo na hadi hivi sasa tayari imeshalipia karibu dola milioni moja kwa Wallis na kwa kampuni ya Aeroman (mafundi) na kampuni ya Storm Aviation (wasafirishaji) ambapo marubani na wahandisi wanaoongozana na ndege hiyo pia watalipwa na ATCL.

Mapema mwezi huu, Ofisi ya Fedha ya ATCL iliidhinisha malipo hayo ya mwanzo, lakini baadaye ikabidi yasitishwe kwa sababu ya matatizo ya mahujaji. Hadi wiki iliyopita, kampuni ya ATCL ilikuwa imechelewa kufanya malipo mengine ya dola 370,000 kwa mwezi na hivyo kuadhibiwa faini ya dola 60,000 kwa mwezi.

Uamuzii wa kukodi ndege ya Airbus badala ya Boeing ulikuja baada ya kukataa ofa ya kampuni ya Boeing ambayo ilimtuma mwakilishi wake, Bw. Robert Faye, Septemba 29, 2007 kuja nchini kufanya majadiliano na ATCL.

Bw. Faye alikuja na mapendekezo ya kulisaidia shirika hilo katika kukodisha ndege kwa masharti kwamba ATCL pia iangalie uwezekano wa kununua ndege mpya kutoka kwao.



WAZIRI wa Miundo mbinu, Andrew Cheng

Afisa mmoja wa ATCL aliyeulizwa kwa nini waliamua kununua ndege hiyo ya Airbus badala ya Boeing, alisema kuwa ndege aina ya Airbus 320 ina matumizi madogo sana ya mafuta ukilinganisha na mshindani wake Boeing 737-200.

“Tunapoelekea kwenye bei ya mafuta kufika na kupita dola 100 kwa pipa, kwa kampuni kama ya kwetu ni lazima tutafute njia mbadala ya kutusaidia kuokoa mafuta na hivyo kupunguza gharama, na hivyo kuliokolea Taifa fedha nyingi”, alisema ofisa huyo aliyekataa kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa shirika hilo lakini, mwenye kulielewa kwa undani suala hilo.

Ukiondoa matatizo hayo ya kiufundi, hadi wiki iliyopita Serikali ya Tanzania, ambayo ndiyo mdhamini wa ununuzi wa ndege hiyo, ilikuwa haijatoa “guarantee” kwa shirika hilo la Wallis kwa mujibu wa kipengele cha mkataba huo.

Kwa mujibu wa mkataba huo ambao mwandishi wa Raia Mwema aliuona, guarantee ya serikali ilihitajika ipatikane ndani ya “siku tatu na si zaidi ya Oktoba 10, 2007”. Ni kukosekana kwa guarantee hiyo ndiko kumesababisha shirika hilo kudaiwa faini ya dola 60,000 kwa mwezi.

Hadi hivi sasa haijajulikana ni kwa nini serikali imeshindwa kutoa guarantee hiyo licha ya kuwaahidi mara kadhaa watu wa ATCL kuwa itafanya hivyo.

Hali hiyo inaonekana kuuchelewesha mpango mwingine wa kampuni hiyo wa kununua ndege mpya ya Airbus toka kwa watengenezaji; mpango ambao unatarajiwa kushuhudiwa na Rais Jakaya Kikwete kwenye ziara yake inayotarajiwa kufanywa nchini Ujerumani katikati ya mwezi ujao.

Wiki iliyopita kampuni ya utengenezaji wa ndege ya Airbus iliwaandikia ATCL barua yenye kumbukumbu namba CSD/ATC/2 ambayo ndani yake imewataka ATCL kukamilisha malipo ya awali ya ununuzi wa ndege hiyo mpya vinginevyo “maandalizi ya ziara ya Rais hayatawezekana bila kukamilika malipo hayo”.

Barua hiyo iliendelea kusema kuwa “kuchelewesha huku siyo tu kunachelewesha jitihada za kuifufua ATCL bali pia inaongeza gharama kubwa kwa kampuni yenu”.

Chanzo chetu cha habari karibu na kampuni ya Airbus, mjini Hamburg, Ujerumani, kimesema kuwa Airbus inafuatilia mkataba kati ya ATCL na Wallis kwani wao kama watengenezaji wa ndege za aina hiyo wana majukumu kadhaa ambayo wanatakiwa kuyatimiza kwenye mkataba huo, na hivyo ucheleweshaji wa kutoa guarantee na hatimaye kuiingiza ndege hiyo katika utendaji, unawahusu “sana”.

Ndege hiyo ambayo inatarajiwa kuingizwa nchini na marubani na mafundi wa Storm Aviation haijajulikana wazi kama taratibu zote za manunuzi ya serikali zilifuatwa na maswali kadhaa bado yanahitaji kujibiwa.

Baadhi ya maswali hayo ni pamoja na ni jinsi gani Waziri wa Miundo Mbinu, Andrew Chenge na watendaji wake walishughulikia mkataba huo wa ukodishaji dege hilo bovu ikizingatiwa kuwa Wizara hiyo tayari imeshawahi kujikuta na kashfa nyingine kadhaa huko nyuma kuhusiana na manunuzi ya ndege.

Si Chenge wala Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, David Mattaka waliopatikana jana kuzungumzia suala hilo.


Kutoka gazeti la Raia Mwema wiki hii