Wednesday, April 30, 2014
Tuesday, April 29, 2014
Monday, April 28, 2014
Saturday, April 26, 2014
Friday, April 25, 2014
British couple to sue Tanzania over farm deal that 'ended in death threats'
Stewart Middleton. and Sarah Hermitage
A British couple aim to take Tanzania to an international arbitration court after they were forced to flee following what they say was a campaign of harassment and intimidation, including death threats. If it goes to court, the case could prove embarrassing for the UK and Tanzania at a time when the British government is promoting private investment in the east African country....
Thursday, April 24, 2014
Aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba, jaji mstaafu, Joseph Warioba, ameeleza wasiwasi wake juu ya lugha zinazotumiwa na wajumbe wa bunge maalum la katiba na kwamba hazimpi matumaini kama wanaweza kufikia maridhiano, huku akiwaonya wajumbe hao kuacha malumbano badala yake watafute njia ya kushirikiana.
Wednesday, April 23, 2014
Tuesday, April 22, 2014
Last week’s “robbery” at Barclays Bank’s Kinondoni branch (Dar es Salaam), where armed gangsters reportedly grabbed Sh300 million, was faked
Dar es Salaam
(The Citizen, Tuesday, 22.04.2014). Last week’s “robbery” at Barclays
Bank’s Kinondoni branch,
where armed gangsters reportedly grabbed Sh300 million, was faked, The Citizen
can authoritatively report.
Impeccable
sources close to the ongoing investigation into the incident confided in The
Citizen that the “raid” by three men was planned and executed to cover up the
theft of tens of millions of shillings that had previously taken place at the
branch.
Some
employees at the branch are said to have colluded with rogue police officers to
fake a robbery in an attempt to hide the truth about the theft. The workers,
including a senior official at the branch, are among those being held for
questioning.
According
to our inquiries, detectives are also looking for a police officer from Oyster
Bay Police Station, who disappeared as investigators zeroed in on him.
The
officer vanished after learning that one of the suspects had told detectives
about the stage-managed “raid” and the role of the fugitive.
Yesterday,
Dar es Salaam
police boss Suleiman Kova declined
to give details about the progress of the investigation, saying he would do so
today at a news conference.
Asked
about the whereabouts of the fugitive police officer, Mr Kova said: “We are still gathering and
receiving more information and will give a comprehensive statement at a media
briefing later.”
Earlier, Kinondoni Regional Police Commander Camillius Wambura told The Citizen that briefings on the
incident would henceforth be provided by Mr Kova.
Contacted
for comment yesterday, Barclays head of Marketing and Communications Neema-Rose Singo told The Citizen that she had nothing
to say as it was a public holiday.
According
to eyewitnesses, the “robbery” took place at around 9.30am last Tuesday and
involved three men, who had arrived at the bank on a motorcycle. One remained
outside while his accomplices entered the branch and walked out a few minutes
later with a big bag that was purportedly stuffed with hundreds of millions of
shillings.
The
three men jumped on their motorcycle and sped away. Police arrived at the scene
about 20 minutes later.
No
shot was fired and the casual manner of the “robbers” raised eyebrows.
A day
after the incident, some employees at the bank and several other people were
arrested and their mobile phones confiscated by police as part of the
investigation.
The
source said the suspects were questioned separately in the presence of Mr Wambura and other senior police officers.
According
to the source, drama unfolded when one of the bank’s employees volunteered to
spill the beans as soon as he entered the interrogation room.
“He
pleaded with investigators not to be too hard on him as he was ready to reveal
the truth.
“At
that juncture, one of the police officers (name withheld) asked to be allowed
to leave the room, saying he was not feeling well.
“As
soon as the officer had left, the Barclays employee said the officer who had
just gone out knew everything about the plot,” the source said.
The
employee told investigators that a huge amount of money had already been stolen
at the branch and the “robbery” was a way of covering up the theft. He said the
police officer
in question knew everything beforehand.
Noticing
that the officer was taking too long to return to the interrogation room, his
boss telephoned him, only to be told by the officer that he had gone home
because he was not feeling well.
When
his bosses decided to trace him to his home, the officer was nowhere to be
seen, and the gun he was carrying was found abandoned at a corner of the police
building.
Last
week, Ms Singo said
the bank and its employees would cooperate with police in their endeavour to
get to the bottom of the incident. The branch re-opened a day after the “raid”.
Police
are under the spotlight again after a gang raided the Kariakoo branch of Habib Bank and reportedly made off with Sh1
billion last August.
Police
have yet to arrest a suspect after what Mr Kova said
was an incident that had all the hallmarks of an inside job.
The
casual manner of the “robbers”, who nonchalantly strolled in and out of the
bank in broad daylight without bothering to hide their identities, has fuelled
complicity theories.
Some 48 hours
later, police still seemed to have no idea who they were.
Monday, April 21, 2014
Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe ametangaza kuungana na wanaodai Serikali ya Tanganyika na kuahidi kujenga ari na shauku ya kuhakikisha inarejeshwa.
ASKOFU KAKOBE;
Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe ametangaza kuungana na wanaodai Serikali ya Tanganyika na kuahidi kujenga ari na shauku ya kuhakikisha inarejeshwa.
Akizungumza wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika kanisani hapo jana, Askofu Kakobe alisema anafanya hivyo si kwa ushabiki ila ni kutokana na mipango ya Mungu, ambayo iliwezesha kuwapo kwa Tanganyika huru. Huku akishangiliwa na waumini wa kanisa hilo, Askofu Kakobe alisema wanaoidai Tanganyika katika Bunge la Katiba wapo sahihi na yeye anaungana nao na kuwa wanaopinga wamekosa hofu ya Mungu.
“Serikali ilitumia mamilioni ya shilingi kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru, lakini wanashindwa kutamka uhuru wa nchi gani!”
(Chanzo, Gazeti la Mwananchi, Jtatu - 21/04/2014)
Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), mjini Moshi, Kilimanjaro, Glorious Shoo amewatahadharisha wajumbe wa Bunge la Katiba kutotumia wingi wao bungeni kuzuia mabadiliko ya Katiba.
ASKOFU GLORIOUS SHOO;
Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), mjini Moshi, Kilimanjaro, Glorious Shoo amewatahadharisha wajumbe wa Bunge la Katiba kutotumia wingi wao bungeni kuzuia mabadiliko ya Katiba.
Akizungumza katika ibada ya Jubilee ya miaka 75 ya kanisa hilo, Askofu Shoo alisema umefika wakati ambao Watanzania wanataka mabadiliko, hivyo wajumbe wa Bunge Maalumu wasitumie wingi wao kuzuia mabadiliko.
“Tusilazimishe kwa wingi wetu kuzuia mabadiliko kwa sababu ukweli tunaposema wingi wetu ni pale bungeni tu, lakini wingi wetu sisi tulioko nje tunasikia kelele nyingi zinazolazimisha mabadiliko naiomba Serikali izingatie hilo,” alisema Askofu Shoo.
“Watu wanaosoma nyakati, wanajua ukifika wakati wa mabadiliko hakuna anayeweza kuzuia na ukijaribu kuyazuia mabadiliko hayo yanakuja kukubadilisha wewe,” alisema Askofu Shoo.
(Chanzo, Gazeti la Mwananchi, Jtatu - 21/04/2014)
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo, Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha mchakato wa Katiba kwa lengo la kunusuru amani ya Taifa.
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo, Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha mchakato wa Katiba kwa lengo la kunusuru amani ya Taifa.
Lusekelo alisema siyo lazima Katiba Mpya ipatikane mikononi mwa Rais Kikwete kwa kuwa hatua iliyofikiwa kwa sasa ni kubwa, hivyo inaweza kuendelezwa na Rais atakayefuatia mwaka 2015.
Akizungumza jana katika ibada ya Pasaka, Lusekelo alisema hali inayoendelea kwa sasa inajenga hofu na kuwachanganya Watanzania kutokana na hofu ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Alisema Bunge la Katiba kwa sasa limekuwa mfano wa klabu ya pombe za kienyeji kutokana na vurugu alizodai kuchangiwa na wajumbe wa CCM.
“Hakuna majadiliano ya kujenga hoja na badala yake tunasikia matusi tu yanarushwa... uamuzi wa Profesa Ibrahim Lipumba kutoka nje ulikuwa ni sahihi. Hata mimi iwapo ningekuwa mjumbe, ningekuwa wa kwanza kutoka,” alisema Lusekelo na kuongeza:
“Kwa hiyo ni vyema mchakato ukasitishwa kwa hatua iliyofikia ili Taifa litulie na wananchi wajiandae kwa Uchaguzi Mkuu ujao.”
(Chanzo Gazeti la Mwananchi Jtatu - 21/04/2014)
Sunday, April 20, 2014
MCHAKATO WA KATIBA MPYA - UJUMBE WA KICHUNGAJI WA PASAKA 2014 KWA WAAMINI NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA
“Sote tuwe na
Umoja” (rej. Yn 17:21)
UTANGULIZI:
Ndugu wapendwa, tunapohitimisha kipindi cha Kwaresima kilichokuwa na ujumbe: “Ukweli utawaweka huru” (Yn. 8: 32), tunawaletea ujumbe wa “Umoja” ili kuongeza msisitizo kwenye ujumbe wetu wa Kwaresma. Tunaitwa kukubali kuwa umoja ni ukweli msingi wa kila mafanikio ya jumuiya ya mwanadamu.
UTANGULIZI:
Ndugu wapendwa, tunapohitimisha kipindi cha Kwaresima kilichokuwa na ujumbe: “Ukweli utawaweka huru” (Yn. 8: 32), tunawaletea ujumbe wa “Umoja” ili kuongeza msisitizo kwenye ujumbe wetu wa Kwaresma. Tunaitwa kukubali kuwa umoja ni ukweli msingi wa kila mafanikio ya jumuiya ya mwanadamu.
Ufufuko ni Pasaka inayomaanisha kivuko au
kupita kwa Wayahudi toka kwenye matatizo ya utumwa hadi uhuru kamili. Kwa
Wakristo ni kuvuka kutoka utumwa wa fikra za kifo (dhambi) hadi uhuru kamili wa
ufufuko wetu na Bwana Yesu. Kwahiyo, furaha za Pasaka zinapaswa kusheheni
shukurani za dhati kwa zawadi nyingi alizotujalia Mungu Muumba wetu tokea
mwanzo na hasa nyakati hizi katika mwanga wa Ufufuko wa Kristo.
Adhimisho la Pasaka litawaliwe na furaha, amani
na matumaini makuu yaliyoletwa kwa Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo. Mtume
Paulo anatuambia: “Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu
Kristo” (1Kor. 15:57).
Wakati dhambi na kifo husababisha kujitenga;
uhuru, furaha na amani husababisha kuungana. Ndivyo ilivyotokea kwa Adamu na
Eva. Walipokuwa bila dhambi walikuwa huru, wenye furaha, amani na umoja na
Mungu. Walipotenda dhambi walimkimbia Mungu, wakatafuta kujificha. Hata wao
wenyewe walioneana aibu na hatimaye wakafukuzwa kutoka kwenye bustani ya Edeni
(Mwa. 2:25; 3:7-8, 23-24).
1.Ndugu zetu katika Kristo, “Amani iwe Kwenu”
(Yn. 20:19). Wakati huu wa Pasaka, wakati ambao pia mchakato wa kuandika Katiba
ya nchi yetu unaendelea, hatuwezi kuacha kutafakari kwa dhati juu ya umoja wetu
sisi Watanzania. Bila shaka, moja ya mihimili mikubwa ya umoja wa kitaifa ni
uongozi bora.
Mwenyezi Mungu aliwatoa watu wake utumwani
Misri na kuwaweka huru kwa kuwateulia viongozi miongoni mwao. Kiongozi wa
kwanza alikuwa Musa (Kut. 3:10).
• Chini ya uongozi wa Musa Wayahudi walichukua
muda mrefu kujenga umoja na uelewa, kwamba walikuwa watu wa Mungu na walipaswa
kumtambua kiongozi wao kama mteule wa Mungu (Kut. 16:3; 17:4;).
• Katika kutangatanga kwao jangwani,
iliwachukua pia muda mrefu kutambua uovu wao na kujitakasa dhidi ya dhambi zao
(Kut. 32:1-14).
• Hata wakiwa tayari katika nchi waliyoahidiwa
hawakuacha machukizo yao kwa Mungu pamoja na kukanywa mara kwa mara na Manabii
wake Mwenyezi Mungu (Amu. 2:11-13).
Wakati ulipowadia, Mungu alimtuma Mwanae Yesu
Kristo kujenga Utawala wa Mungu juu ya msingi wa imani na ukweli (Gal. 4:4):
• Imani kwa Mungu na imani baina ya watu
wenyewe – kuaminiana – ndio msingi wa Utawala wa Mungu (2Thes. 2:13-17).
• Lakini kutokana na udhaifu wa kibinadamu,
mara nyingi tunavunja umoja wetu na Mungu na kati yetu wenyewe kwa kiwango cha
kutotaka kuishi pamoja; tunabaguana na hatutendeani haki (Mwa. 4:7-8).
Katika ulimwengu wa leo, tunashuhudia madhara
ya utengano wa namna nyingi. Dhambi nyingi za binadamu zinasababisha mifarakano
na vita. Hayo ni matukio ya kila mara katika nchi nyingi ulimwenguni na hasa
kwetu Afrika. Hata historia yetu wenyewe ina matukio mengi ya jamii kufarakana
na kujizamisha katika vita.
• Mababu zetu walipitia maisha marefu ya
kuhamahama na kuchukuliwa utumwani na wengine kubaki watwana na watawaliwa wa
kikoloni kwa vipindi virefu kabla ya kujipatia uhuru wa kujitawala.
• Tulipopata uhuru, tulijifunza kujenga umoja
katika tofauti zetu kubwa za kikabila na kufikia taifa moja.
• Tulichukua hatua kubwa kuunganisha nchi mbili
huru, Tanganyika na Zanzibar, na kuifanya kuwa nchi moja ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ikiwa kielelezo kwa Bara la Afrika cha kujenga umoja.
2.Hatua zote hizo tulizopitia na tulizochukua
kwa makusudi kabisa, tulikuwa na nia na utashi wa kuwa wamoja. Tulitaka kujenga
maendeleo ya pamoja na mafanikio ya kila Mtanzania kufikia maisha bora.
Jitihada hizi njema zimekuwepo kwa miaka hamsini iliyopita. Tumefanikisha mambo
mengi katika umoja wetu ambao unatusukuma kumshukuru Mungu. Kwa muda mrefu
umoja wa Watanzania umeonekana kwa mataifa mengine kuwa ni kielelezo cha umoja
wa kitaifa wa hali ya juu sana. Ni umoja uliokua kufikia kiasi cha kufuta
tofauti za awali za mataifa yaliyohusika kuunda umoja.
Tunamshukru mwenyezi Mungu kwa kuifanya Nchi
yetu kuwa kimbilio la waliokata tamaa. Tanzania imewapa wakimbizi mahali salama
pa kuishi pamoja na Watanzania. Chini ya Jamhuhuri ya Muungano wa Tanzania,
waliokuwa bado chini ya wakoloni, waliandaliwa kujikomboa na kuwa mataifa huru.
Pamoja na mafanikio hayo makubwa, zimejitokeza
dosari kadhaa katika umoja zilizofanya umoja wetu upoteze baadhi ya sifa zake
za awali. Kupungua kwa hisia za kujisikia watu wote ni taifa moja, ni dosari
iliyoanza kukua taratibu na sasa inaonekana kuwa ndio ukweli. Baadhi ya
Watanzania wanafikiri kuwa umoja unaofuta tofauti haufai ila umoja unaosisitiza
tofauti kama ulivyo umoja wa kikanda (kama ilivyo SADC, ECOWAS, n.k) ndio
unafaa! Wakati mataifa mengine yanatamani umoja unaofanana na ule umoja wetu wa
awali, baadhi yetu tunatamani kurudi nyuma kwenye umoja wa mpito!
Kutokana na mapungufu yaliyodhihirika ndani ya
mafanikio yetu, umuhimu wa kufanya marekebisho ulidhihirika. Ni kwa sababu
hiyo, watu wengi walitaka na wanataka mabadiliko au mageuzi ya msingi sana. Kwa
msukumo huo ndio sababu tuliingia katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya.
3.Kazi ya kuandika Katiba si nyepesi na yataka
umakini mkubwa. Haishangazi sana tunapojionea mivutano na migongano ya hoja
kutoka kwa makundi kinzani katika nchi moja. Mawazo ya wengi yamewasilishwa
kisheria na Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa ajili ya kujadaliwa na Bunge
Maalum la Katiba (BMK). Sasa, tunashuhudia makundi yenye nguvu yakijaribu
kushinikiza kuingizwa matakwa yake kwenye Katiba kwa njia zozote zile ili
kujihakikishia kuendelea kulinda maslahi yake ya kisiasa. Wajumbe wa Bunge
Maalum Katiba wanazozana, wanakashifiana, wanatukanana na hawataki kuachana na
itikadi za kisiasa ili kufikia muafaka katika masuala muhimu
yatakayowahakikishia raia wa kawaida kushiriki kwenye fursa za maendeleo kwa
manufaa ya wote. Hayo lakini yasitukatishe tamaa na kujiona kama tu watu wa
kushindwa wakati tukiwa bado kwenye mchakato mrefu wa kujipatia jukwaa jipya
kwa mustakabali wa taifa letu Tanzania.
Tushirikiane na wote wenye nia njema kupambana
na nguvu za maovu na ubinafsi na kuachana na itikadi za kisiasa na matakwa ya
kiuchumi ya matabaka ya walio nacho ili kupigania haki za wanyonge. Tuandae
Katiba ambayo itatupatia misingi imara ya maadili itakayotuongoza kupigana
dhidi ya ubinafsi na ufisadi, na kutetea haki za binadamu kwa wote. Vigezo
vyote muhimu kwa maisha ya mshikamano kitaifa vimeandikwa katika Rasimu ya
Katiba Sura ya 1 hadi ya 5. Tukisha kukubaliana na yaliyomo katika sura hizo,
muundo wowote wa Serikali unawezekana kwa kuzingatia kanuni za uwiano wa
madaraka na wajibu wa mihimili mitatu ya Dola kwa mujibu wa Sura za 8 hadi 15.
Ili tufikie lengo letu la kuwa na Katiba bora
katika hatua tuliyofikia ya mchakato wa Katiba Mpya yatubidi kuzingatia
yafuatayo:
• Kuheshimu kazi ya Tume ya Mabadiliko ya
Katiba na kuitumia kama ilivyokusudiwa na sheria iliyoiweka.
• Kuwa na nia njema ya kweli ya kutafuta
suluhisho la matatizo mengi ya utendaji katika Dola zilizopo katika Muungano.
• Kuwa na hamu ya kujitoa kwa taifa na
kulitumikia kwa moyo bila kutawaliwa na ubinafsi au kujipendelea kiinchi na
kiukanda kwa madhumuni ya kuboresha maisha ya Watanzania wote.
• Chaguo la muundo wa Dola, sharti liongozwe na
malengo na madhumuni ya umoja wetu wa kutaka tuishi kwa mshikamano wa dhati.
Uchaguzi wa muuungano wa serikali moja, mbili au tatu sharti ufanywe kwa
dhamiri safi iliyo na uelewa uliochambua matatizo yaliyopo ya Muungano na
kuridhia mfumo utakaosuluhisha matatizo hayo pasipo mashaka yoyote.
4.Baada ya kutafakari historia ya ukombozi wa
mwanadamu kwa ufupi na hatua Watanzania tuliyofikia katika uhuru wetu wakati
huu wa adhimisho la Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo mwaka 2014, tungependa
kwa namna ya pekee kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumvuvia Rais Jakaya M.
Kikwete ujasiri wa kuamua kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania kisheria katika wakati muafaka.
Kwa mchakato huo wa Katiba, kupitia Tume yake
Huru, Watanzania wamepata fursa ya kusema kila jambo lililowaelemea maishani na
kuainisha namna wanavyotaka kujitawala. Wakati ulikuwa mwafaka kwa sababu
kulikuwa na manung’uniko mengi ya ukiukwaji wa Katiba ya sasa ambayo hayakuweza
kujibiwa na Serikali zilizopo. Hatua ya kuamua kuyakabili hayo kwa sheria ya
Kurekebisha Katiba iliwapa wananchi fursa ya kutoa maoni yao bila mizozo na
machafuko.
5.Tume ya Mabadiliko ya Katiba imewasilisha
kwenye Bunge Maalum la Katiba Rasimu ya Katiba iliyotokana na maoni huru ya
watu binafsi na makundi mbali mbali zikiwemo taasisi za dini, mamlaka za
kiserikali na asasi huru za kiraia. Tunalisihi na kulishauri Bunge Maalum la
Katiba kuheshimu mawazo yaliyowasilishwa na kutumia busara zilizopendekezwa za
kujenga muundo wa Muungano utakaokidhi mahitaji ya utangamano, mshikamano,
amani, maadili, uhuru na uwajibikaji wa viongozi na raia wa Tanzania.
HITIMISHO
Ndugu wapendwa,
Wakati huu wa Pasaka, tuendelee kuliombea Bunge Maalumu la Katiba ili wajumbe wawe wazingatifu wa matakwa na matarajio ya Watanzania yalivyoainishwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba na Tume ya mabadiliko ya Katiba kwa kuheshimu maoni ya Watanzania na kuboresha maoni hayo kwa hekima na busara ili kulinda mstakabali wa Taifa letu; Tanzania yenye amani kwa ustawi wa watu wote.
Ndugu wapendwa,
Wakati huu wa Pasaka, tuendelee kuliombea Bunge Maalumu la Katiba ili wajumbe wawe wazingatifu wa matakwa na matarajio ya Watanzania yalivyoainishwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba na Tume ya mabadiliko ya Katiba kwa kuheshimu maoni ya Watanzania na kuboresha maoni hayo kwa hekima na busara ili kulinda mstakabali wa Taifa letu; Tanzania yenye amani kwa ustawi wa watu wote.
“Ingekuwa heri leo msikie sauti hii; msifanye
migumu mioyo yenu”. (rej. Zab 95:7-8)
Tuombe:
Ee Bwana, katika upendo wako uwape neema watu
wa taifa lako, waishio Tanzania. Katika upendo wako ujenge tena nguzo za imani,
matumaini na mapendo katika mji nchi yetu. Watanzania wakiwa na imani,
matumaini na mapendo ya haki utapendezwa na sadaka wakutoleazo; kila mtu
akijitolea yeye mwenyewe kwako kama sadaka safi juu ya altare, pamoja na katika
Kristo Mfufuka aliye katika Ekaristi.
Mama Bikira Maria atuombee ili ndani yetu
uzaliwe upya uaminifu unaotupa uwezo wa kutangaza kazi kuu ya Mungu. Tunaomba
hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
Amani ya Kristo Mfufuka iwe nanyi
Ni sisi Maaskofu wenu:
1. Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Askofu wa Iringa
2. Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Dar es Salaam
3. Mhashamu Askofu Mkuu Josaphat Lebulu, Arusha
4. Mhashamu Askofu Mkuu Paul Ruzoka, Tabora/Kigoma Msimamizi
5. Mhashamu Askofu Telesphor Mkude, Morogoro
6. Mhashamu Askofu Gabriel Mmole, Mtwara
7. Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi, Ofm Cap, Mwanza,/Shinyanga
8. Mhashamu Askofu Bruno Ngonyani, Lindi
9. Mhashamu Askofu Anthony Banzi, Tanga
10. Mhashamu Askofu Agapiti Ndorobo, Mahenge
11. Mhashamu Askofu Evaristo Chengula, IMC, Mbeya
12. Mhashamu Askofu Augustino Shao, Cssp, Zanzibar
13. Mhashamu Askofu Damian Kyaruzi, Sumbawanga
14. Mhashamu Askofu Severine NiweMugizi, Rulenge-Ngara
15. Mhashamu Askofu Desiderius Rwoma, Bukoba /Singida Msimamizi
16. Mhashamu Askofu Method Kilaini, Bukoba
17. Mhashamu Askofu Damian Dallu, Geita/Askofu Mkuu Mteule Songea
18. Mhashamu Askofu Ludovick Minde, OSS, Kahama
19. Mhashamu Askofu Alfred Leonard Maluma, Njombe
20. Mhashamu Askofu Castor Paul Msemwa, Tunduru-Masasi
21. Mhashamu Askofu Beatus Kinyaiya, Ofm Cap, Mbulu
22. Mhashamu Askofu Michael Msonganzila, Musoma
23. Mhashamu Askofu Issac Amani, Moshi
24. Mhashamu Askofu Almachius Rweyongeza, Kayanga
25. Mhashamu Askofu Rogath Kimaryo, Same
26. Mhashamu Askofu Salutaris Libena, Ifakara
27. Mhashamu Askofu Eusebius Nzigilwa, Dar es Salaam
28. Mhashamu Askofu Renatus Nkwande, Bunda
29. Mhashamu Askofu Gervas Nyaisonga, Mpanda /Dodoma
30. Mhashamu Askofu Bernadin Mfumbusa, Kondoa
31. Mhashamu Askofu John Ndimbo, Mbinga
32. Mhashamu Askofu Titus Mdoe, Dar es Salaam
Ni sisi Maaskofu wenu:
1. Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Askofu wa Iringa
2. Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Dar es Salaam
3. Mhashamu Askofu Mkuu Josaphat Lebulu, Arusha
4. Mhashamu Askofu Mkuu Paul Ruzoka, Tabora/Kigoma Msimamizi
5. Mhashamu Askofu Telesphor Mkude, Morogoro
6. Mhashamu Askofu Gabriel Mmole, Mtwara
7. Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi, Ofm Cap, Mwanza,/Shinyanga
8. Mhashamu Askofu Bruno Ngonyani, Lindi
9. Mhashamu Askofu Anthony Banzi, Tanga
10. Mhashamu Askofu Agapiti Ndorobo, Mahenge
11. Mhashamu Askofu Evaristo Chengula, IMC, Mbeya
12. Mhashamu Askofu Augustino Shao, Cssp, Zanzibar
13. Mhashamu Askofu Damian Kyaruzi, Sumbawanga
14. Mhashamu Askofu Severine NiweMugizi, Rulenge-Ngara
15. Mhashamu Askofu Desiderius Rwoma, Bukoba /Singida Msimamizi
16. Mhashamu Askofu Method Kilaini, Bukoba
17. Mhashamu Askofu Damian Dallu, Geita/Askofu Mkuu Mteule Songea
18. Mhashamu Askofu Ludovick Minde, OSS, Kahama
19. Mhashamu Askofu Alfred Leonard Maluma, Njombe
20. Mhashamu Askofu Castor Paul Msemwa, Tunduru-Masasi
21. Mhashamu Askofu Beatus Kinyaiya, Ofm Cap, Mbulu
22. Mhashamu Askofu Michael Msonganzila, Musoma
23. Mhashamu Askofu Issac Amani, Moshi
24. Mhashamu Askofu Almachius Rweyongeza, Kayanga
25. Mhashamu Askofu Rogath Kimaryo, Same
26. Mhashamu Askofu Salutaris Libena, Ifakara
27. Mhashamu Askofu Eusebius Nzigilwa, Dar es Salaam
28. Mhashamu Askofu Renatus Nkwande, Bunda
29. Mhashamu Askofu Gervas Nyaisonga, Mpanda /Dodoma
30. Mhashamu Askofu Bernadin Mfumbusa, Kondoa
31. Mhashamu Askofu John Ndimbo, Mbinga
32. Mhashamu Askofu Titus Mdoe, Dar es Salaam
Saturday, April 19, 2014
How Tanzania foiled terror attack on Kenya poll
President Uhuru Kenyatta and Jakaya Kikwete of Tanzania during the 50th Jamhuri day celebrations held at Safaricom Stadium Kasarani on December 12, 2013. Tanzania helped foil terrorists attacks intended to disrupt last year’s General Election in Kenya and President Uhuru Kenyatta’s swearing-in ceremony. PHOTO| MARTIN MUKANGU ( NAIROBI)
Friday, April 18, 2014
Thursday, April 17, 2014
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Bw. Othman Masoud nae aungana na UKAWA: Asema serikali TATU hazikwepeki
Katika hali ya
kuonyesha kuwa maoni wa wana-CCM kwenye Bunge Maalumu la Katiba, yanazidi
kudhoofika kutokana na dhuluma yao kwa kufidhuli maoni na ukweli wa umma,
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Bw. Othman Masoud amewaumbua wana-CCM
wenzake na 201 waliobaki Bungeni kuwa serikali 3 ni ukweli uliopo wazi na
ndivyo hata Katiba ya sasa inavyothibitisha, na hivyo ni ngumu sana kuufunika
ukweli huo. Katiba ya sasa inazitaja wazi kuwa muungano wetu 'UNAUNDWA NA NCHI
2' na ni ngumu mno kuitaja Zanzibar bila kuonyesha nchi ya pili ni ipi, kwa
hivyo serikali 3 ni jambo lililosemwa hata katika Katiba tuliyo nayo! Kauli
liyowaacha CCM, midomo wazi, kimyaaa na kwa aibu kubwa hawakuthubutu kumzomea,
bali wameugulia mioyo, na kuguna kichinichini!
Chanzo: ITV News.
Balozi Dora Mmari Msechu; ameteuliwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na za Baltics anachukua nafasi ya Balozi Mohamed M .H. Mzale ambaye amestaafu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Mabalozi ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi na Mabalozi wastaafu kwa mujibu wa sheria.
Mabalozi wateule na aliyehamishwa kituo ni kama ifuatavyo:
1. Balozi Dora Mmari Msechu; ameteuliwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Stockholm, Sweden. Hadi uteuzi huu unafanyika Balozi Dora Mmari Msechu ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Anachukua nafasi ya Balozi Mohamed M .H. Mzale ambaye amestaafu.
2. Luteni Jenerali. Wynjones Matthew Kisamba, ameteuliwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Moscow, Urusi. Hadi uteuzi huu unafanyika, Luteni Jenerali. Wynjones Matthew Kisamba alikuwa Mkuu wa Utendaji Kivita na Mafunzo, Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Anachukua nafasi ya Balozi Jaka Mwambi.
3. Kadhalika, Mheshimiwa Rais amemteua Ndugu Joseph Edward Sokoine; kuwa Balozi na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Kabla ya uteuzi huu, Bw. Sokoine alikuwa Afisa Mambo ya Nje Mkuu na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania, Ottawa, Canada.
Imetolewa na:
(John M. Haule)
KATIBU MKUU,
WIZARA YA MAMBO YA NJE
NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM.
SEHEMU YA HOTUBA YA PROF. LIPUMBA LEO JIONI KWA NIABA YA WAJUMBE WANAOTETEA MAONI YALIYOWASILISHWA NA TUME YA KATIBA;
Profesa Ibrahim Lipumba
Mchango
wa Mjadala wa Rasimu;
Mhe. Mwenyekiti gazeti la Mwananchi la tarehe 14 Aprili 2014 limeandika kuwa “Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Ma...badiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.”
Mhe. Lukuvi aliyasema haya katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu. Hoja kama hiyo pia ilizungumzwa na Rais Kikwete wakati akilihutubia bunge Maalum tarehe 21 Machi 2014.
Ni kweli katika Rasimu ya Katiba taratibu imara za Mapato ya Serikali ya Shirikisho hazijawekwa vizuri. Serikali hiyo haina Mamlaka ya Mapato. Baada ya Rasimu ya kwanza kutolewa tatizo hilo nililichambua kwa kina katika mada niliyowasilisha katika Baraza la Katiba la TCD. Makala hii imetumiwa sana na Wajumbe wa Bunge hili. Hata hivyo wajumbe hawa hawanukuu ufumbuzi uliopendekezwa katika mada hii.
Baraza la Katiba la TCD chini ya Uenyekiti wa Augostin Lyatonga Mrema ulipendekeza muundo wa serikali tatu na utaratibu wa uchangiaji wa mapato toka serikali washirika kwa kadri mapato yanavyokusanywa na serikali washirika.
Zaidi ya asilimia 90 ya gharama za Shirikisho siyo mpya. Gharama za Rais wa Muungano za hivi sasa zitahamia kwa Rais wa Shirikisho.
Ikiwa tutakuwa na uwazi na uwajibikaji gharama hizo zitakuwa ndogo kuliko za sasa. Gharama za JWTZ, Polisi, Uhamiaji, Mambo ya nje zitahamia Serikali ya Shirikisho. Zote hizi siyo gharama mpya. Kwa sababu ya uzoefu wa “Akaunti ya Fedha ya Pamoja” na Tume ya pamoja ya Fedha, Rasimu ya Katiba haina pendekezo la kuwepo kwa chombo kinachoshirikisha serikali tatu kujadili na kukubaliana mgao wa mapato ya serikali za washirika kugharamia serikali ya Muungano.
Tume imependekeza ushuru wa bidhaa kuwa chanzo cha mapato ya kodi ya serikali ya shirikisho.Ni vyema mapato ya kugharamia serikali ya Muungano yakachangiwa na mapato ya serikali mbili.
Katiba itamke wazi serikali za washirika zitachangia sehemu ya mapato yao yote kwenye serikali ya Muungano. Kuzuia migongano ni vyema tukafikia muafaka wa asilimia ngapi ya mapato ya serikali yaende kwenye shughuli za Muungano.
Kwa kutumia uchambuzi wa gharama za Muungano uliofanywa na Tume ya Pamoja ya Fedha, gharama za Muungano ni asilimia 20 ya mapato ya Muungano. Katiba inaweza kutamka kuwa kiasi kisichopungua asilimia 20 ya mapato yote ya serikali za Washirika yatawasilishwa katika mfuko wa serikali ya Muungano kwa kadri mapato hayo yanavyokusanywa.
Izingatiwe kuwa kwa utaratibu huu bado mshirika mwenye uchumi mkubwa atakayechangia sehemu kubwa ya gharama za Muungano.
Katiba itamke kuwa Bunge la Shirikisho litatunga sheria ya kuweka utaratibu wa kuhakikisha kuwa sehemu yake ya mapato yanayokusanywa na serikali za Washirika yanawasilishwa kwenye mfuko wa Serikali ya Shirikisho.
Mamlaka ya kukusanya mapato inaweza kusimamiwa kwa pamoja kati ya serikali ya shirikisho na serikali za washirika ili kuhakikisha kuwa mapato yanayokusanywa na kuyawasilisha kwa serikali ya Washirika na serikali ya Muungano kwa uwiano uliokubaliwa.
Miaka ya 1960 na 1970 Mamlaka ya kukusanya mapato ya Afrika Mashariki ilikusanya kodi za mapato, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa Kenya, Tanganyika na Uganda na kuziwasilisha kwenye serikali husika.
Sera za kodi zilitungwa na nchi husika lakini kodi za nchi hasa ushuru wa forodha zilifanana.
Kama CCM ingekuwa na nia njema utaratibu wa kukusanya kodi na kugawa kwenye serikali ya shirikisho na serikali za washirika siyo rocket science ni jambo ambalo linaweza kuwekwa vizuri ndani ya katiba. Katiba ya muungano kama katiba mama ijenge misingi mizuri ya usimamizi wa fedha za umma na ukusanyaji wa kodi.
Mhe. Mwenyekiti, Rasimu ya Katiba imeletwa na Tume ya Rais ili tuijadili na kuipitisha. Rasimu hii siyo ya CUF, siyo ya CHADEMA, siyo NCCR Mageuzi, siyo ya Wapemba. Ni Rasimu ya Tume ya Rais Kikwete.
Katika hotuba yake katika kanisa la Methodist Mhe. Lukuvi pia alisema “Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena.”
Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.
Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.
Mhe. Mwenyekiti je lengo la serikali mbili ni kuwadhibiti Wazanzibari wasianzishe dola ya Kiislam kama alivyoeleza Mhe. Lukuvi? Baada ya hotuba ya Mhe. Lukuvi “Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano.”
Mchakato wa kupata katiba mpya unapaswa kuwa wa maridhiano, Vipi Waziri anayemuwakilisha Waziri Mkuu anaenda kanisani na kusema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.
Kama hamuitaki Rasimu ya Katiba ya Tume ya Rais kwa nini mmetuleta hapa kwa gharama kubwa. Tunaambiwa Bunge limekarabatiwa kwa shilingi bilioni 8.2. Je ni utaratibu wa 10 percent uliohamasisha kutumia fedha nyingi huku serikali ikiamini kuwa Rasimu ya Katiba haifai kabisa.
Mjadala umekuwa wa matusi na siyo wa kujenga hoja. Kauli za kibaguzi zimetolewa dhidi ya Wapemba, dhidi ya Waarabu, dhidi ya Wahindi. Wajumbe wa Bunge Maalum wanashangilia kauli za kibaguzi. Tunaanza kupanda mbegu ya intarahamwe wa Tanzania. Kauli za kibaguzi ni kinyume cha maadili na tunu za Watanzania.
Kwa utaratibu wa kanuni 33 (7), Baada ya taarifa ya kamati namba moja hadi namba kumi na mbili kuwasilishwa, taarifa hizo zitajadiliwa kwa kipindi kisichozidi siku tatu. Baada ya mjadala kamati ya uandishi inapaswa kuanda vifungu vya sura hizo mbili ili vipigiwe kura na wajumbe wa pande mbili za muungano. Hilo halitafanyika.
Kufuatana na Ratiba, Bunge Maalum litaendelea hadi tarehe 25 Aprili bila kupiga kura na kufanya maamuzi ya vifungu vya sura hizi mbili kinyume na kanuni. Bunge linaahirishwa hadi Agosti bila kufanya maamuzi ili kuwapa nafasi CCM watafute theluthi mbili ya pande zote za Muungano kwa njia yeyote ile.
Tunaopigania katiba ya wananchi hatuwezi kubariki uchakachuaji wa maoni ya wananchi. Wakati umefika tuwaache CCM muendelee na vioja vyenu kwani hamtaki kuandika katiba inayotokana na mawazo ya wananchi badala yake mnahamasisha chuki dhidi ya Wapemba, Wahindi na Waarabu na kupandikiza uhasama wa kidini.
Mhe. Mwenyekiti gazeti la Mwananchi la tarehe 14 Aprili 2014 limeandika kuwa “Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Ma...badiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.”
Mhe. Lukuvi aliyasema haya katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu. Hoja kama hiyo pia ilizungumzwa na Rais Kikwete wakati akilihutubia bunge Maalum tarehe 21 Machi 2014.
Ni kweli katika Rasimu ya Katiba taratibu imara za Mapato ya Serikali ya Shirikisho hazijawekwa vizuri. Serikali hiyo haina Mamlaka ya Mapato. Baada ya Rasimu ya kwanza kutolewa tatizo hilo nililichambua kwa kina katika mada niliyowasilisha katika Baraza la Katiba la TCD. Makala hii imetumiwa sana na Wajumbe wa Bunge hili. Hata hivyo wajumbe hawa hawanukuu ufumbuzi uliopendekezwa katika mada hii.
Baraza la Katiba la TCD chini ya Uenyekiti wa Augostin Lyatonga Mrema ulipendekeza muundo wa serikali tatu na utaratibu wa uchangiaji wa mapato toka serikali washirika kwa kadri mapato yanavyokusanywa na serikali washirika.
Zaidi ya asilimia 90 ya gharama za Shirikisho siyo mpya. Gharama za Rais wa Muungano za hivi sasa zitahamia kwa Rais wa Shirikisho.
Ikiwa tutakuwa na uwazi na uwajibikaji gharama hizo zitakuwa ndogo kuliko za sasa. Gharama za JWTZ, Polisi, Uhamiaji, Mambo ya nje zitahamia Serikali ya Shirikisho. Zote hizi siyo gharama mpya. Kwa sababu ya uzoefu wa “Akaunti ya Fedha ya Pamoja” na Tume ya pamoja ya Fedha, Rasimu ya Katiba haina pendekezo la kuwepo kwa chombo kinachoshirikisha serikali tatu kujadili na kukubaliana mgao wa mapato ya serikali za washirika kugharamia serikali ya Muungano.
Tume imependekeza ushuru wa bidhaa kuwa chanzo cha mapato ya kodi ya serikali ya shirikisho.Ni vyema mapato ya kugharamia serikali ya Muungano yakachangiwa na mapato ya serikali mbili.
Katiba itamke wazi serikali za washirika zitachangia sehemu ya mapato yao yote kwenye serikali ya Muungano. Kuzuia migongano ni vyema tukafikia muafaka wa asilimia ngapi ya mapato ya serikali yaende kwenye shughuli za Muungano.
Kwa kutumia uchambuzi wa gharama za Muungano uliofanywa na Tume ya Pamoja ya Fedha, gharama za Muungano ni asilimia 20 ya mapato ya Muungano. Katiba inaweza kutamka kuwa kiasi kisichopungua asilimia 20 ya mapato yote ya serikali za Washirika yatawasilishwa katika mfuko wa serikali ya Muungano kwa kadri mapato hayo yanavyokusanywa.
Izingatiwe kuwa kwa utaratibu huu bado mshirika mwenye uchumi mkubwa atakayechangia sehemu kubwa ya gharama za Muungano.
Katiba itamke kuwa Bunge la Shirikisho litatunga sheria ya kuweka utaratibu wa kuhakikisha kuwa sehemu yake ya mapato yanayokusanywa na serikali za Washirika yanawasilishwa kwenye mfuko wa Serikali ya Shirikisho.
Mamlaka ya kukusanya mapato inaweza kusimamiwa kwa pamoja kati ya serikali ya shirikisho na serikali za washirika ili kuhakikisha kuwa mapato yanayokusanywa na kuyawasilisha kwa serikali ya Washirika na serikali ya Muungano kwa uwiano uliokubaliwa.
Miaka ya 1960 na 1970 Mamlaka ya kukusanya mapato ya Afrika Mashariki ilikusanya kodi za mapato, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa Kenya, Tanganyika na Uganda na kuziwasilisha kwenye serikali husika.
Sera za kodi zilitungwa na nchi husika lakini kodi za nchi hasa ushuru wa forodha zilifanana.
Kama CCM ingekuwa na nia njema utaratibu wa kukusanya kodi na kugawa kwenye serikali ya shirikisho na serikali za washirika siyo rocket science ni jambo ambalo linaweza kuwekwa vizuri ndani ya katiba. Katiba ya muungano kama katiba mama ijenge misingi mizuri ya usimamizi wa fedha za umma na ukusanyaji wa kodi.
Mhe. Mwenyekiti, Rasimu ya Katiba imeletwa na Tume ya Rais ili tuijadili na kuipitisha. Rasimu hii siyo ya CUF, siyo ya CHADEMA, siyo NCCR Mageuzi, siyo ya Wapemba. Ni Rasimu ya Tume ya Rais Kikwete.
Katika hotuba yake katika kanisa la Methodist Mhe. Lukuvi pia alisema “Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena.”
Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.
Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.
Mhe. Mwenyekiti je lengo la serikali mbili ni kuwadhibiti Wazanzibari wasianzishe dola ya Kiislam kama alivyoeleza Mhe. Lukuvi? Baada ya hotuba ya Mhe. Lukuvi “Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano.”
Mchakato wa kupata katiba mpya unapaswa kuwa wa maridhiano, Vipi Waziri anayemuwakilisha Waziri Mkuu anaenda kanisani na kusema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.
Kama hamuitaki Rasimu ya Katiba ya Tume ya Rais kwa nini mmetuleta hapa kwa gharama kubwa. Tunaambiwa Bunge limekarabatiwa kwa shilingi bilioni 8.2. Je ni utaratibu wa 10 percent uliohamasisha kutumia fedha nyingi huku serikali ikiamini kuwa Rasimu ya Katiba haifai kabisa.
Mjadala umekuwa wa matusi na siyo wa kujenga hoja. Kauli za kibaguzi zimetolewa dhidi ya Wapemba, dhidi ya Waarabu, dhidi ya Wahindi. Wajumbe wa Bunge Maalum wanashangilia kauli za kibaguzi. Tunaanza kupanda mbegu ya intarahamwe wa Tanzania. Kauli za kibaguzi ni kinyume cha maadili na tunu za Watanzania.
Kwa utaratibu wa kanuni 33 (7), Baada ya taarifa ya kamati namba moja hadi namba kumi na mbili kuwasilishwa, taarifa hizo zitajadiliwa kwa kipindi kisichozidi siku tatu. Baada ya mjadala kamati ya uandishi inapaswa kuanda vifungu vya sura hizo mbili ili vipigiwe kura na wajumbe wa pande mbili za muungano. Hilo halitafanyika.
Kufuatana na Ratiba, Bunge Maalum litaendelea hadi tarehe 25 Aprili bila kupiga kura na kufanya maamuzi ya vifungu vya sura hizi mbili kinyume na kanuni. Bunge linaahirishwa hadi Agosti bila kufanya maamuzi ili kuwapa nafasi CCM watafute theluthi mbili ya pande zote za Muungano kwa njia yeyote ile.
Tunaopigania katiba ya wananchi hatuwezi kubariki uchakachuaji wa maoni ya wananchi. Wakati umefika tuwaache CCM muendelee na vioja vyenu kwani hamtaki kuandika katiba inayotokana na mawazo ya wananchi badala yake mnahamasisha chuki dhidi ya Wapemba, Wahindi na Waarabu na kupandikiza uhasama wa kidini.
Wednesday, April 16, 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)






















