Monday, March 31, 2008









Usione, usisikilize wala usiamini lolote lile.

Zaidi kuhusu siku ya wajinga, bofya hapa

Waswahili walisema

"Uwongo wa mwenye nyumba,

si ukweli wa mpita njia.



JK aelemewa Butiama



Rais Kikwete akiteta na Nimrod Mkono kijijini Butiama



na Mwandishi Wetu, Musoma

MZIGO mzito wa kimaamuzi unaonekana dhahiri kumlemea Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, ambaye amelazimika kuviongoza vikao viwili vizito vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, vinavyofanyika Butiama bila ya kuwapo kwa nguzo zake kuu kisiasa.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili unaonyesha kwamba, kukosekana kwa wajumbe kadhaa muhimu wa kudumu wa vikao vya CC na NEC ya CCM, kunaweza kwa kiwango kikubwa kutia doa kama si kuathiri baadhi ya maamuzi mazito ambayo yamekuwa yakitarajiwa kufikiwa.

Miongoni mwa watu hao muhimu ambao kukosekana kwao kumeshaanza kuibua hali ya wasiwasi na kuonekana kupwaya kwa uzito wa vikao hivyo vya Butiama vinavyofanyika kwa mara ya kwanza eneo alikozaliwa na kuzikwa, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, ni marais na wenyeviti wastaafu wawili wa chama hicho, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.

Wadadisi wa mambo kadhaa wa ndani ya chama hicho waliozungumza na Tanzania Daima kutoka Butiama, wanakielezea kitendo cha kukosekana kwa Mkapa na Mwinyi kuwa jambo ambalo litasababisha kulemewa kwa Kikwete na pengine kukosekana kwa nguvu ya kufikiwa kwa maamuzi mazito yanayogusa mustakabali wa wakati huu wa chama hicho.

Aidha, wakati kukosekana kwa viongozi hao wawili ambao ni wajumbe wa maisha wa CC na NEC ya chama hicho kunachagizwa na kupewa uzito mkubwa, na kutokuwapo kwa Rais mstaafu wa Zanzibar, ‘Komandoo’ Dk. Salmin Amour Juma.

Kama hiyo haitoshi, vikao hivyo vinafanyika Butiama wakati pia akikosekana mwanadiplomasia adhimu nchini, Dk. Salim Ahmed Salim, ambaye naye ni mjumbe wa CC na NEC kwa pendekezo la Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho.

Mbali ya Dk. Salmin, kikao cha NEC kilichoanza jana jioni majira ya saa 11 kutokana na kuchelewa kwa kikao cha CC, pia kinafanyika pasipo kuwapo kwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.

Kutokuwapo kwa Dk. Salmin na Dk. Salim katika vikao hivyo viwili, kunalifanya suala la kupatikana kwa ufumbuzi wa kudumu kuhusu hali ya kisiasa ya Zanzibar, na hususan kufikiwa kwa muafaka wa kisiasa visiwani humo kati ya vyama vya CCM na CUF kuwa ni wenye mashaka makubwa.

Baadhi ya wajumbe wa NEC waliozungumza na Tanzania Daima kwa sharti la kutotajwa majina yao magazetini, wanakielezea kitendo cha kukosekana kwa viongozi hao wawili wanaotoka Zanzibar kuwa jambo ambalo linaweza kuyafanya maamuzi kuhusu muafaka kuwa magumu.

Jambo gumu kwa chama hicho na hususan kwa Rais Kikwete kuhusu kukosekana kwa viongozi hao wa juu muhimu wanne, ni wasiwasi ambao umeshaanza kuzingira vikao hivyo, unaoonyesha kwamba huenda wazee hao wamekosekana si kwa sababu ya kuwa safari kama inavyodaiwa na uongozi wa juu wa CCM, bali kutoridhishwa kwao na mwenendo wa mambo serikalini na ndani ya chama.

Wana CCM waliozungumza na Tanzania Daima kuhusu hili, wanaielezea hatua ya watu hao kukosekana kuwa ni dalili ya mwanzo ya CCM ya Kikwete kuanza kukosa ushawishi ndani ya mioyo ya viongozi wakuu wastaafu, ambao sasa wanakiona chama kikipoteza misingi yake ya kihistoria ya kushika hatamu.

“Kumekuwa na wasiwasi kwamba, Kikwete amekuwa akifikia maamuzi mazito pasipo kwanza kukitaarifu chama na badala yake amekuwa akifanya hivyo kwa kutumia Bunge na ushauri wa kundi dogo la watu. Hali hii inaonekana kutowafurahisha wazee,” alisema mfuatiliaji mmoja wa karibu wa siasa za ndani ya CCM.

Lakini pengine pigo kubwa kwa Rais Kikwete lilizidi kuonekana dhahiri jana baada ya Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein ambaye pia ni Mzanzibari, kulazimika kuondoka katika vikao hivyo kutokana na kufariki dunia kwa mama yake mzazi.

Kuondoka kwa Dk. Shein, kiongozi wa pili kwa mamlaka katika serikali na mtu aliyetokea kuwa mshauri wa karibu kikatiba na kikazi wa Rais Kikwete, kunayafanya maamuzi kuhusu siasa za Zanzibar kuzidi kuwa magumu.

Kutokana na hali hiyo basi, Rais Kikwete atalazimika kutumia ushauri wa Rais wa Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wake, Amani Abeid Karume, Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Kiongozi mstaafu Gharib Bilal na Wazanzibari wengine wasio na ushawishi mkubwa katika kueleza kwa kina athari za kisiasa, kijamii na kiuchumi za kuhitimishwa kwa muafaka ambao unatarajia kutoa baraka za kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa visiwani.

Ni jambo la bahati mbaya kwamba, watu hao muhimu, Mwinyi, Mkapa, Dk. Salmin, Dk. Salim na Dk. Shein wanakosekana katika vikao wakati moja ya ajenda inayosubiriwa kwa hamu na Wazanzibari ni hiyo ya kufikiwa kwa suluhu ya kudumu ya kisiasa huko visiwani.

Mbali ya hilo la mwafaka, kukosekana kwa Mkapa kwa mfano kunaufanya mjadala kuhusu masuala kama lile la Kashfa ya EPA na mengine yanayomgusa yeye binafsi kushindwa kujadiliwa kwa kina.

Hali hiyo inakuja baada ya watu kuwa na imani kwamba, vikao hivyo vya Butiama vinavyofanyika hatua chache kutoka alipozikwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, vilikuwa vikitarajia kupata majibu ambayo yangekisadia chama hicho kupata majibu kamili kuhusu nini kilitokea katika EPA zama za Mkapa akiwa Rais na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM.

Kama ilivyo kwa Mkapa, kukosekana kwa Mwinyi, kiongozi ambaye kimsingi ndiye anayeweza kubeba mzigo wa kuwa mrithi wa kiuongozi wa taifa baada ya kuondoka kwa Mwalimu Nyerere, kunaufanya mjadala wa masuala kama lile la Richmond lililosababisha kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na kuvunjwa kwa Baraza la Mawaziri kupwaya na kukosa mashiko.

Wafuatiliaji wa mambo wanakuona kukosekana kwa Mwinyi kuwa ni pengo ambalo litamwia vigumu Kikwete kuliziba wakati huu chama hicho kikiwa katika mazingira magumu kuvunja kuimarika na kuibuka kwa makundi mengi zaidi ndani ya chama hicho, yaliyoibuka baada ya masuala ya EPA na Richmond kuibuka.

“Kwa namna yoyote ile sisi kama chama tulihitaji sana hekima za wazee wetu kama Mwinyi na Mkapa katika kuhitimisha haya masuala ya EPA na Richmond, ambayo hayajapata kujadiliwa kwa kina,” alisema mwana CCM mmoja aliyezungumza na Tanzania Daima Jumapili jana.

Baadhi ya minong’ono inayosikika kutoka kwa wajumbe wa mkutano huo inaeleza kwamba, Mkapa hakuhudhuria vikao hivyo kwa sababu ya kuchukizwa kwake na hatua ya kuhusishwa moja kwa moja na ukiukaji wa maadili wakati akiwa madarakani.

Inaelezwa kuwa, ingawa Mkapa alimuunga mkono Kikwete katika kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, kutajwa kwa jina lake sana katika masuala mbalimbali, ni jambo analoliona likiwa na baraka kamili za viongozi wa juu serikalini wenye malengo yao binafsi.

Baadhi ya wadadisi wanahofu kwamba, upo uwezekano mkubwa kuwa baadhi ya viongozi wakuu wastaafu wameanza kuiona serikali ya sasa kuwa iliyopoteza uwezo na umadhubuti wa kuhimili mikiki mikiki na hivyo wakaamua kukaa kando.

Kutoka Tanzania Daima

Uopoaji maiti Mererani wasuasua


*Ukosefu wa vifaa ni tatizo sugu
*JK atuma salamu za rambirambi

Na Said Njuki, Mererani

KAZI ya uopoaji maiti ndani ya migodi ya tanzanite, Mererani wilayani hapa, imezidi kuwa ngumu na hata kukwama kutokana na ukosefu wa vifaa vya kuopolea zikiwamo pampu za kuvutia maji kutoka mashimoni.

Hali hiyo imetokana na kwamba takriban miili 67 bado imo ndani ya migodi hiyo, huku miili sita tu ndiyo ikiwa imeopolewa juzi asubuhi huku viongozi wa Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Bw. Henry Shekifu, wakiunda kamati kadhaa.

Baadhi ya kamati hizo ni ya Operesheni Okoa itakayoongozwa na Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Venance Tossi, ya Maafa ambayo Mwenyekiti wake ni Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Bw. Khalid Mandia na Katibu wake ni Ofisa Madini wa Kanda, Bw. John Nayopa.

Kamati nyingine ni ya wataalamu ambayo wengi wa wajumbe wake ni wachimbaji madini.

Lakini wakati kamati hizo zikiendelea kujipanga, baadhi ya wachimbaji walionesha wasiwasi wao juu ya uwezekano wa kuopoa miili hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara, mchimnbaji Sokota Mbuya, alisema mbali na vifaa kupatikana, Serikali inatakiwa kutoa msaada moja kwa moja wa chakula na posho kwa wachimbaji wazoefu, kwani eneo hilo limekumbwa na baa la njaa na hivyo kuingia mgodini na njaa ni vigumu.

Alisema maiti hawawezi kuopolewa na wataalamu wa Jiolojia peke yao, kwani hata katika maafa ya mwaka 1998 wataalamu hao na vikosi vya majeshi, walisaidiwa kupanda juu baada ya kuingia na kushindwa kutoka.

Mama Stella Shayo, ambaye pia ni mchimbaji, aliwahoji kwa kejeli viongozi wa Serikali akiwamo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Bw. Philip Marmo; Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Lawrence Masha na Waziri wa Nishati na Madini Bw. William Ngeleja, kwamba Serikali Kuu ilifuata nini pale badala ya kuendelea na vikao huku miili ikiendelea kubaki mashimoni.

Akizungumza katika mkutano huo, Bw. Shekifu pamoja na kuwataka wachimbaji kushirikiana katika kadhia hiyo, pia alisimamisha kwa muda usiojulikana shughuli zote za uchimbaji katika migodi hiyo ya vitalu A, B, C na D.

Akizungumzia hatua hiyo, Mkaguzi Mkuu wa Madini nchini, Bw. Edwin Ngonyani, alisema Serikali hufanya kazi kwa mujibu wa sheria ya usalama migodini, inayoipa mamlaka ya kufunga migodi na moja ya sababu ni kuhakikisha kila mmoja anashiriki katika shughuli hiyo.

Waziri Marmo kwa upande wake, alisema Serikali inafanya kazi na kamati mbalimbali za maafa za ngazi zote na atapokea mapendekezo ya kamati husika ili naye atoe mchango wake.

Lakini wakati yote hayo yakiendelea, tayari wataalamu kutoka mgodi wa dhahabu wa Barrick waliripotiwa kutua Mererani, ili kuongeza nguvu za uopoaji huku wajumbe wa moja ya kamati wakiwa migodini tangu asubuhi kutathmini ugumu wa kazi hiyo.

Kamati hiyo inaundwa na wachimbaji, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wana usalama, Polisi.

Jumla ya wachimbaji 166 ndio waliodaiwa kuingia katika migodi hiyo huku 93 wakitoka salama na 67 wakiaminika kuwa bado hawajaopolewa. Ajali hiyo ilitokea juzi kwa mashimo kujaa maji kutokana na mvua kubwa iliyonyesha.

Wakati huo huo, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za pole Mkuu wa Mkoa na wananchi wa Mkoa wa Manyara, kutokana na maafa hayo.

Taarifa ya Ikulu kutoka Butiama, Musoma jana, ilisema Rais alipokea kwa masikitiko, huzuni na mshtuko mkubwa taarifa za janga hilo kubwa.

Alihuzunishwa kwa upotevu wa maisha ya watu ambao mpaka sasa imethibitika kuwa wamepoteza maisha.

Rais pia aliwaombea wachimbaji ambao taarifa zao hazijathibitika waweze kupatikana haraka wakiwa hai na salama na pia aliwaombea wote walioumia katika ajali hiyo wapone haraka.

Alitoa pole kwa familia ambazo zimeathirika na janga hilo na kuzihakikishia kuwa yuko pamoja nazo katika wakati huu wa majonzi na huzuni.

Kutoka Tanga Bakhya Said, anaripoti kuwa kivuko cha Mto Pangani, mv Pangani kilizama juzi saa moja asubuhi wakati kikipakia gari lililokuwa limebeba marobota ya mkonge yenye uzito wa tani nane na kusababisha mlango wa kivuko hicho kukatika.

Akizungumzia juzi mchana baada ya ajali hiyo katika eneo la tukio, katika gati la ng'ambo ya Bweni, Mkuu wa kivuko hicho, Bw. Marko Manyala, alidai kuwa chanzo cha ajali ni uchakavu wa milango ya kivuko hicho.

Bw. Manyala alisema katika ajali hiyo hakuna abiria wala mfanyakazi aliyepata madhara kwa kuwa kilizama katika gati kabla ya abiria kuingia.

"Tulianza kazi saa 12 asubuhi na tulivusha basi na abiria, lakini dereva wa gari lililobeba marobota aina ya Mitsubishi T 416 AMG lililokuwa na uzito wa tani nane kabla ya abiria kupanda, tulimruhusu aingize gari lake na baada ya kuingiza tairi za mbele alifunga breki ghafla na uzito wote ukawa nyuma ya mlango, ukakatika likabaki linaning’inia na sehemu kubwa ya kivuko ikawa imeshikilia majini," alisema Bw. Manyala.

Alisema maji yalivyozidi kujaa kivuko hicho kilizidi kufunikwa na maji lakini walivuta gari hilo ambalo nusu lilikuwa nchi kavu kwenye gati na nusu kwenye kivuko.

Wakati hali hiyo ikitokea Naibu Waziri wa tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bi Selina Komba alikuwa katika ziara ya siku tatu kutembelea miradi mbalimbali ya wananchi na kusikiliza maoni na kero zao na alipangiwa kuvuka ng’ambo ya pili ya Mto Pangani, ambako ndipo ilipo sehemu kubwa ya Wilaya.

Naibu waziri huyo alilazimika kuvuka kwa kutumia boti na pia alijionea hali halisi ya kivuko hicho na amekiri kuwa malalamiko ya wananchi na viongozi wa wilaya ya Pangani yana msingi sana.

Wakati haya yakitokea, msafara huo wa Naibu Waziri pia uliongozana na Mbunge wa Pangani, Bw. Rished Abdallah.

Jana mafundi wa kivuko hicho walikuwa wamefunga mapipa na kuweka pampu za kutolea maji, ili kukifanya kiweze kuelea ili waanze ukarabati wa bodi na mashine ambazo zimeingia maji ya chumvi.

Sunday, March 30, 2008

Duniani kuna mambo..

Thomas Beatie, a married

man who used to be a woman,

is pregnant with a baby girl


A married man who used to be a woman says that he is pregnant and will give birth to a baby girl in July.

“How does it feel to be a pregnant man? Incredible,” wrote Thomas Beatie, 34, from the Pacific North West of the United States, in the latest issue of the gay magazine The Advocate.

“Despite the fact that my belly is growing with a new life inside me, I am stable and confident being the man that I am.”

Mr Beatie was born female, named Tracy Lagondino, but had gender reassignment surgery and is now legally male and married to a woman.

He decided to carry a baby for his wife, Nancy, because she had a hysterectomy years ago. He was able to get pregnant because he kept his female organs when he switched genders.

“Sterilisation is not a requirement for sex reassignment, so I decided to have chest reconstruction and testosterone therapy but kept my reproductive rights,” he writes. “Wanting to have a biological child is neither a male nor female desire but a human desire.” The couple, who have been together for ten years, run a custom screenprinting business in Bend, Oregon, where neighbours do not know that Mr Beatie was once a woman.

“Our desire to work hard, buy our first home and start a family was nothing out of the ordinary. That is, until we decided that I would carry our child,” he wrote.

Before becoming pregnant, Mr Beatie stopped the testosterone injections he was receiving as part of his gender reassignment. “It had been roughly eight years since I had my last menstrual cycle so this wasn’t a decision that I took lightly. My body regulated itself after about four months and I didn’t have to take any exogenous oestrogen, progesterone or fertility drugs to aid my pregnancy,” he wrote.

The couple bought donor vials from a cryogenic sperm bank and, facing resistance and prejudice from doctors, resorted to home insemination. “Doctors have discriminated against us, turning us away due to their religious beliefs. Healthcare professionals have refused to call me by a male pronoun or recognise Nancy as my wife. Receptionists have laughed at us. Friends and family have been unsupportive; most of Nancy’s family doesn’t even know I’m transgender,” he said.

Mr Beatie’s first successful insemination ended in a life-threatening ectopic pregnancy with triplets that required surgery, resulting in the loss of all his embryos and his right Fallopian tube. “When my brother found out about my loss, he said, ‘It’s a good thing that happened. Who knows what kind of monster it would have been?’,” he wrote.

The second pregnancy resulted in a baby girl who is due to be born on July 3. “I will be my daughter’s father, and Nancy will be her mother. We will be a family,” he wrote.

Mr Beatie would not be the first transgender man to give birth, according to Lisa Masterson, an obstetrician at Cedars-Sinai Medical Centre in Los Angeles.

“A transgender man can be pregnant because he has the same organs as a woman,” Dr Masterson said on the ABC Good Morning America show.

Dr Masterson said, however, that transgendered men face special health risks resulting from their sex change. “It’s really important that he doesn’t take any testosterone early on in the pregnancy and later on,” she said. “That can cause male-type characteristics in the female baby.”

Some of the Beaties’ neighbours in Bend voiced scepticism about the pregnancy claim. One resident, Josh Love, told ABC: “I couldn’t say that he looks pregnant. I can stick my stomach out and almost make it look like that. I think it’s kind of bizarre. I don’t know if I believe it or not.”

The Advocate said it had confirmed the story with Mr Beatie’s doctor.

Source: Times Online UK


Tafakari ya Jumapili:

Serikali mbona

kigugumizi kuhamia Dodoma?


Na Elias Mhegera

UAMUZI wa kuhamishia makao makuu ya Chama na Serikali mjini Dodoma ulifanyika katika awamu ya kwanza ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Hata hivyo, hivi karibuni Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda ameonyesha ugumu wa azma hiyo kutekelezwa.

Inabidi tukiri sasa, kwa mwenendo wa mambo ulivyo, inaonekana katika mambo ambayo yanaweza kuingizwa katika kumbukumbu kuwa ni maamuzi yanayoonekana kuitatiza sana Serikali basi ni uamuzi huo.

Kwa miaka kadhaa Serikali imekuwa ikitoa maelezo kwamba uamuzi wa kuhamia Dodoma bado upo pale pale, lakini kivitendo inaonekana hilo limeshindikana na badala yake kuna kila ishara kwamba serikali imedhamiria kubakia jijini Dar es Salaam.

Je, ni kwa nini basi Serikali isitangaze tu kwamba uamuzi wa kuhamia Dodoma umebatilishwa? Maana yangu ni kwamba kuendelea kuahidi jambo ambalo una uhakika kwamba huna uwezo wa kulitekeleza kunaweza kukushushia heshima yako na pia kuwafanya watu wasiamini ahadi zako nyingine.

Nitatoa mifano michache kuhusiana na maamuzi yasiyotekelezwa na ambayo yanawanyima haki wananchi katika ujumla wao. Mojawapo ya maamuzi ambayo ni lile la uamuzi uliotolewa mwezi Mei, 2006 na Mahakama Kuu uliopitishwa na jopo la majaji watatu Amir Manento, Salum Massati, na Thomas Mihayo, ukiruhusu kuwapo kwa wagombea binafsi katika chaguzi zetu.

Upo pia mlolongo wa matukio ya maamuzi yenye utata na yasiyozingatia maslahi ya Taifa. Kwa mfano uteuzi wa watu wenye kashfa sehemu moja na kuwapeleka sehemu nyingine, hilo limewahi kujitokeza ambapo mmoja wa walioteuliwa kuwa balozi wetu nchini Marekani aliwahi kuhusika katika uagizaji wa kivuko kibovu ambacho hatimaye kilisababisha kuangamia wa maisha ya Watanzania.

Upo ule mpango wa usafiri kwa wanafunzi wa Dar es Salaam, zoezi hilo liliratibiwa na Jumuia ya Umoja wa Vijana wa CCM. Matokeo yake mradi huo uliwanufaisha wajanja wachache ambao waliufilisi mradi huo na mpaka leo watu hao bado wanapeta na nyadhifa nzito serikalini.

Miaka kadhaa nyuma aliyepata kuwa waziri katika Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, Bw. Jackson Makweta aliamua kuisafisha wizara yake kutokana na tuhuma za uuzwaji wa skolashipu za nje hata hivyo uamuzi huo ulimtokea puani kwani yeye ndiye aliyesafishwa na kuanzia wakati ule hajapata kuingia tena katika Baraza la Mawaziri.

Lakini Je, tumefanya tathmini ya kina kuhusu baadhi ya wale 'aliowasafisha’ katika wizara yake si baadhi yao ndiyo hao hao ambao leo wanatuhuma za kuhujumu mali ya umma? Kumbe basi jitihada zake zilistahili kuungwa mkono badala ya kupingwa.

Majowapo ya mambo ambayo Serikali imekuwa na kigugumizi cha kuyatekeleza ni pamoja na mapendekezo ya kuwashirikisha wapinzani katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Mapendekezo ya awali yalipitishwa katika mazungumuzo ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuia ya Madola Chifu Emeka Anyouku.

Serikali pia haikuchukua hatua zinazostahili kwa wale wote ambao walituhumiwa kuhusika katika vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa Watanzania ndani ya nchi yao wenyewe katika kuwahamisha wakazi wa Bulyanhulu ili kupisha ujenzi wa mgodi wa dhahabu mwaka 1996. jambo hilo liliiabisha nchi miongoni mwa jumuiya ya kimataifa kwa mujibu wa jarida la 'Africa Confidential,' toleo namba 18, Septemba 2001.

Katika tafakuri yangu leo, nimebaini kuwa ucheleweshaji wa uamuzi wa kuhamia Dodoma umesababisha baadhi ya watu kujinufaisha kwa kuiba mamilioni ya pesa ambazo zilitolewa kwa ajili ya Mamlaka ya Uendelezaji wa Makao Makuu Dodoma (CDA) na bado Serikali itaendelea kuingia hasara kubwa kwa kupekeka miradi, ofisi na programu mbalimbali za kiserikali, lakini viongozi wote wako Dar es Salaam.

Wahenga walionya kuwa la kuvunda halina ubani, hivi vigugumizi vya maamuzi nyeti vitaendelea kuligharimu taifa hasara nyingi na kubwa iwapo hatutafikia mahali na kusema sasa basi kila jambo na lihitimishwe au iwekwe bayana kuwa limeshindikana na wahusika waombe radhi. Najua mko Butiama, jifunzeni, Mwalimu alipata kukiri makosa yake kadhaa, alikuwa muungwana!

*Mwandishi wa makala haya anapatikana kupitia baruapepe: mhegeraelias@yahoo.com. Simu: 0754 826272

Kipanya na wanaorudisha hela za ufisadi

Strike threat after wage

talks break down



Negotiations between the Confederation of Trade Unions (LO) and the Confederation of Norwegian Enterprise (NHO), aided by the State Arbitrator, broke off on Friday, with the possibility that 40,000 union members may go on strike next week.


he two sides were not able to reach agreement on wages and how to maintain special pension benefits (AFP).

If no settlement is reached by Wednesday, around 40,000 employees will walk out on strike as a first step.

First out would be workers in the building industry and the breweries, auto mechanics, shipyard workers, cleaning crews, newspaper carriers and health care personnel.

Source: Norwegian Broadcasting Corporation/Norway Post.

Saturday, March 29, 2008






Leo usiku wa manane saa 8

kuamkia Jumapili 30 Machi 2008

majira ya Kiangazi yanaanza

Ulaya ya Magharibi

(Central European Time = CET).

Hivyo basi sogezeni saa moja mbele.

Saa 8 za usiku sogeza saa na

kuwa saa 9 za usiku kuamkia

Jumapili 30 Machi 2008.

Kuanzia Jumapili 30 Machi 2008

kutakuwa na tofauti ya

saa moja na saa za Afrika Mashariki

(East African Time = EAT)



Udaku wa Jumamosi


Na Mariam Mndeme.

Kauli ya mwanamuziki anayevuma hivi sasa nchini, Nakaaya Abraham Sumari, kuhusu sura na umbo lake vinawadatisha wanawake wenzake, imezua minong’ono kwamba huenda msanii huyo ni msagaji...

Msikilize Nakaaya na wimbo wake "MATATIZO"






Nakaaya kupitia kipindi cha Friday Night Live cha Luninga ya EATV, Ijumaa iliyopita alisema kuwa uzuri wake unawadatisha watu wa jinsia tofauti, hivyo hashangai wanawake wenzake kumtongoza.

Kabla ya kauli hiyo ya Nakaaya, mtazamaji mmoja mwanamke, alituma ujumbe wa simu ya mkononi (sms) na kusomwa na mtangazaji wa kipindi hicho, Denis Busulwa ‘Sebo’, akieleza jinsi anavyovutiwa na msanii huyo.


Msikilize Nakaaya na wimbo wake "Mr. Politician"





Kwa mujibu wa ujumbe huo wa maneno na jinsi ulivyosomwa na Sebo ni kwamba mtazamaji huyo wa kike, alikuwa akivutiwa na Nakaaya kimapenzi.

Mara baada ya kuiona sms hiyo, Sebo alimuuliza Nakaaya kuwa iweje awavutie mpaka wanawake wenzake?

Hata hivyo, msanii huyo alijibu kwamba yeye anawavutia watu wote, kauli ambayo ilitafsiriwa na baadhi ya watazamaji kuwa pengine anapenda ‘hako kamchezo’ ndiyo maana hakuchukia kutongozwa na mwanamke mwenzake.

“Huyu dada naye yumo nini katika mambo hayo, maana jibu lake linaonesha anaona poa tu kutongozwa na wanawake wenzake!” Alisema mtazamaji mmoja, katika baa moja iliyopo Sinza, jijini Dar es Salaam, huku mwandishi wetu akimsikia.

Katika kipindi hicho, Nakaaya alialikwa akiwa na mwenzake Jacqueline Ntuyabaliwe ‘K-Lyn’ pamoja na wanamuziki nguli wa R&B duniani, Wamarekani KCI & Jojo.

Wasanii hao wote, walikuwa wakizungumzia ‘shoo’ ya KCI & Jojo, iliyoandaliwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo ambapo Nakaaya na K-Lyin waliisindikiza katika Ukumbi wa Hoteli ya Movenpick jikjini Dar es Salaam Jumamosi iliyopita.

Aidha, siku moja baada ya kipindi hicho, habari tulizozipata kutoka kwa rafiki wa Nakaaya zilisema kuwa msanii huyo amekuwa akipigiwa simu na wakati mwingine kutumiwa ujumbe na idadi kubwa ya wanawake wakimtongoza.

Rafiki huyo alisema: “Wanawake wengi wamekuwa wakijieleza eti wanavutiwa na Nakaaya kwa sura yake halisi (natural), umbo, mtindo wake wa kukata nywele fupi na sauti yake.”

Nakaaya ambaye ni dada wa Miss Tanzania na Miss World Africa mwaka 2005-06, Nancy Abraham Sumari kwa sasa ‘anafunika’ katika anga ya burudani kupitia kibao chake cha Mr. Politician kilichobeba jina la albamu yake yenye jumla ya nyimbo 10.

Nyimbo hizo zinazopatikana katika albamu hiyo inayogombewa vilivyo sokoni ni Nervous Conditions, Mr. Politician, Matatizo, New day, Malaika, Iyeyo, Love me, Nyimbo za Uhuru, A town girl na I’m Free


Ali Farah relieved over

discrimination ruling


Ali Farah, an African-Norwegian abandoned by ambulance personnel after he'd been beaten in an Oslo park last summer, says he's "relieved and happy" that a state commission has concluded he was a victim of discrimination.

Ambulance personnel refused to take an injured Ali Farah to hospital last summer.

PHOTO: CARLOLINE DREFVELIN

Related stories:

State health officials in charge of the ambulance service had earlier concluded no laws were broken when two ambulance attendants refused to take Ali Farah to hospital.

An inquiry by the Norwegian Board of Health Supervision (Statens helsetilsyn) claimed racism wasn't an issue when the attendants left Ali Farah injured and bleeding.

The state Equality and Anti-Discrimination Ombud, however, disagreed. It now says Ali Farah was a victim of discrimination and that the ambulance personnel violated Norway's anti-discrimination law.

Ali Farah, who was found to have suffered a severe head injury after being taken to hospital in a taxi, said the ombud's ruling has renewed his faith in the Norwegian system and state agencies. "I feel that this report strengthens my case," he said. "It's good to be believed."

The fate of the ambulance personnel, who initially were suspended from duty after the incident, remains unclear. Both kept their jobs but health officials said they now will reevaluate the case with the ombud's decision under advisement.

Aftenposten English Web Desk



Mambo yote Butiama...


Rais jakaya kikwete akiwapungia wananchi wa Butiama kabla ya kuingia kwenye ukumbi wa kumbukumbu ya Joseph Kazurira Nyerere ulioko Butiama kuongoza mkutano wa Kamati kuu ya CCM jana.Kushoto ni katibu mkuu wa CCM, Yusufu Makamba na wapili kushoto ni mkamau mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa.

Rais jakaya Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ukumbi wa kumbukumbu ya Joseph Kazurira Nyerere, Butiama jana kuongoza mkutano wa Kamati Kuu ya CCM. Wengine pichani kutoka kushoto ni Mama Maria Nyere, katibu Mkuu wa CCM , Yusufu Makamba, Makamu wa Rais, Dr. Ali Mohammed Shein, Makamu Mwenyekiti wa CCM Mstaafu, John Malecela na Waziri Kiongozi wa Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha.
-----------------
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana ameongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) katika kijiji cha Butiama, wilaya ya Musoma, Mkoa wa Mara.Kikao hicho kimeanza tu muda siyo mrefu baada ya Rais Kikwete kuwa amewasili Butiama tayari kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM .

Kikao cha NEC kinaanza kesho ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika katika kijiji ambako alizaliwa Baba wa Taifa na mwanzalishi wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Rais Kikwete aliwasili Butiama kwa barabara akitokea Mwanza ambako ndege yake ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza mapema asubuhi na akaamua kusafiri kwa gari kwenye Musoma.Mjini Mwanza, mamia ya wakazi wa mji huo na vitongoji vyake, walijitokeza kwa wingi, katika baadhi ya sehemu za jiji hilo mvua ikiwa inanyesha, kumshangilia Rais wakati msafara wake ukikatisha mitaa ya jiji hilo kuelekea Musoma.

kutoka: http://haki-hakingowi.blogspot.com/



Watoto wamtapeli

Mama Rwakatare


KATIKA hali isiyotarajiwa, watoto waliojulikana kwa jina moja moja la Yusufu na Ramadhani, wamelidanganya Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God linaloongozwa na Mchungaji Dk. Gertrude Rwakatare, baada ya kujifanya kuwa wamedondoka kutoka angani walikokuwa wakiwanga, kutokana na nguvu ya maombi ya waumini wa kanisa hilo.

Utapeli kuhusu watoto hao, ambao ulitangazwa kwa mara ya kwanza na Kituo cha Televisheni cha ITV, ulithibitishwa kwa gazeti hili na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Jamal Rwambow, juzi.

Kamanda Rwambow, alisema kabla ya kujifanya wameanguka katika kanisa hilo la Mchungaji Rwakatare, hivi karibuni, watoto hao walifanya jambo kama hilo Januari 6, mwaka huu katika eneo la Tangi Bovu jijini Dar es Salaam.

“Baada ya polisi wangu kupata taarifa za kuanguka kwa watoto hao, walifika eneo la tukio na kuwachukua hadi Kituo Kidogo cha Polisi Kawe na kuwahoji, halafu wakawapeleka Hospitali ya Mwananyamala kwa ajili ya uchunguzi wa afya zao.

“Madaktari walichunguza afya zao na kubaini kuwa hawana maradhi yoyote. Lakini jeshi letu lilipata taarifa zaidi kutoka kwa watu wanaowafahamu watoto hao wakisema kwamba, watoto hao ni matapeli,” alisema Kamanda Rwambow.

Aliongeza kuwa, mwanzoni mwa Februari, watoto hao tena walijifanya wameanguka huko Manzese, ambako polisi wa eneo jirani na walipodai kudondoka watoto hao, walifika na kuwachukua.

Kamanda Rwambow, aliongeza kuwa baadhi ya waumini na viongozi wa kanisa moja lililopo Manzese waliwachukua, kuwaombea na kuwapeleka kwenye kituo cha kulelea yatima Kurasini.

Alisema, waumini hao walibaini kwamba watoto hao ni matapeli, waliwaacha na kusisitiza kuwa hao si wachawi wala misukule walioanguka kwa nguvu za maombi kama inavyodaiwa, na kuyatahadharisha makanisa na jamii kuepukana nao pia kuwa makini na matukio ya namna hiyo.

Kabla ya uzushi huo wa aina yake, watoto hao baada ya kubainika na kuwekwa hadharani kwa mara ya kwanza na ITV, waliueleza uongozi wa Kanisa la Mikocheni kuwa walikuwa wakiishi kama misukule katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Wakizungumza kuhusu watoto hao Jumanne wiki hii katika ITV, walezi wao walieleza kuchoshwa na tabia ya utukutu wa Yusufu na Ramadhani wanaokadiriwa kuwa na kati ya miaka saba au 10.

Alipozungumzia suala hilo wakati wa mkutano na waandishi wa habari aliouitisha Machi 17, mwaka huu, Mchungaji Dk. Rwakatare, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), alisema watoto hao walidondoka wakati waumini wa kanisa hilo walipokuwa wakiomba na kumtukuza Mungu.

Mchungaji huyo, alikaririwa na vyombo vya habari akisema watoto hao walianguka kutoka juu katika eneo la kanisa hilo baada ya nguvu za giza kushindwa kutokana na maombi ya kawaida yaliyokuwa yakiendelea ndani ya kanisa lake.

Hata hivyo, siku kadhaa baada ya mkutano na waandishi wa habari, Mchungaji Dk. Rwakatare, alionekana tena kwenye luninga akiwa katika shughuli za kiroho na kuwahoji watoto hao waliodaiwa kudondoka kanisani hapo, waliosema walikuwa wakitokea Mwanza wakielekea Mtwara.

Akiwa na wachungaji wengine wa kanisa hilo, Dk. Rwakatare, aliwaombea watoto hao na kuwaeleza waumini wake kuwa, hayo ni matunda ya maombi yao na kwamba ‘Yesu wa kanisa lao’ anatenda miujiza.

Kwa muda mrefu sasa, kumekuwa na taarifa za watu wanaotuhumiwa kujihusisha na masuala ya kishirikina kudondoka kutoka angani kila mara wanapopita katika anga za baadhi ya makanisa nchini.

Hata hivyo, matukio hayo ambayo yamekuwa yakiripotiwa makanisani na katika vyombo kadhaa vya habari, yamekuwa yakiibua maswali mbalimbali kuhusu uthabiti wake ambao ni vigumu kutolewa maelezo katika hali ya kawaida.


Kutoka: Tanzania Daima

juu
Maoni ya Wasomaji

Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 6 yameshatolewa.

(Nawe toa maoni yako!)

hii inadhihirisha tu jinsi ambavyo hawa wachungaji wetu, wengi wao ni fix-kamba tu...otherwise huyu mama angekua serious na nguvu za roho mtakatifu, angeweza kutambua hilo mapema...sometimes GOD exposes the other side of a person thru simple acts...after all,siasa na dini wapi na wapi?

na mdau, dsm, - 29.03.08 @ 10:20 | #3962

Acheni kuwatapeli watu kwa kisingizio cha kuwa na uwezo wa kiungu. Hii tabia inayofanywa na baadhi ya makanisa na wachingaji wao eti wananguvu ya kiungu ni uhuni na utapeli na inakera sana. Watoto hawa wasilaumiwe, bali wanaowatumia kwa maslahi yao binafsi ndo wa kulaumiwa. Siamini watoto wadogo kama hawa wakabuni mkakati huu wanaodaiwa kuuendesha, lazima viongozi wa makanisa wanaojifanya wananguvu ya uungu wanawatumia kujitangazia umaarufu na kujipatia wafuasi. Yakowapi sasa.

na Kely - 29.03.08 @ 10:21 | #3963

nakubaliana nawe mdau. Mungu hamfichi mnafiki.

na Kely - 29.03.08 @ 10:24 | #3965

Ama kweli duniani kuna mambo! yaani Mchungaji, Dr. Rwakatare na waumini wote wa Kanisa la Mikocheni wameingizwa mkenge na hao watoto?

Watoto Yusufu na Ramadhani inabidi watafutiwe Chuo wasome ili waendeleze vipaji vyao vya usanii, Taifa lisiache tu vipaji kama hivyo vikapotea bure!

na A.S. Mbweni, DSM, - 29.03.08 @ 10:26 | #3967

Huu mama ni mbunge.Hivi kweli tunakuwa na wabunge wapumbavu namna hii. Sasa huko bungeni ataenda kusema nini kama anaweza kuwa na akili ndogo kiasi cha kutapeliwa na watoto. Linalo nitia uchungu ni kwamba anaweza kuwadanganya waumini wake kwamba ana nguvu za kiroho wakati anajua fika kwamba hamna lolote. Huu ni ufisadi, tena ufisadi mkubwa sana. Hawa wachungaji wanaojitia wana nguvu za kiroho ni mafisadi wakubwa. Kazi yao ni kutapeli tu watu dhaifu wasiokuwa na muono wa maisha. Hawa ni wakufilisiwa tu hamna jingine.

na chombeza, bongo, - 29.03.08 @ 10:41 | #3971

Acha usanii wewe mama lwakatare na kwa nini kanisa lako una liita mikocheni b assemblies of God instead of TANZANIA assembies of God.
Kwa nini hujatumie kile kitambaa chako kuwajua watoto hao kwa kipindi chote ulichokuwa unatangaza kudondoka kwa watoto hao na ukawaita misukule????????????

na P.K.Mduma, Dar, - 29.03.08 @ 10:44 | #3973





Hata kaburini, Mwalimu bado

anatusikitikia Watanzania


“KAMA mtaamua fedha kuwa ndio chanzo cha kuwapatia viongozi, basi mjue nchi inakwisha na CCM inakwisha. Oh! Nawasikitikia Watanzania wenzangu waliokuwa na uwezo wa kuongoza lakini hawana fedha, wataukosa uongozi.”

Hayo yalipata kutamkwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere katika moja ya hotuba zake wakati wa uhai wake.

Naam sherehe za Maulid na Pasaka za mwaka huu ziliambatana na kauli nzito za viongozi wa dini za Kikristo na Kiislamu kukemea ufisadi ulioshamiri nchini na hususan unaofanywa na viongozi.

Kimsingi, mashehe, mapadri na maaskofu ni viongozi wa kiroho. Viongozi wa kidini wana nafasi kubwa katika jamii yenye waumini wengi wa dini hizi kubwa mbili; Uislamu na Ukristo.

Tafsiri ya kemeo la viongozi wa kidini juu ya ufisadi ni kuitahadharisha Serikali juu ya kinachoendelea katika jamii na athari zake mbaya. Ukiona katika jamii viongozi wa kidini wamekaa kimya muda mrefu bila kutoa kauli za kuitahadharisha serikali, basi, ujue mambo yanakwenda vema.

Maana, si kazi ya mashehe na maaskofu kusimama na kuitetea au kuipongeza serikali. Hiyo ni kazi ya wanasiasa na wadau wengine wa masuala ya kiutawala.

Lakini mambo yanapokwenda kombo, ni kazi na wajibu wa mashehe, mapadri, maaskofu na hata viongozi wa imani za kijadi kusimama na kusema, kwa ukweli kabisa na bila ya chembe ya fitina au unafiki, kuwa mambo yanakwenda kombo. Na ndiyo maana ya kauli za viongozi wa kidini kuwa kuna ufisadi unaotokana na ubinafsi wa viongozi zinachukuliwa kwa uzito mkubwa na waumini wa dini zote na hata wasio waumini.

Huko nyuma tumeona matumizi makubwa ya fedha katika kutafuta uongozi. Hata sehemu ya fedha zilizopotea katika akaunti ya EPA inadaiwa zimetumika katika masuala ya uchaguzi kwa maana kutumika katika kuwapata viongozi. Ndipo hapa tunapaswa kurejea kauli ya busara ya Mwalimu hapo juu. Ni kweli, baadhi wameamua kutumia fedha kama chanzo cha kupata uongozi, na ni kweli sasa CCM inayumba na nchi inakwenda kombo.

Rais na Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete ana wajibu wa kwanza wa kuhakikisha imani ya wananchi kwake na Serikali yake inarudi haraka na kubaki. Hivyo basi, ana wajibu wa kwanza wa kuongoza harakati za kukisafisha chama chake ili kiondokane na kundi dogo la viongozi walioonyesha wazi wazi hulka za kifisadi. Jambo hili lina lazima ya kufanyika.

Naam. Viongozi wetu wa sasa wanahitaji kuambiwa mipaka yao kwa maana ya kuwa na miiko ya uongozi itakayowekwa wazi na ikajulikana na umma. Na adhabu ziainishwe kwa watakaokiuka miiko hiyo. Miiko ya uongozi yaweza kuwa tiba ya kuondokana na viongozi mafisadi wenye kutanguliza ubinafsi. Na hilo la ubinafsi ndilo lenye kuchangia sana vitendo vya kifisadi.

Kuna wanaoutafuta uongozi kwa maslahi yao binafsi. Inahusu haki pia. Na hii ni hoja ya msingi. Tumeona hata mifano ya baadhi ya viongozi waliotumia hila kukwapua nyumba za Serikali ili baadaye waje wazitumie kwa maslahi yao binafsi.

Ni hao, ambao bila haya, wanafanya dhuluma kubwa kwa wananchi wanaodai wanawaongoza. Baadhi yao kimsingi ni wahalifu kwa maana vitendo vyao vya kuhujumu mali za umma ni vya kihalifu. Hawa hawawatendei haki wananchi wanaodai wanawaongoza.

Siku zote, kujipendelea ndilo shina la maovu. Mathalan, tunaamini lililosababisha uamuzi wa kuuza nyumba za Serikali ni ubinafsi na hulka ya baadhi ya viongozi kutaka kujipendelea. Ni ajabu sana kwa viongozi hawa kutafuta hila za kukwapua nyumba za Serikali kwa kisingizio cha shida ya makazi wakati wa kustaafu wakati asilimia kubwa ya viongozi wetu waandamizi tayari wanazo nyumba walizojenga na nyingine kupangisha!

Naam. Siku zote, hamu inakuwa ni jambo jema, endapo binadamu ataweza kuitawala hamu yake.Tusipoitawala hamu yetu, tukaanza kujipendelea, kuwasahau wengine, basi, hilo huwa ndio chimbuko la maovu, huleta kutoelewana baina ya wanandugu na hata kwa maswahiba walioshibana. Huzua vurugu na machafuko katika jamii. Tunazungumzia uwepo wa upendo, haki na usawa.

Dini nyingi zinazungumzia umuhimu wa upendo, haki na usawa katika jamii. Iwe ni Uislamu na Ukristo vivyo hivyo. ” Naapa kwa zama . Hakika binadamu wote wamo katika hasara isipokuwa wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri. Wakahusiana na haki na wakahusiana na subira” (Koran tukufu, Surat ASWR)

Na Biblia inasema kuwa Kaini alikuwa mtu wa kujipendelea mno, akamwua nduguye. Mfalme Saulo alijipendelea mno, akamdhulumu Daudi. Yuda alijipendelea mno, akaiba fedha za wenzake, hatimaye akamsaliti Yesu.

Ikumbukwe, mwaka 1966 kabla ya Azimio la Arusha, Mwalimu Nyerere na TANU waliliona tatizo la baadhi ya viongozi kuwa na tamaa ya kuishi kifahari na kujipendelea. Baadhi ya viongozi na hususan jijini Dar Es Salaam walianza ujenzi wa majumba ambayo baadaye yalipangishwa hata kwa ofisi za kibalozi au mashirika ya kimataifa. Jambo hilo linaandikwa na mwandishi Cranford Pratt katika kitabu chake; ” The Critical Phase In Tanzania 1945-1968).

Haikuwa haramu kwa viongozi kujijengea majumba ya kupangisha, kwani viongozi wa wakati huo walijenga nyumba hizo kwa kutumia mikopo ya watumishi. Hata hivyo, kulingana na sera za TANU za Ujamaa na Kujitegemea, Mwalimu Nyerere na TANU waliona haja ya kubadilisha taratibu hizo za mikopo ili kupunguza wimbi la viongozi kujijengea majumba ya kupangisha na kuongezeka kwa pengo la kipato kati ya viongozi na wanaowaongoza, yaani wananchi. Nyerere na Rashidi Kawawa waliamua kulishughulikia jambo hili kwa kupitishwa azimio la NEC ya TANU . Ndipo hapa tunaona chimbuko la miiko ya uongozi katika Azimio la Arusha.

Miaka ile ya 1960 TANU ililiona hilo la kiongozi kukopa na kujenga kuwa ni dhambi kwa vile iliona hatari ya kuwapo kwa pengo kubwa kati ya waongozao na waongozwao. Masikini, viongozi wale katika uadilifu wao, hawakujiwa hata na wazo la kuzigeuza nyumba za Serikali kuwa mali yao. Walichotaka ilikuwa ni mikopo tu, wajenge nyumba wapangishe, na bado haikuwa sahihi kwa mazingira ya wakati ule.

Mwalimu Nyerere aliziona nyumba za serikali, alikuwa na uwezo wa kutumia mamlaka yake na kukwapua yeyote aliyoitaka na kuifanya kuwa mali yake, akawapa hata wanae, nduguze na marafiki. Lakini akaamua kuchukua mkopo na kujijengea nyumba yake pale Msasani. Kawawa ni mfano mwingine. Amepata kuwa Waziri Mkuu na nyadhifa nyingine nyingi. Naye aliziona nyumba za Serikali, lakini leo anaishi kule kijijini kwake Kiluvya kwenye nyumba aliyojenga kwa jasho lake. Kuna mifano mingine mingi ya viongozi wa namna hiyo. Bila shaka, kuendekeza ubinafsi kunachangia katika mamuzi yasiyo na maslahi kwa taifa kama vile Richmond, IPTL na miradi mingineyo.

Kama vikao vya CCM kule Butiama havitafaulu kuja na azimio au taratibu zitakazoweza kukisafisha chama hicho na kuondokana na mafisadi wachache ndani ya chama hicho, basi, hata Mwalimu akiwa kaburini kwake Butiama , bado ataendelea kutusikitikia Watanzania wake aliotupenda kwa dhati.

Ikumbukwe siku zote, kuwa jambo zuri na la halali, daima litabaki kuwa ni zuri na la halali hata kama hakuna mwenye kuitenda halali hiyo. Na jambo baya na haramu, daima litabaki kuwa ni jambo baya na la haramu hata kama ni wengi wenye kuifanya haramu hiyo. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.

0754 678 252
mjengwamaggid@gmail.com
http://mjengwa.blogspot.com


Kutoka gazeti la Raia Mwema wiki hii


Friday, March 28, 2008

Laana ya mwaka!!!


Na Imelda Mtema, Mkuranga


Hii ni laana! Wakazi wa Kijiji cha Mwalusembe kilichopo Mkuranga mkoani Pwani, wanadai kushangazwa na familia moja iliyopo kijijini hapo kwa madai baba mwenye nyumba na mkewe wanafanya ngono na watoto wao.....

Chanzo chetu cha habari kilitupasha kuwa, sakata la familia hiyo kwa baba kula mayai yake na mama pia kuwavulia nguo wanawe wa kiume, lilianza muda mrefu lakini lilizimwa kimyakimya, huku wazee wa kijiji wakiamua kutumia busara zao kurekebisha mambo.

Mpashaji wetu alidai baba wa familia (jina tunalihifadhi kwa sasa) ndiye aliyeanza tabia hiyo chafu ya kufanya mapenzi na binti zake na kuna siku alifumwa na mkewe (jina tunalo) akivunja amri ya sita akiwa na mwanawe.

Inadaiwa mke alitishia kuondoka ndipo mumewe alipoomba msamaha na kuahidi kutorudia tena kitendo hicho, huku mama mwenye nyumba akikubali kwa sharti la mzee huyo kutowasogelea binti zake.

“Mzee (akimtaja jina) hakukoma, kwani baada ya muda alihamia kwa mtoto wake mwingine aliyekuwa anasoma na kuanza kufanya naye mapenzi, kitendo hicho kilimkasirisha mkewe ambaye aliamua kumshawishi mtoto wake wa kiume nao wazini,” kilisema chanzo chetu.

Mwandishi wa habari hizi alipofika kijijini hapo ili kujua hali halisi, baadhi ya wanakijiji walikiri kuwepo kwa tukio hilo na kudai linawakera kwani inaonekana kama ni laana kwao.

Aidha, mzee anayetuhumiwa kutembea na wanawe wa kike, alikana kuwepo kwa kitu hicho na kudai kuna hali ya kumuonea wivu, kwani huo uvumi unasambazwa na wasiomtakia mema.

Mkewe naye alikataa kutokea kwa tukio hilo la wao kutembea na watoto wao, huku akisisitiza ni majungu ya watu wasiopenda kuona maendeleo yao.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwalusembe, Manzi Mkomo alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alikiri kulisikia lakini akadai halijafikishwa mezani kwake kushughulikiwa kwani ni suala la kifamilia zaidi.

“Hili ni suala la kifamilia na inaonekana limemalizwa na wao wenyewe, lakini nimesikia kuwepo kwa tukio hilo ila sijui kama ni kweli, kwani sijalithibitisha zaidi ya kusikia maneno yaliyozagaa hapa kijijini juu ya tukio hilo, “ alisema.

Kutoka gazeti la Ijumaa, 28 Machi 2008


Na Imelda Mtema

Mke wa mwanamuziki wa dansi nchini Muumini Mwinjuma, Chiku Kasika amekunywa sumu kwa nia ya kutaka kujiua, kwa kile kilichodaiwa ni baada ya kunyimwa talaka na mumewe....

Akizungumza na Ijumaa, mtoa habari kwetu alisema Chiku alikunywa sumu hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita akiwa nyumbani kwake Tandale kwa Mtogole, Dar es Salaam.

Shuhuda wetu alitupasha kuwa, mara baada ya kunywa sumu kulisikika mikoromo hali iliyosababisha majirani kuvamia nyumbani kwake na kumkuta akigaagaa chini kwa maumivu.

Chanzo chetu kinasema, majirani hao kuona hivyo waliamua kukodisha teksi na kumkimbiza katika Hospitali ya Mwananyamala, alipofikishwa madaktari walianza kuhaha ili kuokoa maisha yake.

Mtoa habari kwetu alidai kuwa, kwa muda mrefu sasa, Chiku alikuwa anadai talaka baada ya kuchoshwa na mienendo isiyoridhisha ya mumewe ambayo kwake aliona kama inamdhalilisha.

Chanzo chetu kilidai kuwa, Muumini aligoma kutoa talaka kwa kile alichoona jamii itamfikiria vibaya kutokana na kitendo chake cha kuoa na kuacha kila mara. Kwa Muumini Chiku ni mke wake wa tatu.

Baada ya Muumini kugoma kutoa talaka, inadaiwa Chiku alikasirika na kuamua kununua sumu ya panya na kunywa, kabla ya majirani kumuwahi na kumkimbiza Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam ili kuokoa maisha yake.

“Chiku ameshachoka na mambo ya Muumini ndiyo maana aliamua kudai talaka na aliponyimwa aliamua kunywa sumu,” kilisema chanzo chetu.

Mwandishi wa habari hizi alifika katika Hospitali ya Mwananyamala na kumkuta Chiku amelazwa katika Wodi na. 15, huku akiwa hoi na amewekewa dripu.

Alipoulizwa kiini cha yeye kunywa sumu, alianza kulia kwa sauti kubwa huku akidai kuna matatizo makubwa yaliyomsababisha achukue hatua hiyo.

“Samahani sana dada yangu acha tu ni matatizo makubwa ndugu yangu, nitakapojaliwa kutoka ndio nitaeleza vizuri kila kitu,” alisema Chiku huku akilia.

Muumini alipoulizwa kuhusu hilo, alitupa lawama na kudai anashangaa anafuatwa yeye kwani kuna watu wengi wanafumaniwa lakini hawaandikwi.

“Mimi kama mke wangu kanywa sumu mngemuuliza yeye mwenyewe, lakini mimi sina jibu labda mngeniuliza mafanikio yangu tu ndiyo ningewajibu.”

Habari tulizozipata wakati tunaenda mitamboni zinasema Chiku aliruhusiwa kutoka hospitalini hapo juzi Jumatano.





Norway kusaidia bilioni 1.8/-

sekta ya asasi za kiraia


Daily News; Friday,March 28, 2008 @00:04


SERIKALI ya Norway kupitia Wizara yake ya Mambo ya Nje, imekubali kutoa Dola za Marekani 1,578,747 ( Sh 1,881,082,554) kwa ajili ya kusaidia Taasisi ya Mfuko wa Vyama vya Kiraia (Foundation for Civil Society) katika kuimarisha sekta ya asasi za kiraia nchini.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, John Ulanga, msaada huo ambao umelenga kuziimarisha asasi nchini kwa miaka mitatu, upo katika mkataba uliosainiwa kati ya Balozi wa Norway, Jon Lomoy na Ulanga mwenyewe.

“Kiwango hicho kilichokubaliwa kitatolewa kwa awamu kufuatana na maombi yatakayotolewa na taasisi hii na kiwango cha kwanza cha NOK 1,500,000 kitatolewa mara tu baada ya kusaini mkataba,” alisema Ulanga. Alisema Norway ni miongoni mwa wafadhili wakuu wa taasisi hiyo tangu mwaka 2004, na hadi mwaka jana, ilikuwa imeshaisaidia Taasisi hiyo Dola za Marekani 945.951.

Taasisi hiyo hujenga uwezo wa asasi za kiraia kwa mwelekeo wa kuziwezesha kuchangia katika kuwashirikisha wananchi vyema katika mchakato wa kidemokrasia na kuwafanya waelewe, wadai na wapate haki zao, alisema.

Alisema tangu mwaka 2003 ilipoanzishwa taasisi hiyo hadi Desemba 2007, imeidhinisha ruzuku yenye thamani ya Sh bilioni 20 na kati ya hizo Sh bilioni 14 zimeshatolewa kwa wafadhiliwa wa taasisi hiyo.


'Peeping Tom' plagues

roadside restrooms


A kinky problem continues to confound maintenance workers along the highway that winds through the scenic valley of Gudbrandsdalen in Norway.

Maintenance workers plug the holes, and new ones reappear within a week.

PHOTO: JOHANNES GRÃ…BERG/VEGVESENET


Someone has been drilling holes into the walls of public roadside restrooms in the area around Lillehammer.

The first holes were found more than 10 years ago. Maintenance workers patched them up, only to find new holes drilled shortly thereafter.

The problem has persisted, with new holes being found in a restroom near the Vingrom Church as recently as during last week's Easter holiday.

The state highway workers don't think the holes are being drilled to increase ventilation in the restrooms. They think someone is using them to spy on those using the public toilet facilities.

"We have discussed who might be behind this, but haven't come to any conclusions," said Johannes Gråberg, building leader of the Sør-Gudbrandsdalen district of the state highway department (Vegvesenet)

"I can't even say whether it's the same person drilling the holes," Gråberg added. "A few years ago we thought we were on the trail of someone, but don't know if it's the same person now."

Reststops at Vingrom and Skarsmoen have been hit the hardest, but holes have also been drilled at reststops between Gjøvik and LIllehammer, and along the E6 highway at Sjoa, south of Otta. Sometimes it only takes a few days before metal plates set up to cover the holes are found to have been removed, or new holes emerge.

"Sometimes we've had to repair the same place twice in the course of a week," Gråberg said. The highway department hasn't, however, received any reports from people reporting uncomfortable experiences at the rest stops.

Aftenposten's reporter
Marie Norum Lerbak

Aftenposten English Web Desk
Nina Berglund


Thursday, March 27, 2008



Confirmed: Tanzania

has strong oil deposits



ALVAR MWAKYUSA
Dar es Salaam

LABORATORY test results of liquid hydrocarbons extracted by Canada’s Artumas Group at Mnazi Bay in Mtwara Region last year have established that there is high quality crude oil in the area, it has been confirmed.

The Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) Managing Director, Yona Killagane, told a press conference in Dar es Salaam yesterday that Artumas is now studying whether there are enough reserves to warrant commercial exploitation.

He was echoed by TPDC’s Chief Exploration Geologist Herry Kajato, who said Artumas is drilling more wells in the area to determine whether the oil deposits justify large investments required to commercially extract the commodity.

’’Hydrocarbons results from wells number 2, 3 and 4, which are licensed to Artumas, have showed positive results. However, in order to determine if the project is viable for commercial purposes, the company is currently undertaking further surveys and assessments,’’ said Kajato.

He stated that after two months of assessment, the viability of the project for commercial purposes will be known.

Artumas last year announced discovery of hydrocarbons at Mnazi Bay in Mtwara Region, where it had drilled about 50 barrels for testing. According to exploration geologists, hydrocarbons are a good sign of existence of oil.

The company said in a statement earlier this year that substantial crude oil potential has been observed in the Ruvuma basin lying midway between Tanzania and Mozambique.

According to an announcement by Artumas Group Energy & Power, the Canadian-based parent company of Artumas Tanzania Limited, 86 barrels of liquid hydrocarbons from Mtwara Region had been sent abroad for evaluation.

’’In November (last year), Artumas successfully completed a $170m (approx. 170.025m/-) financing enabling the next stage of exploration and development over the upcoming two years, with proposed capital spending of $124m (approx. 124.018m/-) on its upstream work programme for both Mozambique and Tanzania,’’ the company said.

It declared progress in developing its assets in Tanzania and Mozambique, saying market confidence in the company and potential to deliver had been confirmed by the successful $170m equity and debt issue earlier this year.

’’We are well capitalized to move forward with our planned activities through 2008. One of the greatest challenges for any E&P company in today’s environment is access to exploration acreage,’’ said Artumas Group Chief Executive Officer, Stephen Mason.

He said the 25,000-square kilometre land position that the company is operating in the Ruvuma basin is recognized as a ’’highly potential deltaic basin’’ and gives Artumas substantial room to run in growing its resource base.

Artumas has also announced significant progress in power sales from its 12-megawatt Mtwara energy project increasing by 8.7 per cent over the second quarter average this year.

An ’arranger agreement’ with Dutch FMO was completed to facilitate the financing of Artumas planned 300MW integrated power project also in Mtwara Region. FMO will act as arranger for two structured finance facilities for the power generation plant and the high-voltage transmission interconnect to the Tanzania grid, estimated at $225m and $400m respectively.

Kikwete azindua shirika la

utangazaji Tanzania (TBC)



Raisi Jakaya Mrisho Kikwete,akisoma hotuba wakati wa uzinduzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jana mchana jijini Dar-es-salaam.TBC imezinduliwa upya rasmi jana pamoja na nembo/logo mpya ya shirika hilo.Kuanzia sasa, iliyokuwa Televisheni ya Taifa (TVT) itaitwa TBC-One na iliyokuwa Radio (PRT) itaitwa TBC-FM na pia kutakuwepo na External Service itakayoitwa TBC International.

Wengine pichani (kulia kwa JK) ni First Lady,Mama Salma Kikwete na Tido Mhando ambaye ndio Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo.Kabla ya kurudi Tanzania kushika wadhifa huo mpya,Tido Mhando alikuwa Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC)




Nembo mpya ya Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC).Nembo ina kauli mbiu ya Ukweli na Uhakika. Ni matumaini yetu kwamba hivyo ndivyo itakavyokuwa na si vinginevyo.Picha zote na Ahmad Michuzi.

Habari toka Bongo Celebrity


Collapsed building still burning,

victims inside


Firefighters in the west coast city of Ã…lesund were trying Thursday morning to cool down fires that continued to burn inside a residential building destroyed by a landslide. Five persons remain trapped inside.

This aerial photo shows how the hill behind the newly built condominium complex gave way.

PHOTO: ODD MEHUS/BERGENS TIDENDE

Related stories:

The fires sparked by gas leaks, along with the building's instability, have blocked rescue workers' attempts to reach victims.

It's believed that five residents living on the building's lower floors were caught under the rubble. The landslide hit just before 4am Wednesday, knocking the building off its foundation and causing the lower floors to collapse.

The neighbourhood around the building on Fjelltunvegen, not far from downtown, also remained evacuated Thursday morning. Fear of explosions from the fires and leaking gas prevented residents from returning to their homes.

Police said it was impossible for emergency workers to enter the building until the gas had burned out. There was less smoke than on Wednesday, and firefighters believed they had control over the burning wreckage.

Fifteen of the building's 21 residents were rescued after the landslide hit, one resident was said to be away on a trip and five others are believed to have been caught inside and are feared dead.

Speculation over the cause of the landslide continued to rage. One geologist said he'd warned that the hill behind the building, completed just four years ago, could give way.

Others, however, said it had been secured and the building's developer and contractor claimed all regulations and re-enforcement measures had been followed. City officials had issued building permits after approving plans submitted.

Norway has a long history of land- and rockslides, and many of them have occurred in the western, mountainous area near Ã…lesund. Some geologists claim that warmer and wetter weather raises the danger of slides.

Aftenposten English Web Desk
Nina Berglund

Soccer boss found guilty



Morgan Andersen, who played a key role in the controversial transfer of young Nigerian player John Obi Mikel to top British club Manchester United, was found guilty on Wednesday of contract forgery. The former director of Oslo club Lyn was also convicted of filing a false police report against Mikel's agent.

Morgan Andersen

PHOTO: HÃ…KON MOSVOLD LARSEN/SCANPIX

Related stories:

A court in Oslo found Andersen guilty on all counts of his indictment and handed him a one-year suspended jail term, meaning he won't actually have to spend time in prison.

Andersen appealed the court's decision on the spot nonetheless. He has vigorously denied all charges of falsifying documents.

Prosecutors had sought a year in prison for Andersen, with just half of it suspended, mainly for forging a contract it claimed it had with Lyn's former rising star Mikel.

Prosecutor Svein Holden claimed Andersen, who later went to work for Fredrikstad Football Club, falsified the contract so that Lyn and its owner, businessman Atle Brynestad, could claim rights to sell Mikel to top British club Manchester United, profit from the transfer and from any subsequent transfers.

Mikel and his agent had claimed all along that Mikel wanted to play for top London club Chelsea and was merely spending time at Lyn until he was old enough to sign a professional deal with Chelsea. Instead, Andersen claimed Lyn had rights to Mikel, and the right to transfer him to Manchester United.

The two British clubs ultimately struck a deal allowing Mikel to land at Chelsea, where he currently plays. Mikel testified in court that Andersen had lied, and insisted he never had a contract with Lyn.

The case shed light on the money and power plays behind professional soccer. Some observers likened the buying and selling of Mikel to human trafficking, as agents and club managers sought ways of getting around international regulations aimed at protecting young players.

Aftenposten English Web Desk
Nina Berglund


Wednesday, March 26, 2008

Brick & Lace waahidi makubwa kesho


na Khadija Kalili tarehe 27.03.2008

WASANII mahiri wa kundi la Brick & Lace wanaotamba na miondoko ya R&B kutoka Jamaica, wameahidi shoo ya aina yake watakapotumbuiza kesho katika fainali za kumsaka nyota wa Bongo ‘Bongo Stars Search’ zitakazorindima kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana kwenye hoteli ya Movenpick, wasanii hao ambao wanatamba na wimbo wao unaofahamika kama, ‘Your Love is Wicked’, walisema wamekuja Tanzania kuwapa raha na si vinginevyo.

Wamewataka mashabiki wa muziki kufika kwa wingi ili kupata burudani ya uhakika, ambako wamewaandalia vitu vya uhakika.

Kundi hilo liliwasili jana jijini Dar es Salaam na kufikia Hoteli ya Movenpick ambako kesho litaungana na wasanii mbalimbali katika kupamba fainali hizo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Benchmark Productions, ambao ndiyo waratibu wa shindano hilo, Rita Paulsen alisema kwamba maandalizi ya fainali za shindano hilo yamekamilika, hivyo mashabiki wajitayarishe kumpata mrithi wa mshindi wa BSS wa mwaka jana, Jumanne Idd.

Rita alisema, mshindi katika fainali hizo, atapatikana kutokana na kupigiwa kura na mashabiki, hivyo mashabiki wawapigie kura washiriki ambao wanaona wanafaa kutwaa taji hilo.

“Mashabiki wana asilimia yao ya kumteua mshindi, kadhalika na majaji nao tuna nafasi yetu ya kutoa kura kwa washiriki pia, hivyo kila shabiki anapaswa kutambua kwamba ana wajibu wa kumchagua yule ambaye anaona kwamba anafaa kuwa mshindi wa BSS 2008,” alisema Rita.

Washiriki watano watakaochuana katika fainali hizo na namba zao kwenye mabano ni Ellynema Mbwambo (BSS 16), Misoji Nkwabi (BSS 11), Maangaza Nyange (BSS 05), Yohana Simon (BSS 14) na Rogers Lucas (03).


Brick & Lace kutua Dar es Salaam


na Khadija Kalili, tarehe 26.03.2008





Brick & Lace. Picha kutoka:
http://www.brickandlacemusic.com


Sikiliza "Love is Wicked"






WASANII mahiri wa kundi la Brick & Lace wanaotamba na miondoko ya R&B kutoka Jamaica, wanatarajiwa kuwasili nchini leo, mahusus kwa ajili ya kupamba fainali za shindano la kumsaka nyota bora wa bongo katika Bongo Stars Search, zitakazorindima Ijumaa, katika mbanda wa Blue Pear, Ubungo, Dar es Salaam.

Brick na Lace ambao wimbo wao unatamba katika kumbi mbalimbali za burudani unaofahamika kama ‘Your Love is Wicked’, watazungumza na waandishi wa habari, kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), mara baada ya kuwasili nchini.

Akizungumza jijini, jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Benchmark Productions, waratibu wa shindano hilo, Rita Paulsen, alisema kwamba maandalizi ya fainali za shindano hilo, yamekamilika, hivyo mashabiki wajitayarishe kumpata mrithi wa aliyekuwa mwasisi na mshindi wa BSS wa mwaka jana, Jumanne Iddi.

Rita alisema mshindi katika fainali hizo za Machi 28, atapatikana kutokana na kupigiwa kura na mashabiki, hivyo mashabiki wawapigie kura washiriki wanaoona wanafaa kutwaa taji hilo.

“Mashabiki wana asilimia yao ya kumteua mshindi, kadhalika na majaji nao tuna nafasi yetu ya kutoa kura kwa washiriki pia, hivyo kila shabiki anapaswa kutambua kwamba ana wajibu wa kumchagua yule anayeona kwamba anafaa kuwa mshindi wa BSS 2008,” alisema Rita.

Washiriki watano watakaochuana katika fainali hizo na namba zao kwenye mabano ni pamoja na Ellynema Mbwambo (BSS 16), Misoji Nkwabi (BSS 11), Maangaza Nyange (BSS 05), Yohana Simon (BSS 14) na Rogers Lucas.

Chanzo: Tanzania Daima